Thursday, February 28, 2013

FRIENDS OF SIMBA WATAKIWA KUJITOKEZA KUTATUA MGOGORO



Na John Gagarini, Kibaha
MARAFIKI wa Simba (Friends of Simba) wametakiwa kuingilia kati tatizo lililopo kwenye klabu yao ili iweze kuwa na mwenendo mzuri katika mashindano mbalimbali inayoshiriki timu yao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi msemaji wa tawi la Simba wilayani Kibaha “Simba Tishio” Fahim Lardhi alisema kuwa hadi sasa timu hiyo bado haijapata tiba ya tatizo lililopo ndani ya klabu hiyo.
Lardhi alisema kuwa wakati huu wa matatizo wanachama na wadau wa Simba lazima wajitokeze kusaidia timu ili iweze kufanya vema kwani kwa sasa mwenendo wake ni mbaya.
“Marafiki wazuri huonekana wakati wa shida hivyo tunataka marafiki wetu wajitokeze kuinusuru timu kwani kwa sasa timu inaonekana kufanya vibaya kwenye michezo yake tofauti na matarajio ya wengi,” alisema Lardhi.
Alisema kuwa marafiki wa Simba mbali ya kusaidia fedha pia wanatakiwa kuisaidia timu hiyo kwa mchango wa mawazo ili kujua tatizo lililopo hadi timu kufanya vibaya kwenye michezo yake.
“Wanapaswa kuonyesha upendo wao kwa klabu kwani hadi sasa hatujaona jitihada zozote walizofanya kuinusuru timu na matokeo mabaya, tunawpongeza wanaposaidia timu katika mazingira yote pia waonyeshe upendo hata kama timu inafanya vibaya ili kuinusuru timu yetu ambayo inatetea ubingwa wake wa ligi kuu ya Tanzania Bara,” alisema Lardhi.
Msemaji huyo wa tawi la Simba wilayani Kibaha alisema kuwa Wanasimba wanatakiwa kuungana katika kipindi hichi kigumu kinachoikabili timu yao kwa kuwa na matokeo mabaya inayoyapata ili kujinusuru na kupata matokeo mazuri.
“Tunapaswa kuungana na kuonyesha mshikamano ili kuisaidia timu yetu kwani timu inapofanya vibaya tunaumia sana hivyo tuungane ili kuiletea maendeleo mazuri,” alisema Lardhi.
Ameipongeza kamati ya utendaji kwa kuandaa mkutano wa kujadili kiini cha timu kufanya vibaya katika michezo yake hali ambayo inaifanya timu hiyo kuwa kwenye mashaka ya kutetea ubingwa wake.
Mwisho.    

KAYA ZAIDI YA 1000 ZAKUMWA NA NJAA



Na John Gagarini, Bagamoyo
KAYA 1,138 katika vijiji vitano kwenye kata ya Miono wilayani Bagamoyo mkoani Pwani vinakabiliwa na baa la njaa na kuhitaji msaada wa chakula.
 Kwa mujibu wa Diwani wa kata hiyo Sangali Kiselu alisema kuwa kaya hizo zinahitaji msaada ili kukabiliana na njaa hiyo.
Kiselu alisema kuwa kutokana na tatizo hilo uongozi wa kata ya Miono umeiomba serikali Mkoani Pwani  kuharakisha kuwapatia msaada wa chakula kaya hizo ili kukabiliana na tatizo hilo.
“Hali kwa sasa inazidi kuwa mbaya katika kaya hizo ikiwa ni kati ya kaya 4,271 zenye watu zaidi ya 20,000 ambazo zimekumbwa na baa hilo la njaa,” alisema Kiselu.

Alivitaja vijiji ambavyo vimepata athari hiyo kuwa ni
Kweikonje, Masimbani, Mihuga, Kikalo na Miono kwenye kata hiyo.

Kwa upande wake mtendaji wa kata hiyo Ramadhani Nguya alisema kwa sasa wanahofia kutokana na hali kufikia pabaya hivyo haina budi kutoa kilio hicho kwa niaba ya wananchi ili kunusuru maisha yao.

