Na John Gagarini, Kibaha
ASKARI wa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani mwenye namba F.1839 sajent (SGT) Ally Salum maarufu Kinyogori ameuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake.
>
> Tukio hilo limetokea may 19,majira ya saa 1.30 usiku huko katika kijiji cha Chatembo kata ya Mwandege wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
>
> Kamanda wa polisi mkoani hapo,Boniventure Mushongi,amesema katika hali isiyo ya kawaida watu wawili wakiwa wamevalia makoti meusi na nyuso zao wakiwa wamezificha kwa mask walifanya mauaji hayo na kutokomea.
>
> Amesema watu hao waliingia ndani ya uzio wa nyumba ya askari huyo wakitumia usafiri wa pikipiki aina ya boxer na baada ya kushuka kwenye pikipiki waliingia ndani na kumfyatulia risasi askari huyo kichwani pamoja na ubavuni na kumpotezea maisha yake.
>
> Kamanda Mushongi amesema katika tukio hilo wauaji hao hawakuchukua kitu chochote zaidi ya funguo wa gari la marehemu ambapo waliondoka nalo.
>
> Amesema msako mkali wa kuwasaka waliohusika na tukio unaendelea na ameomba ushirikiano kutoka kwa wananchi kwa wale wenye taarifa zitakazosaidia kuwapata wahusika hao.
>
> Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital ya Temeke na utakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi mara baada ya kufanyiwa uchunguzi .
>
> Mwisho
>
> Tukio hilo limetokea may 19,majira ya saa 1.30 usiku huko katika kijiji cha Chatembo kata ya Mwandege wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
>
> Kamanda wa polisi mkoani hapo,Boniventure Mushongi,amesema katika hali isiyo ya kawaida watu wawili wakiwa wamevalia makoti meusi na nyuso zao wakiwa wamezificha kwa mask walifanya mauaji hayo na kutokomea.
>
> Amesema watu hao waliingia ndani ya uzio wa nyumba ya askari huyo wakitumia usafiri wa pikipiki aina ya boxer na baada ya kushuka kwenye pikipiki waliingia ndani na kumfyatulia risasi askari huyo kichwani pamoja na ubavuni na kumpotezea maisha yake.
>
> Kamanda Mushongi amesema katika tukio hilo wauaji hao hawakuchukua kitu chochote zaidi ya funguo wa gari la marehemu ambapo waliondoka nalo.
>
> Amesema msako mkali wa kuwasaka waliohusika na tukio unaendelea na ameomba ushirikiano kutoka kwa wananchi kwa wale wenye taarifa zitakazosaidia kuwapata wahusika hao.
>
> Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital ya Temeke na utakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi mara baada ya kufanyiwa uchunguzi .
>
> Mwisho
No comments:
Post a Comment