Na John Gagarini, Mkuranga
WAKAZI wa mkoa wa Pwani wametakiwa
kuunga mkono mkakati wa serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk John
Magufuli ya kuhamasisha ujenzi wa viwanda na uwekezaji.
Akizungumza na wakazi wa vijiji vya
Nyamato na Mkiu wilayani Mkuranga wakati alipotembelea kiwanda cha kutengeneza
vigae (Tiles) cha Goodwill Tanzania Ceramic mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia
Evarist Ndikilo alisema kuwa wananchi wananafasi kubwa ya kufanikisha nchi kuwa
ya viwanda kwa kushirikiana na wamiliki wa viwanda.
Ndikilo alisema kuwa wananchi wanapaswa
kuwapa ushirikiano wawekezaji wa viwanda ili waweze kufanya kazi bila ya
kuhujumiwa kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa wakihujumu miundombinu ya
viwanda.
“Wawekezaji kama hawa wa viwanda
mnapaswa kuwaunga mkono kwani manufaa ya uwepo wao ni mengi sana ikiwa ni
pamoja na kupata ajira pamoja na nyie kuuza bidhaa zenu kwani biashara zitakuwa
nyingi hivyo mtaweza kubadilisha maisha yenu lakini endapo mtawafanyia vitendo
vya kuwakatisha tama wataondoka,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa kwa sasa mkoa wa Pwani
ajenda yake ni kuhakikisha unakuwa mkoa wa viwanda na hilo linawezekana kwa
kuwa na viwanda vingi vya kuzalisha bidhaa mbalimbali.
“Mkoa kwa sasa umeamua kujitangaza
kiviwanda kwnai nafasi za uwekezaji bado zipo nyingi na lengo ni kuhakikisha
wananchi wanakuwa na uchumi wa kati na utainuka endapo kutakuwa na viwanda
vingi mfano tu wilaya ya Mkuranga mmeanza kutekeleza kwa vitendo mkakati wa
Rais wa kuwa na viwanda kwnai kwa sasa kuna viwanda 59,” alisema Ndikilo.
Aliwataka wakurugenzi na wakuu wa
wilaya za mkoa huo kuhakikisha wanatenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji na
kuhamasisha wageni na wazawa kujenga viwanda ili kuinua uchumi wa wananchi
lakini wahakikishe wawekezaji wan je wanafuata taratibu za nchi kwa wafanyakazi
kwa kuzingatia sheria za kazi.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa
kiwanda hicho Yang Zhen alisema kuwa kiwanda hicho ni cha pekee kwani kitakuwa
cha pili barani Afrika kwa ukubwa na cha kwanza Tanzania kwa uzalishaji wa
vigae ambapo kwa siku kitakuwa kikizalisha meta 80,000 kwa siku.
Zhen alisema kuwa maradi huo una
thamani ya dola za Kimarekani 100 na umegawanyika kwenye hatua mbili ambapo
awamu hii ya kwanza itaisha mwishoni mwa mwaka huu huku ile ya pili ikiisha
mwishoni mwa mwakani hivyo bidhaa hizo za vigae zitakuwa zikizalishwa hapahapa
na siyo nje ya nchi.
Aidha alisema kuwa wanatarajia kujenga
shule, kuwapatia maji, zahanati pamoja na kituo cha polisi ikiwa ni kama
mchango wao kwa jamii inayozunguka kiwanda hicho ambapo mara kitakapokamilika
kitaajiri watu 2,000 na kwa sasa kimetoa ajira kwa watu 200.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment