Sunday, May 29, 2016

POLISI WATUMIA VIPIMA ULEVI KUDHIBITI AJALI PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
KITUO cha Afya cha Mkoani kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Jenereta ili kukabiliana na tatizo la ukatikaji umeme kwenye chumba cha akinamama wanapojifungulia hivyo kuwaomba wadau mbalimbali.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Happiness Ndosi wakati akipokea msaada wa vifaa mbalimbali kwa watoto waliozaliwa na watakaozaliwa kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali la Abubaker Darwesh International Charitable Foundation (ADICF) la Jijini Dar es Salaam.
Dk Ndosi alisema kuwa kukatika kwa umeme kwenye kituo hicho ni changamoto kubwa hasa nyakati za usiku na wakati mama wajawazito wanapokuwa wanajifungua hali ambayo inahatarisha maisha ya akinamama hao.
“Kutokana na hali hiyo tunawaomba wadau mbalimbali wajitokeze kutusaidia kupata jenereta kwa ajili ya kusaidia mara umeme unapokatika katika chumba cha uzalishaji mama wajawazito ili kunusuru maisha yao,” alisema Dk Ndosi.
Aidha alisema mbali ya changamoto hiyo pia wanakabiliwa na changamoto nyingine ikiwa ni pamoja na ukosefu wa chumba cha upasuaji, Ultra Sound na X-Ray, gari la wagonjwa kwani lililopo ni chakavu, magodoro na vitanda hasa ikizingatiwa kuwa kituo hicho kiko mbioni kuwa Hospitali ya Wilaya.
Kwa upande wake mwanzilishi na meneja mradi wa shirika hilo Bilal Abubekar alisema kuwa shirika lake limeamua kutoa misaada hiyo kwa lengo la kuisaidia jamii hasa kwa watoto wadogo wenye umri chini ya miaka mitano ili kuisaidia serikali kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanapata huduma bora.
Abubaker alisema kuwa shirika lao limekuwa likisaidia makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wajane yatima na watu wenye mahitaji, pia kusaidia elimu watu wenye ulemavu.
Naye moja ya wagonjwa waliopata msaada huo Mariamu Ally alishukuru shirika hilo na kusema kuwa wameonyesha moyo wa upendo na kuwataka waendelee kusaidia hospitali hiyo ili iweze kukabiliana na changamoto zilizopo kwa wagonjwa.
Alisema kuwa moja ya changamoto iliyopo kwenye wodi hiyo ni kuchanganywa kati ya akinamama waliojifungua na wale wanaosubiri kujifungua na kutaka watu hao kutenganishwa ili kila moja wawe na sehemu yao.
Mwisho.   
Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza kata ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.  
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
BAADHI ya wakazi kwneye eneo la Sagulasagula maarufu kama Loliondo Mtaa wa Machinjioni kata ya Tangini wilayani Kibaha mkoani Pwani wanaodaiwa kuvamia eneo lililotengwa kwa ajili ya soko wameiomba Halmashauri ya Mji kuwalipa fidia na maeneo ya kuishi baada ya kupewa siku 14 kuhama kwenye eneo hilo.
Wakizungumza mara baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya kupitia na kuangalia eneo hilo na kutoa maagizo kwa wakazi hao kubomoa nyumba zipatazo 55 zilizojengwa kwenye eneo hilo walisema kuwa kwa kuwa ni mpango wa maendeleo basi nao waangaliwe kwani wamekaa hapo kwa muda mrefu.
Said Tekelo alisema kuwa baadhi ya watu wako hapo tangu mwaka 1970 na mwaka 2003 Rais Benjamin Mkapa wakati ule alifuta hati ya eneo hilo toka eneo la Viwanda na kutaka lirejeshwe kwenye mtaa kwa ajili ya matumizi mengine.
“Baada ya kurejeshwa kwenye mtaa baadhi ya watu walipimiwa maeneo yao baada ya kupigwa picha na kamahaitoshi hata alipokuja waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitoa miezi mitatu sasa sita Halmashauri ikae na wakazi hao ili kujadili namna nzuri ya kufanya,” alisema Tekelo.
Alisema kuwa licha ya maagizo hayo walikwenda Mahakamani kwenda kulalamika walipotakiwa kuondoka na kesi iliendeshwa na wao kushindwa na Mahakama ili amuru Halmashauri ikae nao lakini hakuna kilichofanyika hadi mwishoni mwa wiki walipotakiwa kuvunja wenyewe na endapo hawatafanya hivyo Halmashauri itabomoa nyumba hizo.
“Tumeambiwa tubomoe wenywe na kuanzia leo Tanesco na Dawasco wameshapewa maagizo ya kuondoa miundombinu yao ilkiwa ni maandalizi ya kubomoa sisi tunaomba Halmashauri itufikirie kwa kutulipa fidia pamoja na maeneo kwa ajili ya kuishi kwani wenzetu jirani ambao tuko kwenye mgogoro mmoja wamelipwa na kupewa viwanja,” alisema Tekelo.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Tangini Theodori Joseph alisema kuwa suala hilo ni la muda mrefu ambapo baraza la Madiwani miaka ya nyuma waliwatambua wakazi hao kutaka walipwe fidia na walikuwa wakishirikiana nao katika mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchukua kodi za majengo.
Joseph alisema kuwa kuna haja ya Halmashauri kuwafikiria wakazi hao kwani wengine wako hapo miaka 40 iliyopita na wameendeleza ardhi kwa kipindi chote hicho lakini jirani zao ambao wametengwa na barabara wao  wamepewa fidia na watapewa viwanja.
Ofisa Habari wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Inocent Byarugaba alisema kuwa eneo hilo lilitengwa kwa ajili ya soko na liko kwenye Ramani ya Mji na  wakazi hao walilivamia eneo hilo na wanapaswa kuliachia.
Byarugaba alisema kuwa tayari eneo hilo liko kwenye maandalizi ya ujenzi wa soko unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani tayari ramani imeshatoka ambapo soko linalotumika kwa sasa liko kwenye hifadhi ya barabara na litabomolewa muda wowote na Tanroads.
Naye kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Lucy Kimoi alisema kuwa wakazi hao wanapaswa kuondoka na kwa sasa wanaandaa notisi kwa ajili ya kuwataka waliachie eneo hilo kwani wako hapo kinyume cha Sheria.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
HALMASHAURI ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani imetenga kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 990 kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisasa kwenye eneo la mnada wa kila wiki  maarufu kama Sagulasagula au Loliondo kwa ajili ya wakazi wa mji huo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha ofisa habari wa Halmashauri hiyo Inocent Byarugaba alisema kuwa soko hilo litachukua wafanyabiashara wapatao 286 ambao walikuwa kwenye soko la zamani la Maili Moja ambalo linatarajiwa kubomolewa.
Byarugaba alisema kuwa lengo la kujenga soko hilo kubwa na la kisasa ni kutaka kuwarahisishia wananchi kupata huduma bora badala ya kukimbilia kwenye maosko makubwa kama vile la Kariakoo Jijini Dar es Salaam.
“Tutajenga kwa kushirikiana na wananchi kwa mtindo wa jenga, endesha na rudisha  (BOT) ambapo watajenga kwa mkataba maalumu ambao utakuwa na manufaa kwa pande zote mbili,” alisema Byarugaba.
Alisema kuwa ujenzi huo wa soko hilo utahusisha maduka ya jumla na rejareja, sehemu ya kuuzia mazao ya nafaka, samaki, mabucha ya nyama 10, mbogamboga, sehemu ya kuchinjia kuku, matunda na sehemu ya kupaki magari.
“Lengo ni kuwa na huduma bora ya soko kwani lililopo lilikuwa ni dogo na halikuwa na huduma nyingi kutokana na ufinyu wake na mabanda yake yalijengwa kwa muda kutokana na kuwa kwenye hifadhi ya barabara ambapo wenywe wanalitaka eneo lao kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo,” alisema Byarugaba.
Aidha alisema kuwa ujenzi wa soko hilo unatarajiwa kuanza wakati wowote kwani tayari ramani imeshachorwa kinachosubiriwa ni taratibu chache zilizosalia ili kuanza kazi.
Mwisho.   
Na John Gagarini, Kibaha
MADEREVA wa mabasi ya abiria yanayopita mkoani Pwani wametakiwa kuacha tabia ya kutumia vilevi ikiwemo pombe ili kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikileta madhara na uharibifu wa mali ulemavu na kupoteza maisha ya abiria wanaowasafirisha.
Hayo yamesemwa na mwalimu wa kufundisha matumizi ya vifaa vya kupima ulevi wa Jeshi la Polisi mkoani humo Aisha Sudi na kusema kuwa moja ya vyanzo vikuu vya ajali vinatokana na ulevi hususani ule wa pombe.
Sudi amesema kuwa dereva wa basi hapaswi kabisa kutumia pombe pale anapokuwa akiendesha gari licha ya kuwa ulevi chini asilimia 80 ni wa kawaida ila unapozidi zaidi ya hapo ni hatari kwa uendeshaji wa gari.
Amesema kuwa wanapowapima na kuwabaini wana vilevi hawaruhusiwi kuendesha basi na kutakiwa kubadilisha dereva ili kuendelea na safari na hali hiyo imesababisha kupungua kwa ajali katika mkoa huo.
Aidha amesema kuwa hufikia kuyakagua mabasi hayo baada ya kupata taarifa toka kwa abiria ambao wanaangalia mwenendo wa dereva au wanapomtilia shaka dereva wa basi na anapobainika kutumia kilevi anapelekwa mahakamani kwa hatua zaidi.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani humo Abdi Issango amesema kuwa vifaa hivyo vinatumika kwenye maeneo mbalimbali kwenye barabara za kwenda mikoa jirani ya Tanga, Morogoro na Lindi.
Issango ametaja maeneo ambapo kuna askari wanaotumia hivyo vifaa kuwa ni pamoja na Maili Moja, Mlandizi, Vigwaza, Chalinze, Mdaula, Wami Mbwewe, Mapinga, Kiwangwa, Vikindu, MKuranga, Kimazinchana na Kibiti.
Amesema kuwa kutokana na Jeshi la Polisi kuweka mikakati mbalimbali ya kuzuia ajali katika kipindi cha Januari hadi Aprili hakuna ajali kubwa ya basi iliyosababisha vifo kwani nyingi ni zile ndogondogo ambazo hazina madhara makubwa.
Amebainisha kuwa ajali zinazoleta madhara kwa sasa ni za pikipiki kutokana na madereva wengi wa bodaboda kutozingatia sheria za usalama barabarani ambapo wengi hawana leseni kwani biashara hiyo ilianza bila ya utaratibu ambapo kwa sasa wanaendelea kuwapatia elimu ili waendeshe vyombo hivyo kwa kuzingatia sheria.
Mwisho.       


