Thursday, May 5, 2016

MKUU WA MKOA AWATAKA WAKURUGENZI WATAKIWA KULIPA ZAWADI HEWA

Na John Gagarini, Mkuranga
MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo ametoa muda wa siku tatu hadi Mei 3 kwa wakurugenzi wa Halmashauri tatu za mkoa huo kuwapa zawadi za fedha watumishi  bora kwa mwaka huu baada ya Halmashauri hizo kutoa zawadi hewa kwenye Sherehe za siku kuu ya wafanyakazi May Mosi .
Sambamba na wakurugenzi hao wa Halmashauri pia ofisi ya Katibu Tawala mkoa (RAS) pamoja na mkurugenzi wa Shirika la Elimu nao wametakiwa kuwalipa wafanyakazi ambao walifanya vizuri kwenye vitengo vyao ambapo walipewa vyeti tu bila ya fedha kama taratibu zinavyokuwa za kuwapa fedha taslimu au hundi.
Ndikilo alitoa agizo hilo wilayani Mkuranga kwenye sherehe hizo ambazo kimkoa zilifanyika wilayani humo na kusema kuwa hayo ni masihara na yeye hayuko tayari kufanyiwa mzaha katika suala ambalo liliandaliwa kwa muda mrefu na kuwakopa zawadi hizo za fedha kwani nyingine toka mwaka jana hazijalipwa .
“Katika risala ya Shirikisho la Vyama Huru Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) mkoa wa Pwani walilalamika kuwa kumekuwa na tabia ya baadhi ya waajiri kuwakopa zawadi za fedha watumishi wanaofanya vizuri  kama motisha lakini kwa hali hili siwezi kukubaliana nalo  nawapa siku tatu muwe mmewalipa watumishi hao vinginevyo atakayeshindwa aje ofisini kwangu akutane na adhabu niliyoiandaa,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa hawezi kuvumilia watu wazembe wanaofanya dharau kwenye mambo mazito na kwamba atachukua hatua kali kwa Halmashauri ambazo zitashindwa kutoa zawadi hizo kwani zingene zimetoa kwanini wengine washindwe.
“Mimi siyo mtani wenu wala si saizi yenu haiwezekani mniite nije kutoa zawadi hewa ndo maana hatoa zikichukuliwa za kinidhamu mnasema mnaonewa ikifika Jumatano muwe mmeshawapa zawadi zao wahusika huu ni mzaha umepitiliza kiwango anayedhani tunatania aendelee aone,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema kuwa ameshangazwa na kitendo hicho cha wao kumfanya atoe zawadi hewa kwani hiyo ni dharau Ras Pwani, Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Halmashauri ya Mji Kibaha, Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji na Mkurugenzi wa Shirika la Elimu Kibaha.
“Hatutaniani hapa huu ni mzaha uliopitiliza kiwango ujumbe umefika namna hii mnakatisha tamaa watumishi kwa kudai kuwa mchakato bado ni jambo ambalo halijanifurahisha na nisingependa hali hii isijitokeze tena,” alisema Ndikilo.
Awali akisoma risala ya TUCTA Amini Msambwa alisema kuwa wafanyakazi wana haki ya kutimiziwa haki zao za msingi na siyo lazima zipatikane kwa shinikizo la maandamano, migomo na hata kufungia nje waajiri.
Msambwa alisema kuwa moja ya changamoto ni baadhi ya wawekezaji wa nje na wandani kuwanyima fursa wafanyakazi kujiunga na vyama vyao sehemu za kazi ambayo ni haki yao ya kisheria na kwa kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu ya Dhana ya Mabadiliko ilenge kuinua hali za wafanyakazi.
Aidha wameomba Halmashauri kuruhusu kuwa na mabaraza ya wafanyakazi na ambako yako yakutane kwenye vikao vyao vya kisheria lakini yanafanyika kwa ajili ya kupitisha bajeti za halmashauri.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment