Na John Gagarini, Kibaha
UONGOZI wa Timu ya Soka ya Simba ya
Jijini Dar es Salaam wametakiwa kuwajibika kutokana na matokeo mabaya ya timu
kwenye mashindano ya Ligi Kuu ya Voda Com iliyomalizika mwishoni mwa wiki.
Akizungumza na mwandishi wa habari
hizi mjini Kibaha msemaji wa Tawi la Simba Kibaha maarufu kama “Simba Tishio”
Fahim Lardhi alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakiwawajibisha wachezaji pale wanapofanya
vibaya hivyo na wao lazima wawajibike kwa hilo.
Lardhi alisema kuwa timu hiyo
imefanya vibaya kwenye misimu minne na kuifanya timu hiyo ishindwe kushiriki
michuano ya kimataifa kutokana na matokeo mabaya ambapo kwa msimu huu imeshika
nafasi ya tatu.
“Timu ina vitengo vingi na kamati
mbalimbali hivyo kama kuna kiongozi ambaye alizembea kwenye kitengo chake na
kufanya timu ifanye vibaya kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake anapaswa
kuwajibika kwa kuachia ngazi,” alisema Lardhi.
Alisema kuwa inasikitisha kuona timu
inafanya vibaya kila mwaka ambapo kwa mwaka huu mwenendo wake haukuwa mzuri na
kufanya timu kupata matokeo mabaya huku ikiwa imetambiwa na mtani wake Yanga kw
akufungwa michezo yote.
“Tumechoka kusemwa vibaya na watani
wetu hii ni fedheha kwetu tunaomba kiongozi yoyote ambaye alisababisha timu
kufanya anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi au kuondolewa,” alisema Lardhi.
Aidha alisema kuwa anawapongeza
wanachama na wapenzi wa timu yao kwa kuwa na uvumilivu kwani kwa kipindi cha
miaka minne timu yao imekuwa ikifanya vibaya lakini wametulia wakiamini kuwa
timu itapata matokeo mazuri lakini imekuwa kinyume.
“Ligi imeshakwisha kila kiongozi atoe
ripoti yake na kuonyesha uzaifu ulikuwa wapi ili kujipanga na msimu mwingine wa
ligi ijayo ili timu ifanye vizuri na si kushika nafasi ambazo haiipi timu
kushiriki michuano ya kimataifa,” alisema Lardhi.
Aliutaka uongozi kuwa makini katika
usajili kwa kusajili wachezaji wenye uwezo na kuacha kusajili wachezaji wasio
na uwezo kwani Simba inahitaji wachezaji wenye uwezo na si kila mchezaji
anastahili kuichezea Simba kama ilivyokuwa kwa msimu huu kuwa na wachezaji wenye
uwezo mdogo.
No comments:
Post a Comment