  
  



WAIOMBA HALMASHAURI IWALIPE FIDIA BAADA YA KUPEWA SIKU 14 KUVUNJA NYUMBA ZAO

Na John Gagarini, Kibaha
BAADHI ya wakazi kwneye eneo la Sagulasagula maarufu kama Loliondo Mtaa wa Machinjioni kata ya Tangini wilayani Kibaha mkoani Pwani wanaodaiwa kuvamia eneo lililotengwa kwa ajili ya soko wameiomba Halmashauri ya Mji kuwalipa fidia na maeneo ya kuishi baada ya kupewa siku 14 kuhama kwenye eneo hilo.
Wakizungumza mara baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya kupitia na kuangalia eneo hilo na kutoa maagizo kwa wakazi hao kubomoa nyumba zipatazo 55 zilizojengwa kwenye eneo hilo walisema kuwa kwa kuwa ni mpango wa maendeleo basi nao waangaliwe kwani wamekaa hapo kwa muda mrefu.
Said Tekelo alisema kuwa baadhi ya watu wako hapo tangu mwaka 1970 na mwaka 2003 Rais Benjamin Mkapa wakati ule alifuta hati ya eneo hilo toka eneo la Viwanda na kutaka lirejeshwe kwenye mtaa kwa ajili ya matumizi mengine.
“Baada ya kurejeshwa kwenye mtaa baadhi ya watu walipimiwa maeneo yao baada ya kupigwa picha na kamahaitoshi hata alipokuja waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitoa miezi mitatu sasa sita Halmashauri ikae na wakazi hao ili kujadili namna nzuri ya kufanya,” alisema Tekelo.
Alisema kuwa licha ya maagizo hayo walikwenda Mahakamani kwenda kulalamika walipotakiwa kuondoka na kesi iliendeshwa na wao kushindwa na Mahakama ili amuru Halmashauri ikae nao lakini hakuna kilichofanyika hadi mwishoni mwa wiki walipotakiwa kuvunja wenyewe na endapo hawatafanya hivyo Halmashauri itabomoa nyumba hizo.
“Tumeambiwa tubomoe wenywe na kuanzia leo Tanesco na Dawasco wameshapewa maagizo ya kuondoa miundombinu yao ilkiwa ni maandalizi ya kubomoa sisi tunaomba Halmashauri itufikirie kwa kutulipa fidia pamoja na maeneo kwa ajili ya kuishi kwani wenzetu jirani ambao tuko kwenye mgogoro mmoja wamelipwa na kupewa viwanja,” alisema Tekelo.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Tangini Theodori Joseph alisema kuwa suala hilo ni la muda mrefu ambapo baraza la Madiwani miaka ya nyuma waliwatambua wakazi hao kutaka walipwe fidia na walikuwa wakishirikiana nao katika mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchukua kodi za majengo.
Joseph alisema kuwa kuna haja ya Halmashauri kuwafikiria wakazi hao kwani wengine wako hapo miaka 40 iliyopita na wameendeleza ardhi kwa kipindi chote hicho lakini jirani zao ambao wametengwa na barabara wao  wamepewa fidia na watapewa viwanja.
Ofisa Habari wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Inocent Byarugaba alisema kuwa eneo hilo lilitengwa kwa ajili ya soko na liko kwenye Ramani ya Mji na  wakazi hao walilivamia eneo hilo na wanapaswa kuliachia.
Byarugaba alisema kuwa tayari eneo hilo liko kwenye maandalizi ya ujenzi wa soko unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani tayari ramani imeshatoka ambapo soko linalotumika kwa sasa liko kwenye hifadhi ya barabara na litabomolewa muda wowote na Tanroads.
Naye kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Lucy Kimoi alisema kuwa wakazi hao wanapaswa kuondoka na kwa sasa wanaandaa notisi kwa ajili ya kuwataka waliachie eneo hilo kwani wako hapo kinyume cha Sheria.
Mwisho.

