Monday, May 23, 2016

MABILIONI YATENGWA SEKTA YA ELIMU KIBAHA

Na John Gagarini, Kibaha
KATIKA kukabiliana na changamoto za elimu  wilaya ya  Kibaha mkoani Pwani imetenga bajeti ya shilingi bilioni 1,789,828,891 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa shule za sekondari kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba na kusema kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kupunguza changamoto mbalimbali kwenye shule za sekondari wilayani humo.
Kihemba amesema kuwa kabla ya bajeti hiyo kupitishwa jumlaya shilingi milioni 640,424,679 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika shule za sekondari za Zogowale na Hosteli ya shule ya sekondari ya Pangani.
Amesema kuwa pia fedha hizo zimetumika katika ujenzi wa matundu 20 ya vyoo, madarasa matano na nyumba moja ya mwalimu katika shule za sekondari za Pangani, Simbani na Ruvu Station.
Akizungumzia upande wa shule za msingi amesema kuwa katika bajeti hiyo zimetengwa kiasi cha shilingi milioni 943,144,394 kwa ajili ya miradi ya maendeleo  kwa elimu ya msingi.
Aidha amesema kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ya 2015/ 2016 wilaya ilipokea kiasi cha shilingi milioni 140,254, 154 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya mwalimu Kumba, vyumba 9 vya vya madarasa katika shule za Visiga, Lumumba, Bamba na Matuga.
Amebainisha kuwa fedha hizo pia zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo na ununuzi wa madawati 46, meza 4 na viti 6 kwa ajili ya shule ya Msingi ya Matuga.

No comments:

Post a Comment