Wednesday, March 8, 2023

TASAC YATOA FURSA SEKTA USAFIRISHAJI MAJINI

Na Mwandishi Wetu Dodoma

SHIRIKA la Wakala wa  Meli Tanzania (TASAC) linatoa fursa katika sekta ya usafiri majini kwa kuazisha utaratibu kwa kusajili meli kwa masharti nafuu ukarabati wa ujenzi wa meli na kuazisha maegesho ya boti ndogo katika ukanda wa Pwani, viwanda vya utengenezaji wa maligafi za ujenzi wa boti za plastiki pamoja na kujenga bandari rasmi za uvuvi.

Hayo yamesemwa na Mkurugezi Mkuu wa Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) Kaim Abdi Mkeyenge wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa majukumu ya shirika. 

Mkeyenge amesema shirika hilo limefanikiwa kuboresha ufanisi wa bandari kwa kupunguza uwezo wa shehena inayoruhusiwa kukaa bandarini kwa wakati mmoja kutoka asilimia 65 hadi asilimia 50 kwa kuweka amri ya Tozo ya Bandari Kavu ambapo wamefungua ofisi 11 za Shirika katika maeneo mbalimbali ili kusogeza huduma karibu na wananchi Shirika lina ofisi katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Mtwara, Tanga, Mwanza, Kagera, Mara, Kigoma, Rukwa, Ukerewe pamoja na Geita.

Amesema TASAC imefanikiwa kukagua meli za kigeni 36 kwa kipindi kuanzia Julai 2022 hadi Desemba 2022 na kuanzia Januari 2023 wamekagua meli za kigeni 37 ambapo shirika linategemea kukagua meli 61 hadi kufikia Juni 2023.

TASAC ilianzishwa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania, Sura 415 na kuanza rasmi kutekeleza majukumu yake tarehe 23 Februari, 2018. 

Kuundwa kwa TASAC ni hatua ya kisera ya Serikali, kwa upande wa Tanzania Bara, inayokusudia kukuza sekta za usafiri majini, kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma hususan kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Pia kuinua mchango wa usafiri kwa njia ya maji na hii ni kwa sababu Tanzania ina ukanda mkubwa wa Bahari ya Hindi wenye urefu takriban Kilomita 1,424, Maziwa makubwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa

No comments:

Post a Comment