KITUO CH AFYA MKOANI CHAHITAJI JENERETA

Na John Gagarini, Kibaha
KITUO cha Afya cha Mkoani kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Jenereta ili kukabiliana na tatizo la ukatikaji umeme kwenye chumba cha akinamama wanapojifungulia hivyo kuwaomba wadau mbalimbali.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Happiness Ndosi wakati akipokea msaada wa vifaa mbalimbali kwa watoto waliozaliwa na watakaozaliwa kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali la Abubaker Darwesh International Charitable Foundation (ADICF) la Jijini Dar es Salaam.
Dk Ndosi alisema kuwa kukatika kwa umeme kwenye kituo hicho ni changamoto kubwa hasa nyakati za usiku na wakati mama wajawazito wanapokuwa wanajifungua hali ambayo inahatarisha maisha ya akinamama hao.
“Kutokana na hali hiyo tunawaomba wadau mbalimbali wajitokeze kutusaidia kupata jenereta kwa ajili ya kusaidia mara umeme unapokatika katika chumba cha uzalishaji mama wajawazito ili kunusuru maisha yao,” alisema Dk Ndosi.
Aidha alisema mbali ya changamoto hiyo pia wanakabiliwa na changamoto nyingine ikiwa ni pamoja na ukosefu wa chumba cha upasuaji, Ultra Sound na X-Ray, gari la wagonjwa kwani lililopo ni chakavu, magodoro na vitanda hasa ikizingatiwa kuwa kituo hicho kiko mbioni kuwa Hospitali ya Wilaya.
Kwa upande wake mwanzilishi na meneja mradi wa shirika hilo Bilal Abubekar alisema kuwa shirika lake limeamua kutoa misaada hiyo kwa lengo la kuisaidia jamii hasa kwa watoto wadogo wenye umri chini ya miaka mitano ili kuisaidia serikali kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanapata huduma bora.
Abubaker alisema kuwa shirika lao limekuwa likisaidia makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wajane yatima na watu wenye mahitaji, pia kusaidia elimu watu wenye ulemavu.
Naye moja ya wagonjwa waliopata msaada huo Mariamu Ally alishukuru shirika hilo na kusema kuwa wameonyesha moyo wa upendo na kuwataka waendelee kusaidia hospitali hiyo ili iweze kukabiliana na changamoto zilizopo kwa wagonjwa.
Alisema kuwa moja ya changamoto iliyopo kwenye wodi hiyo ni kuchanganywa kati ya akinamama waliojifungua na wale wanaosubiri kujifungua na kutaka watu hao kutenganishwa ili kila moja wawe na sehemu yao.
Mwisho.   


Thursday, May 26, 2016

MWENYEKITI AKATALIWA KWENYE MKUTANO

Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.   

Mwisho.   

MWENYEKITI AKATALIWA KWENYE MKUTANO

Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.   

Mwisho.   

Monday, May 23, 2016

KIBAHA YAKAMATA KILOGRAMU 441 ZA DAWA ZA KULEVYA

Na John Gagarini, Kibaha

WILAYA ya Kibaha mkoani Pwani imefanikiwa kukamata madawa ya kulevya yenye uzito wa kilogramu 441.6 katika kipindi cha mwaka 2015 / 2016.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha ambaye pia ni wenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya amesema kuwa katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya kipindi cha mwaka 2015/ 2016 wamefanikiwa kukamata dawa zenye uzito wa kilogramu 441.65.

Kihemba amesema kuwa kati ya hizo Cocain na Heroin ni kilo 6.1, Bhangi kilo 418,mirungi kilo 17.5 ambapo jumla ya kesi 153 zimefunguliwa kwenye kituo cha Polisi cha wilaya ya Kibaha.

Amesema kuwa kesi zilizopelekwa mahakamani ni 132 na zilizo kwenye upelelezi ni 21 ambapo kesi za Bhangi na Mirungi zilizo kwisha mahakamani ni 57. 

aidha amesema kuwa jumla ya watuhumiwa ambao walikamatwa na bangi na mirungi ni 163 wanawake wakiwa ni 28 na wanaume ni 135 na wilaya inaendelea kutoa elimu ili watu waepukane na dawa za kulevya.


Mwisho.       

MABILIONI YATENGWA SEKTA YA ELIMU KIBAHA

Na John Gagarini, Kibaha
KATIKA kukabiliana na changamoto za elimu  wilaya ya  Kibaha mkoani Pwani imetenga bajeti ya shilingi bilioni 1,789,828,891 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa shule za sekondari kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba na kusema kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kupunguza changamoto mbalimbali kwenye shule za sekondari wilayani humo.
Kihemba amesema kuwa kabla ya bajeti hiyo kupitishwa jumlaya shilingi milioni 640,424,679 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika shule za sekondari za Zogowale na Hosteli ya shule ya sekondari ya Pangani.
Amesema kuwa pia fedha hizo zimetumika katika ujenzi wa matundu 20 ya vyoo, madarasa matano na nyumba moja ya mwalimu katika shule za sekondari za Pangani, Simbani na Ruvu Station.
Akizungumzia upande wa shule za msingi amesema kuwa katika bajeti hiyo zimetengwa kiasi cha shilingi milioni 943,144,394 kwa ajili ya miradi ya maendeleo  kwa elimu ya msingi.
Aidha amesema kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ya 2015/ 2016 wilaya ilipokea kiasi cha shilingi milioni 140,254, 154 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya mwalimu Kumba, vyumba 9 vya vya madarasa katika shule za Visiga, Lumumba, Bamba na Matuga.
Amebainisha kuwa fedha hizo pia zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo na ununuzi wa madawati 46, meza 4 na viti 6 kwa ajili ya shule ya Msingi ya Matuga.

VIONGOZI SIMBA WAWAJIBIKE


Na John Gagarini, Kibaha

UONGOZI wa Timu ya Soka ya Simba ya Jijini Dar es Salaam wametakiwa kuwajibika kutokana na matokeo mabaya ya timu kwenye mashindano ya Ligi Kuu ya Voda Com iliyomalizika mwishoni mwa wiki.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha msemaji wa Tawi la Simba Kibaha maarufu kama “Simba Tishio” Fahim Lardhi alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakiwawajibisha wachezaji pale wanapofanya vibaya hivyo na wao lazima wawajibike kwa hilo.

Lardhi alisema kuwa timu hiyo imefanya vibaya kwenye misimu minne na kuifanya timu hiyo ishindwe kushiriki michuano ya kimataifa kutokana na matokeo mabaya ambapo kwa msimu huu imeshika nafasi ya tatu.

“Timu ina vitengo vingi na kamati mbalimbali hivyo kama kuna kiongozi ambaye alizembea kwenye kitengo chake na kufanya timu ifanye vibaya kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi,” alisema Lardhi.

Alisema kuwa inasikitisha kuona timu inafanya vibaya kila mwaka ambapo kwa mwaka huu mwenendo wake haukuwa mzuri na kufanya timu kupata matokeo mabaya huku ikiwa imetambiwa na mtani wake Yanga kw akufungwa michezo yote.

“Tumechoka kusemwa vibaya na watani wetu hii ni fedheha kwetu tunaomba kiongozi yoyote ambaye alisababisha timu kufanya anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi au kuondolewa,” alisema Lardhi.

Aidha alisema kuwa anawapongeza wanachama na wapenzi wa timu yao kwa kuwa na uvumilivu kwani kwa kipindi cha miaka minne timu yao imekuwa ikifanya vibaya lakini wametulia wakiamini kuwa timu itapata matokeo mazuri lakini imekuwa kinyume.

“Ligi imeshakwisha kila kiongozi atoe ripoti yake na kuonyesha uzaifu ulikuwa wapi ili kujipanga na msimu mwingine wa ligi ijayo ili timu ifanye vizuri na si kushika nafasi ambazo haiipi timu kushiriki michuano ya kimataifa,” alisema Lardhi.

Aliutaka uongozi kuwa makini katika usajili kwa kusajili wachezaji wenye uwezo na kuacha kusajili wachezaji wasio na uwezo kwani Simba inahitaji wachezaji wenye uwezo na si kila mchezaji anastahili kuichezea Simba kama ilivyokuwa kwa msimu huu kuwa na wachezaji wenye uwezo mdogo.

Mwisho.

VIJANA WAILILIA SERIKALI KUWAINUA KIUCHUMI

Na John Gagarini, Kisarawe

SERIKALI imeombwa kusaidia vikundi vya vijana vinavyopata mafunzo mbalimbali ya kuwainua kiuchumi ili waweze kujiajiri wakiwa Vijijini badala ya kukimbilia Mijini.

Akisoma risala ya wahitimu mbele ya mgeni rasmi ambaye ni kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa George Mbijima kwenye Kijiji cha Kibuta wilayani Kisarawe, Mariam Christopher alisema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha kuweza kukabili mazingira wanayoishi huko huko waliko kuliko kukimbilia mjini kutafuta ajira.

Christopher alisema kuwa masomo waliyojifunza ni ya ufundi kwa vijana wa kata ya Kurui kupitia mradi wa kuwajengea uwezo vijana (YEE) unaosimamiwa na shirika lisilokuwa la kiserikali Plan International wilaya ya Kisarawe.

“Tunashukuru wafadhili wetu kwani tumeweza kujifunza mambo mengi ya ufundi tunaamini yatatusaidia tukiwa huku huku bali kikubwa ni Halmashauri kutuwekea mazingira mazuri ya kufanya kazi ili tuisaidie jamii ya Kijijini hasa ikizingatiwa nako kuna hitaji maendeleo,” alisema Christopher.

Alisema kuwa mafunzo hayo wameyapata kwa kina katika fani mbalimbali za upambaji, mapishi, udereva, ushonaji na utengenezaji wa mapambo na wanatarajia kuboresha shughuli hizo Vijijini ili kuleta maendeleo kwa familia zao na wao binafsi.

Aidha alisema kuwa mafunzo hayo yanafadhiliwa na Eu, Vso, Uhiki, Veta na Plan International wilayani humo na yanatekelezwa kwenye kata Sita za Kibuta, Kisarawe, Manerumango, Msimbu, Kurui na Marumbo na yanatarajiwa kuwafikia vijana 1,000 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kwa upande wa kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa George Mbijima alisema kuwa Halmashauri inapaswa kuwatengenea vijana asilimia tano ya mapato yao kwa ajili ya kuwakopesha vijana kwani suala hilo liko kisheria na wanapaswa kutekeleza ili kuwajenga vijana kiuchumi, Mwenge huo leo unatarajiwa kukimbizwa wilaya ya Rufiji.

Mwisho. 





SERIKALI KUWAWEKEA MAZINGIRA MAZURI WAWEKEZAJI

Na John Gagarini, Kisarawe
SERIKALI itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wa ndani na nje ambao watafuata taratibu za nchi ili kuongeza pato la taifa kupitia sekta ya uwekezaji ambayo kwa sasa inakuwa kwa kasi kwenye mikoa mbalimbali.
Hayo yalisemwa na kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa George Mbijima alipokuwa akiweka jiwe la msingi kwenye Bandari ya Nchi Kavu inayojengwa kwenye Kijiji cha Kazimzumbwi wilayani Kisarawe mkoani Pwani.
Mbijima alisema kuwa nchi kwa sasa iko kwenye kipindi cha utekelezaji  kwa vitendo sera ya uwekezaji ili iweze kuleta manufaa kwa wananchi pamoja na serikali ili iweze kuwaletea maendeleo wananchi kupitia uwekezaji.
“Serikali inathamini mchango wa wawekezaji kwani wana nafasi kubwa ya kuleta maendeleo kwa wananchi pamoja na nchi lakini kikubwa ni kuwa wazi wakati wa kufanya taratibu za uwekezaji ili kuondoa malumbano yanayojitokeza baina ya wananchi na wawekezaji,” alisema Mbijima.
Alisema kuwa baadhi ya wawekezaji wamekuwa wakikiuka taratibu za uwekezaji kwa kutokuwa wazi wakati wakufanya michakato ya uwekezaji kwani wanapaswa kuwa wazi kwa pande zinazohusika ili kuondoa mikanganyiko.
“”Wawekezaji wanapaswa kufuata sheria za nchi zilizowekwa ili faida inayopatikana iweze kuleta manufaa kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya uwekezaji hivyo wanapaswa kushirikiana na wananchi ili kuondoa migogoro isiyo na tija kwa uwekezaji”,  alisema Mbijima.
Aidha alisema kuwa serikali inatoa ushirikiano na wawekezaji kwnai mbali ya kutoa ajira kwa wananchi pia serikali inapata mapato yake kupitia sekta hiyo ili iweze kuendesha shughuli zake kupitia kodi na ushuru mbalimbali.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Kampuni ya DSM Corridor Group  Sada Shaban alisema kuwa ujenzi huo wa Bandari kavu ulianza 2013 na kukamilika mwaka huu kwa baadhi ya vitengo ukiwa umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 7.5 ambapo gharama iliyobakia ni kiasi cha shilingi bilioni 38 hadi kukamilika kwake.
Shaban alisema kuwa eneo hilo litakuwa ni hifadhi ya bidhaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na maghala ya mazao mbalimbali, madini na mizigo ya kila aina na itasaidia kupunguza msongamano barabarani kwani ikitoka hapo inapakizwa kwenye treni ambayo iko jirani na bandari hiyo. Mwenge huo ukiwa wilayani Kisarawe ulizindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 6.5 leo mwenge unakimbizwa wilayani Rufiji.
Mwisho.





Friday, May 20, 2016

WANANCHI KUEPUKANA NA ADHA YA UKOSEFU WA MAJI

Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wa Mitaa ya Viziwaziwa na Sagale wilayani Kibaha mkoani Pwani wataondokana na adha ya ukosefu wa Maji baada ya mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya shilingi 517,110,110 kuzinduliwa na kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa George Mbijima.
Mradi huo utakaohudumia wakazi 1,482 umekamilika baada ya Halmashauri kuomba maji kwenye bomba kuu la Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASCO) la Ruvu Juu baada ya majaribio ya kuchimba visima vya ardhini ambavyo havikupata maji.
Akielezea juu ya mradi huo katibu wa Jumuiya ya Watumiaji Maji wa Ziwaziwa na Sagale (SAVI) Abdulrahman Mango alisema kuwa mradi huo ni moja ya miradi ya Maji na Usafi wa Mazingira ni moja wapo ya mitaa minne iliyopo kwenye kata ya Viziwaziwa ambako katika Halmashauri kwenye miradi hiyo kuna jumla ya mitaa 13.
“Kabla ya kuwa na mradi huu tulikuwa tunategemea maji ya visima vya asili ambavyo ni vya msimu ambapo maji tuliyokuwa tukiyatumia yalikuwa siyo safi wala salama na inapofikia wakati wa kiangazi tunakwenda kuchota maji kwenye mtaa jirani wa Kwa Mfipa uliopo kilomita saba na kuwachukulia wananchi muda mwingi kutafuta maji badala ya kufanya shughuli za maendeleo,” alisema Mango.
Mango alisema kuwa mradi huo una husisha ujenzi wa tanki la chini lenye ujazo wa lita 50,000, ujenzi wa chumba kwa ajili ya kuweka pampu, uchimbaji wa mitaro na ulazaji wa mabomba, tanki la juu lenye ujazo wa lita 50,000, ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji na ujenzi wa mifumo matanki ya uvunaji wa maji ya mvua.
“Ujenzi wa miundombinu ya umekamilika na kwa sasa vituo tisa kati ya 10 vinatoa huduma ya maji kwa mgao wa DAWASCO siku mbili kwa wiki na unasimamiwa na SAVI na jamii huchangia shilingi 100 kwa ndoo ya lita 20 ambapo fedha hupelekwa benki na hadi sasa kuna akiba ya shilingi 950,000 na fedha zinazopatikana hutumika kwa ajili ya kulipia bila ya umeme, kufanya ukarabati mdogomdogo, uendeshaji wa ofisi na kulipa bili ya DAWASCO,” alisema Mango.
Aidha alisema kuwa mradi huo umechangiwa na wananchi kiasi cha shilingi milioni 12 kwa kutoa maeneo yao na kupitisha mabomba na kujenga vituo vya maji vya jamii na kutekeleza azma ya Rais Dk John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani.
Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mbijima alisema kuwa azma ya serikali ni kuwapunguzia kero wananchi kwa kupata huduma za kijamii karibu ili wapate muda mwingi wa kufanya shughuli za maendeleo na si kutumia muda mwingi kutafuta huduma.  

Mwisho.

MWENGE HAUNA ITIKADI

Na John Gagarini, Kibaha
IMEELEZWA kuwa dhana ya Mwenge wa Uhuru si itikadi ya chama au watu wa aina fulani bali ni kuhamasisha maendeleo ya wananchi kupitia miradi ambayo imetokana na nguvu zao.
Hayo yalisemwa wilayani Kibaha na kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa George Mbijima alipokuwa akizindua bweni la wasichana kwenye Shule ya Sekondari ya Zogowale wakati mwenge huo ukikimbizwa wilayani humo.
Mbijima alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ni alama ya maendeleo katika nchi ambapo mwasisi wake Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliutumia kama ishara ya maendeleo.
“Mwenge ni alama muhimu katika maendeleo ya nchi kwani kila mahali ulipopita umeacha alama ya maendeleo na lengo lake ni kuhamasisha watu kuwa wanapaswa kuwajibika ili kuleta mafanikio kwa mtu mmoja mmoja na jamii nzima kwa jumla,” alisema Mbijima.
Alisema kuwa watu wanaobeza Mwenge hawajui historia ya nchi na umuhimu wa mwenge ambacho umezindua na kufungua miradi mingi ya maendeleo ambayo imewaletea watu mafanikio.
“Sehemu yoyote ambayo mwenge umepita umeleta mafanikio kutokana na miradi iliyopo na kufunguliwa au kuzinduliwa na mbio hizi ambazo hufanyika kila mwaka,” alisema Mbijima.
Aliwaasa wanafunzi kuzingatia masomo na kuacha kujiingiza kwenye mambo ambayo yatawaharibia masomo yao ikiwa ni pamoja na matumizi ya dawa za kulevya au kushiriki kwenye vitendo vya ngono ambavyo mwisho wake ni kupata maambukizi ya magonjwa mbalimbali ukiwemo ukimwi.
Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi mwalimu mkuu wa shule hiyo tatu Mwambala alisema kuwa ujenzi huo ulianza mwaka 2015 na kukamilika mwaka mwaka huo huo na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 230,814,608.
Mwambala alisema kuwa lengo la ujenzi huo ni kuweka mazingira rafiki ya kujifunza na kujifunzia kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita ili kuongeza ufaulu ambapo bweni hilo lina uwezo wa kulaza wanafunzi 86 na lina miundombinu yote. Shule hiyo ilianzishwa mwaka 2007 na ilipata kibali cha kuanzisha kidato cha tano na sita mwaka 2014 na ina wanafunzi 408.
Mwenge huo ukiwa wilayani Kibaha ulitembelea miradi mbalimbali yenye tahamani ya shilingi zaidi ya bilioni nne leo unakimbizwa wilayani Mkuranga kuendelea na mbio zake.

Mwisho.          

ASKARI POLISI AUWAWA KWA RISASI

Na John Gagarini, Kibaha

ASKARI wa jeshi la  polisi kikosi cha usalama barabarani mwenye namba F.1839 sajent (SGT) Ally Salum maarufu Kinyogori ameuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika akiwa nyumbani  kwake.
>
> Tukio hilo limetokea may 19,majira ya saa 1.30 usiku huko katika kijiji cha Chatembo kata ya Mwandege wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
>
> Kamanda wa polisi mkoani hapo,Boniventure Mushongi,amesema katika hali isiyo ya kawaida watu wawili wakiwa wamevalia makoti meusi na nyuso zao wakiwa wamezificha kwa mask walifanya mauaji hayo na kutokomea.
>
> Amesema watu hao waliingia ndani ya uzio wa nyumba ya askari huyo wakitumia usafiri wa pikipiki aina ya boxer na baada ya kushuka kwenye pikipiki waliingia ndani na kumfyatulia risasi askari huyo kichwani pamoja na ubavuni na kumpotezea maisha yake.
>
> Kamanda Mushongi amesema katika tukio hilo wauaji hao hawakuchukua  kitu chochote zaidi ya funguo wa gari la  marehemu ambapo waliondoka nalo.
>
> Amesema msako mkali wa kuwasaka waliohusika  na tukio unaendelea  na ameomba  ushirikiano kutoka kwa wananchi kwa wale wenye taarifa zitakazosaidia kuwapata  wahusika hao.
>
> Mwili  wa marehemu umehifadhiwa  katika hospital ya Temeke na utakabidhiwa  kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi mara  baada ya kufanyiwa uchunguzi .
>
> Mwisho

Thursday, May 19, 2016

MKURANGA MBIONI KUMALIZA TATIZO LA MADAWATI

Na John Gagarini, Kibaha
WILAYA ya Mkuranga mkoani Pwani limechonga madawati 5,043 ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa madawati kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Abdala Kihato akisoma taarifa ya wilaya hiyo kwa mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo wakati wa ziara yake kutembelea wilaya hiyo kukagua shughuli za maendeleo.
Kihato alisema kuwa wilaya hiyo ilikuwa na upungufu wa madawati 5,131 hivyo kubakiwa na upungufu wa madawati 500 ambayo wanatarajia kukamilisha utengenezaji muda mfupi ujao.
“Tatizo la upungufu wa madawati kwa wanafunzi wa shule za Sekondari tatizo hilo hakuna ila tatizo kubwa liko kwa wanafunzi wa shule za Msingi kutokana na uwingi wao na hata wale wa darasa la kwanza ambapo kwa mwaka huu walioandikishwa ni wengi sana,” alisema Kihato.
Alisema kuwa hawana wasiwasi kwani hadi ule muda uliowekwa wa Juni 30 kwa wilaya zote kuondoa tatizo la wanafunzi kukaa chini litakuwa limekwisha kabisa kwani wanashirikiana na wadau mbalimbali kutengeneza madawati.
“Tunawahimiza watendaji wa vijiji na kata kuhakikisha wanakamilisha zoezi hilo ili kuwaondolea adha wanafunzi kukaa chini na kuwafanya washindwe kujifunza vizuri masomo yao,” alisema Kihato.
Aidha aliwaomba wadau wa maendeleo ndani ya wilaya hiyo kuwaunga mkono katika kufanikisha zoezi hilo la uchongaji wa madawati kwa wanafunzi kwenye wilaya hiyo.
Naye mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo alisema kuwa anaipongeza wilaya hiyo kwa kuweza kufanikisha kuchonga madawati hayo ambayo sasa yanaenda kuondoa tatizo hilo la upungiufu wa madawati.
Ndikilo alisema kuwa mkoa huo ulikuwa una upungufu wa madawati 43,047 kwa shule za msingi lakini kwa jitihada hizo zitakuwa zimepunguza kwa kiasi kikubwa upungufu huo.

Mwisho.

MKURANGA YAZUIA MALIPO YA MISHAHARA YA WATUMISHI 15

Na John Gagarini, Mkuranga
WILAYA ya Mkuranga mkoani Pwani imewasimamishia malipo watumishi 15 ambao wameondoka kwenye vituo vyao vya kazi bila ya taarifa kwa mwajiri wake ambaye ni Halmashauri.
Hayo yalisema na mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Abdala Kihato alipokuwa akisoma taarifa ya wilaya wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Pwani kutembelea shughuli za maendeleo kwenye wilaya hiyo.
Kihato alisema kuwa mishahara hiyo ilizuiliwa kutokana na watumishi hao kutotoa taarifa walipoondoka kwenye vituo vyao vya kazi wakati wa uhakiki watumishi katika zoezi la kutambua watumishi hewa.
“Tulifanya uhakiki wa watumishi 179 na kubaini kuwa watumishi 85 walikuwa ni watoro ambapo 51 wamehamia kwenye vituo vingine vya kazi 10 hawakujitokeza na 15 ndiyo walioondoka kwenye vituo vya kazi bila ya taarifa na watano ni watoro kabisa,” alisema Kihato.
Alisema kuwa zoezi hilo ni endelevu na linaendelea kwani linaoneka lina changamoto nyingi katika kubainisha watumishi hewa na wale ambao wako kisheria.
“Hatua tuliyoichukua kwa wale ambao waliondoka kwenye vituo vyao vya kazi bila ya taarifa ni kusimamisha mishahara yao ili wasije wakwa wanachukua fedha pasipo kufanya kazi,” alisema Kihato.
Kwa upande wake Ndikilo alisema kuwa maofisa utumishi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa serikali katika kuhakikisha watumishi hewa wanapatikana na itawachukulia hatua kali wale watakaowaficha watumishi hewa.
Ndikilo alisema kuwa zoezi hilo litakapokamilika mkoa utatoa taarifa juu ya zoezi hilo ambalo lina lengo la kuondoa watumishi hewa ambao wamekuwa wakijipatia fedha pasipo kufanya kazi.

Mwisho.

MWENGE KUPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 66.3

Na John Gagarini, Bagamoyo
MWENGE wa Uhuru jana ulianza mbio zake mkoani Pwani baada ya kumaliza kuzunguka mkoa wa Dar es Salaam ambapo utakimbizwa kwenye Wilaya Sita za mkoa huo na kupitia miradi 47 yenye thamani ya shilingi bilioni 66.3.

Akizungumza mara  baada ya kukabidhiwa mwenge  wa uhuru kutoka wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam  mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, alisema miradi hiyo imetekelezwa kwa ushirikiano wa serikali kuu na wananchi.

Ndikilo alisema kuwa kati ya miradi hiyo 47, miradi 14 itawekwa mawe ya msingi, 11 itazinduliwa,11 itafunguliwa na miradi mingine 11 itakaguliwa na mwenge huo utakapokuwa mkoani hapa.

 “Miradi mingine  imetekelezwa na Halmashauri, wahisani wa kitaifa na kimataifa pamoja na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ambapo ujumbe wa mwenge  mwaka huu unasema vijana ni nguvu kazi ya taifa na shirikisho la kuwezeshwa hivyo tupige vita matumizi ya madawa ya kulevya,” alisema Ndikilo.

Alisema kuwa kwa kutambua changamoto za vijana mkoa umejipanga katika kutatu  changamoto za vijana kwa ushirikiano na vijana wenyewe ambao katika mkoa huu wapo vijana 379,646 kati ya watu milioni 1.9.

“Mkoa umejipanga kutekeleza ujumbe huo kwa vitendo kwani  msingi mkubwa wa ujumbe ni vijana ndio nguzo na ni chachu kubwa ya maendeleo katika taifa hivyo lazima tuwape nafasi,” alisema Ndikilo.

Aidha aliwataka vijana kuchangamkia fursa za kiuchumi na kijamii zilizopo ili kujibu changamoto hususan za ajira walizonazo na ni wakati wa vijana kujitokeza kutumia fursa mbalimbali zikiwemo kujiajiri na kuwajibika ili kukabiliana na changamoto walizonazo kwa kuzigeuza kuwa fursa za ajira kwenye maeneo yao.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paulo Makonda akimkabidhi Ndikilo mwenge huo wa Uhuru alishukuru kukabidhi mwenge  huo kwa mkoa wa Pwani huku ukiwa umetembea mkoani kwake bila ya tatizo lolote na Mwenge leo  utakimbizwa katika wilaya ya Kibaha.

Mwisho


WANANCHI WALILIA DARAJA

Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wa mtaa wa Mkombozi wilayani Kibaha mkoani Pwani umeiomba Halmashauri ya Mji wa Kibaha kuwajengea kivuko au daraja kwenye mto Mpiji kwa ajili ya kuvuka kwenda Majohe wilaya ya Kinondoni kupata huduma za kijamii ambako ni jirani na ikilinganishwa na Maili Moja wilaya ya Kibaha umbali wa kilometa zaidi ya 10.
Akizungumza na waandishi wa habari mkazi wa mtaa huo Malaki Lakibuka alisema kuwa  huduma hizo wanazipata Majohe kutokana na ukaribu uliopo wa kilometa mbili ukilinganisha na Kibaha ambako ni mbali kwa zaidi ya kilometa 10, lakini tatizo lililopo ni kukosa kivuko au daraja.
Lakibuka alisema kuwa wako kwenye wakati mgumu kuvuka mto huo kutokana na kuwa na mamba wengi jambo ambalo ni hatari kwa usalama wao ambapo kwa miaka ya nyuma watu walikuwa wakiliwa na mamba.
“Tunapata taabu sana kuvuka hapo mtoni kwani mamba ni wengi na pia endapo utapita vibaya unaweza kuchukuliwa na maji hasa wakati wa mvua hivyo kuhatarisha maisha yetu na ikizingatiwa kuwa watumishi wanaofanya kazi Majohe,” alisema Lakibuka.
Naye mweneykiti wa mtaa huo ambao ni mpya Moshi Mhagama alisema kuwa kutokuwa na kivuko ni changamoto kubwa kwa wananchi ambao wanategemea  hali inakuwa mbaya kipindi cha mvua ambapo mto huo unakuwa umejaa maji.
Moshi alisema kuwa wanategemea Majohe kama ni sehemu ya kupata mahitaji yao ya kawaida ambako ni jirani ikilinganishwa na Kibaha ambako ni mbali sana hivyo tungeomba Halmashauri iwasaidie ujenzi huo ambapo nao tayari walishaanza kuchangishana fedha kwa ajili ya ujenzi wa kivuko.
“Kwa wagonjwa au mama wajawazito ni taabu kwani wanajifungulia wakiwa njiani lakini pangekuwa na daraja wangepita kwa urahisi na kuwawahisha wagonjwa kupata matibabu pia kuna wafanyakazi wanafanya kazi ngambo ya pili ni shida sana kuvuka mvua zinapokuwa nyingi,” alisema Moshi.
Naye diwani wa kata hiyo Agustino Mdachi alisema kuwa jambo hilo alilipeleka Halmashauri lakini alijibiwa kuwa uwezo wa kujenga daraja hilo haupo kutokana na gharama za ujenzi kuwa kubwa sana kiasi cha zaidi ya bilioni mbili.
Mdachi alisema kuwa changamoto kwenye eneo hilo ni kubwa sana kwani mbali pia kuna mamba ambao ni hatari kwa watu wanaovuka hapo hivyo kuhatarisha maisha yao.
“Mbali ya Halmashauri kusema kuwa hawana uwezo wa kujenga daraja kwa sasa pia walisema hawawezi kujenga kivuko cha muda kwani gharama itakuwa mara mbili wao wanataka wajenge kitu cha kudumu ambapo ni ujenzi wa daraja,”alisema Mdachi.
Mwisho. 

Wednesday, May 18, 2016

WAMKATAA MWENYEKITI WAMFUNGIA OFISI

Na Mwandishi Wetu, Kibaha
WAKAZI wa Mtaa wa Muheza kata ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani wamefunga ofisi ya mtaa huo kwa madai ya kuukata uongozi ambao wamesema haufanyi kazi kwa utaratibu uliowekwa ikiwa ni pamoja na kutofungua ofisi.
Wakizungumza na waandishi wa habari walisema kuwa uongozi huo tangu umechaguliwa umeshindwa kabisa kuwajibika hivyo kushindwa kuleta maendeleo kwa kipindi chote cha uongozi wao walipochaguliwa mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka jana.
Moja ya wakazi hao ambaye alijitambulisha kwa jina la Modestus Mpelembwa alisema kuwa uongozi huo chini ya mwenyekiti wake Maulid Kipilili umeshindwa kabisa hata kuitisha mikutano ya kisheria ambayo ndiyo sehemu ya wananchi kuweza kuchangia maendeleo na kujua kinachoendelea ndani ya mtaa huo.
“Wananchi wamefikia hatua ya kufunga mlaango wa ofisi kutokana na kuona kuwa hawana msaada wowote na uongozi ambapo hata kama unashida huwezi kusaidiwa kwani hakuna kiongozi hata mmoja anayeonekana zaidi ya kuonekana kwa matukio maalumu,” alisema Melembwa.
Mpelembwa alisema kuwa hata mapato ya mtaa hayaonekani licha ya kuwa mtaa huo ni moja ya mitaa ambayo ina maeneo makubwa ya ardhi ambayo yanauzwa kama viwanja kwa ajili ya makazi kutokana na eneo hilo kuanza kujengeka kwa sasa.
“Ofisi muda mwingi imefungwa kama una shida umpigie simu mwenyekiti na kama ni suala la mauziano ya viwanja ni huko huko na siyo ofisini kama taratibu zinavyosema hali ambayo inaonyesha kuwa hakuna uwazi wa fedha za asilimia zinazotakiwa kubaki kwenye mtaa kwa ajili ya shughuli za maenedeleo,” alisema Mpelembwa.
Naye Angela Mduma alisema kuwa uongozi huo haufai kuwaongoza kwani umeshindwa kukabili changamoto za wananchi ambao waliwachagua kwa ajili ya kutatua kero mbalimbali ikiw ani pamoja na ubovu wa barabara.
“Tuna chanagamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa zahanati, shule ya msingi, maji pamoja na huduma nyingine za kijamii lakini endapo uongozi ungekuwa makini kupitia mikutano kama ingekuwa inafanyika tungeweka vipaumbele vya kuanza kuvifanyia kazi lakini uongozi hauna ushirikiano hakuna kilichofanyika hadi sasa,” alisema Mduma.
Mduma alisema kuwa kwa upande wa kinamama wanapata taabu hasa kwenye huduma za kiafya kliniki kwa wajawazito, kuwapeleka watoto wao kliniki na matibabu kwa ujumla kwao ni changamoto kubwa sana.
Naye Modestus Mapunda alisema kuwa mara ya mwisho mwenyekiti aliitisha mkutano wa mtaa lakini cha ajabu muda mfupi baadaye aliahirisha wakati tayari wananchi wameshajiandaa kwa mkutano hali ambayo ilisababisha wananchi kushikwa na hasira na kuifunga ofisi.
“Tunachotaka ni mkuu wa wilaya kuja hapa kwa ajili ya kujua kero zetu kwani uongozi umeshindwa kufanya kazi lakini cha kushangaza wajumbe kutakiwa kutofanya chochote na mwenyekiti na hawaruhusiwi kuingia ofisini hadi watakapoitwa,” alisema Mapunda.
Mwenyekiti wa mtaa huo Maulid Kipilili alisema kuwa hawezi kuongea chochote kwani anaongea na uongozi wa juu na pia suala hilo tayari amelipeleka polisi kulalamika wananchi hao kufunga ofisi ya mtaa.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lipwai alisema kuwa kufungwa kwa ofisi hiyo ni kinyume cha utaratibu kwani ile ni mali ya umma na wananchi wanapata huduma kupitia ofisi hiyo.
Lipwa alisema kuwa anafanya mawasiliano na viongozi mbalimbali ili kupata suluhu la tatizo hilo ili ofisi hiyo iweze kufunguliwa ili wananchi waweze kupata huduma kupitia ofisi hiyo ambayo imefungwa tangu Mei 15 baada ya mkutano wa mtaa kushindwa kufanyika.
Mwisho.  











   

Thursday, May 12, 2016

NOAH KUTOSAJILIWA KUBEBA ABIRIA BARABARA KUU

Na John Gagarini, Kibaha
MAGARI ya kusafirisha abiria aina ya Noah Hiace pamoja na pikipiki yamesababisha vifo vya watu 102 huku 246 wakijeruhiwa katika kipindi cha kuanzia 2015 hadi Machi 2016.
Kutokana na kukithiri kwa ajali za vyombo hivyo Mamlaka ya Udhibiti  wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) mkoa wa Pwani imesitisha utoaji wa lesseni mpya kwa magari aina ya Noah maarufu kwa jina la ‘Mchomoko’, na Hiace  kwenye barabara zote kuu ikiwamo barabara ya Morogoro.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha ofisa mfawidhi wa SUMATRA mkoa wa Pwani Nashon Iroga alisema kuwa kwa mujibu wa waraka walioupata kutoka makao makuu magari  hayo yote madogo  ya abiria yanayokwenda masafa  marefu kupitia barabara kuu hayatapewa leseni ya kubeba abiria.
“Barabara kuu kuna vyombo vikubwa vya  usafiri hivyo hayataruhusiwa kupata leseni mpya badala yake yaliyokwisha pata leseni yataendelea hadi hapo muongozo mwingine utakapo toka tena,” alisema Iroga.
Alisema kuwa agizo hilo limetolewa baada ya ongezeko kubwa la magari madogo ya kubeba abiria hasa magari  aina ya noah, kufanya safari ndefu huku baadhi  yakiwa yamebeba abiria na mizigo  bila kuangalia usalama wa abiria  na matokeo yake ni kusababisha ajali za mara kwa mara na msongamano katika barabara kuu.
“Ukiangalia kwa hali ya kawaida magari aina ya Noah yanabeba abiria wachache lakini ili wapate faida inabidi watoze viwango vikubwa vya nauli, kubeba abiria kuliko uwezo wake na kwenda mwendo kasi  ili wafanye safari nyingi na kupata faida, matokeo yake wanahatarisha usalama wa maisha ya abiria,” alisema Iroga.
Aidha alisema kuwa  magari hayo madogo yakiwamo Noah na Hiace yanayobeba abiria yatapewa lesseni mpya za kufanya biashara kutumia ruti za barabara  za ndani na sio barabara kuu.

Mwisho.

JESHI LA POLISI LAMSAKA MWANAFUNZI ALIYECHOMA BWENI


Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi Mkoani Pwani bado linaendelea kumtafuta mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Rafsanjani iliyopo Soga Tarafa ya Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani baada ya kuchoma bweni la wasichana la shule hiyo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa mwanafunzi huyo ambaye hakuweza kufahamika alichoma bweni hilo juzi majira ya saa 4 usiku liitwalo Umoja.
Mushongi alisema kuwa hata hivyo tukio hilo halikuwa na madhara kwa wanafunzi zaidi ya kuharibu mali zilizokuwa kwenye bweni hilo ambazo hata hivyo thamani yake haikuweza kufahamika mara moja.
“Tunaendelea kumfuatilia mwanafunzi huyo ili tuweze kumjua na kumchukulia hatua za kisheria lakini hadi sasa bado hatujafanikiwa kumpata kwani aliandika kwenye sanduku la maoni juu ya dhamaira yake hiyo mbaya ya kuchoma bweni,” alisema Mushongi.
Alisema kuwa wanaendelea kuzifanyia kazi taarifa hizo ili waweze kumbaini mwanafunzi huyo ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake kwani kitendo alichokifanya ni cha hatari kwa maisha ya wanafunzi wenzake na mali.
“Tunatoa wito kwa wanafunzi wanapokuwa shuleni wazingatie masomo na kuachana na vitendo visivyo kuwa na maadili kwani jeshi halitawavumilia wanafunzi ambao wanabainika kufanya vitendo viovu kwani tutawakamata na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria ikiwa ni pamoja na mahakamani,” alisema Mushongi.
Bweni hilo lilichomwa moto juzi na mwanafunzi huyo lakini hata hivyo kikosi cha zimamoto mkoa wa Pwani polisi pamoja na wananchi walifanikiwa kuzima moto huo na haukuweza kuleta madhara kwa wanafunzi.

Mwisho.

KIWANDA CHA TILES KUJENGWA MKURANGA


Na John Gagarini, Mkuranga
WAKAZI wa mkoa wa Pwani wametakiwa kuunga mkono mkakati wa serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk John Magufuli ya kuhamasisha ujenzi wa viwanda na uwekezaji.
Akizungumza na wakazi wa vijiji vya Nyamato na Mkiu wilayani Mkuranga wakati alipotembelea kiwanda cha kutengeneza vigae (Tiles) cha Goodwill Tanzania Ceramic mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo alisema kuwa wananchi wananafasi kubwa ya kufanikisha nchi kuwa ya viwanda kwa kushirikiana na wamiliki wa viwanda.
Ndikilo alisema kuwa wananchi wanapaswa kuwapa ushirikiano wawekezaji wa viwanda ili waweze kufanya kazi bila ya kuhujumiwa kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa wakihujumu miundombinu ya viwanda.
“Wawekezaji kama hawa wa viwanda mnapaswa kuwaunga mkono kwani manufaa ya uwepo wao ni mengi sana ikiwa ni pamoja na kupata ajira pamoja na nyie kuuza bidhaa zenu kwani biashara zitakuwa nyingi hivyo mtaweza kubadilisha maisha yenu lakini endapo mtawafanyia vitendo vya kuwakatisha tama wataondoka,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa kwa sasa mkoa wa Pwani ajenda yake ni kuhakikisha unakuwa mkoa wa viwanda na hilo linawezekana kwa kuwa na viwanda vingi vya kuzalisha bidhaa mbalimbali.
“Mkoa kwa sasa umeamua kujitangaza kiviwanda kwnai nafasi za uwekezaji bado zipo nyingi na lengo ni kuhakikisha wananchi wanakuwa na uchumi wa kati na utainuka endapo kutakuwa na viwanda vingi mfano tu wilaya ya Mkuranga mmeanza kutekeleza kwa vitendo mkakati wa Rais wa kuwa na viwanda kwnai kwa sasa kuna viwanda 59,” alisema Ndikilo.
Aliwataka wakurugenzi na wakuu wa wilaya za mkoa huo kuhakikisha wanatenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji na kuhamasisha wageni na wazawa kujenga viwanda ili kuinua uchumi wa wananchi lakini wahakikishe wawekezaji wan je wanafuata taratibu za nchi kwa wafanyakazi kwa kuzingatia sheria za kazi.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa kiwanda hicho Yang Zhen alisema kuwa kiwanda hicho ni cha pekee kwani kitakuwa cha pili barani Afrika kwa ukubwa na cha kwanza Tanzania kwa uzalishaji wa vigae ambapo kwa siku kitakuwa kikizalisha meta 80,000 kwa siku.
Zhen alisema kuwa maradi huo una thamani ya dola za Kimarekani 100 na umegawanyika kwenye hatua mbili ambapo awamu hii ya kwanza itaisha mwishoni mwa mwaka huu huku ile ya pili ikiisha mwishoni mwa mwakani hivyo bidhaa hizo za vigae zitakuwa zikizalishwa hapahapa na siyo nje ya nchi.
Aidha alisema kuwa wanatarajia kujenga shule, kuwapatia maji, zahanati pamoja na kituo cha polisi ikiwa ni kama mchango wao kwa jamii inayozunguka kiwanda hicho ambapo mara kitakapokamilika kitaajiri watu 2,000 na kwa sasa kimetoa ajira kwa watu 200.
Mwisho.