Naye Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Ahmed Kipozi amekiri kuwepo kwa hali hiyo nakusema si kweli kuwa serikali inachelewesha kupeleka msaada wa chakula katika maeneo hayo.

“Serikali imeshaidhinisha tani 400 ambazo zitasambazwa katika maeneo mbalimbali yaliokumbwa na baa hilo wilayani humo, ikiwa ni pamoja na kata ya Kibindu, Mbwewe, Kimange, Miono na Kiwangwa ambayo haijapata athari sana.

Kipozi alisema kuwa janga la njaa limezikumba kata hizo kutokana na mavuno hafifu kwa mwaka jana yaliyosababishwa na mvua iliyokuwa hairidhishi hivyo kwa sasa amehimiza kilimo cha mhogo na mtama ambayo yanahimili ukame.

Mwisho

Tuesday, February 26, 2013

WALIOMTEKA MWANAFUNZI WASHIKILIWA NA POLISI


Mwandishi Wetu, Kibaha
JESHI la polisi mkoani Pwani linawashikilia vijana watatu kwa tuhuma za kumteka mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Pangani Kata ya Pangani wilayani Kibaha mkoani Pwani ambaye alikuwaaingie kidato cha pili mwaka huu mwenye umri wa miaka (16) na kushindwa kwenda shule baada ya kutekwa na vijana watatu kwa kipindi cha miezi mitatuambapo alipata mimba na vijana hao waliitoa.

Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwao Kidimu wilayani Kibaha huku akibubujikwa na machozi alisema kuwa vijana hao ambao ni wakulima kati yao wawili ni ndugu walimteka kwa kutumia visu vitatu walivyokuwanavyo.

Aliwataja vijana hao ambao anawatuhumu kumfanyia kitendo hicho kuwa ni
Jovinas Oswald , Isaka Joseph na Faida Joseph (22) ambao ni ndugu walimteka Novemba 3 mwaka jana baada ya kumdanganya kuwa anatakiwa kwenda kuchukua mzigo wa ndugu yake.

“Baada ya kwenda kufuata mzigo huo niliwakuta wakiwa na visu vitatu ambapo
kila mmoja alikuwa na kisu na kunipeleka kwenye nyumba waliyokuwa wakiishi
kusema kuwa hapo ndipo nitakapokuwa naishi na endapo nitajaribu kutoka basi
wataniua,” alisema.

Alisema kuwa kwa kipindi chote hicho walikuwa wakifunga mlango kwa nje kwa
kutumia kufuli kwa nje huku wakiwa wamemhifadhi kwenye kisehemu mithili ya kajeneza kwani juu waliweka miti na pembeni waliweka matofali na juu waliweka godoro huku yeye akiwa chini hali ambayo ilimfanya ashindwe kutoka pia
ikizingatiwa kuwa nyumba hiyo iko mbali na nyumba zingine na kuwa katika
kichaka.

“Faida ambaye ndiye aliyenifanya kama mke wake alinipa mimba lakini baada
ya kuona hivyo walinilazimisha kuitoa kwa kutumia majani ya chai ambayo
yalichemshwa na maji na kuniamuru ninywe na kusababisha mimba kutoka ambapo nilitokwa na damu nyingi na kupata maumivu makali,” alisema mwanafunzi huyo.

Aidha alisema kuwa walimtengenezea kajumba kadogo kwa kupanga matofali na
miti kisha yeye kuingia humo mfano wa kaburi ambapo alikuwa akijisaidia
kwenye mifuko ya plastiki na chupa kwa ajili ya haja ndogo na kuoga ni humo
ndani.

“Kwa upande wa chakula walikuwa wakipika usiku tu kwani walikuwa wakifika
majira ya saa sita au saba usiku wanapika tunakula ila asubuhi na mchana
nilikuwa sili chakula hata mavazi yangu waliyachoama moto nikawa navaa nguo
ya moja ya vijana hao,” aliongeza.

Aliongeza kuwa siku moja vijana hao walisahau kufunga mlango na ndipo
alipotoka na kuomba msaada kwa mtu ambaye alimpeleka hadi nyumbani kwa
walezi wake ambao ni babu na bibi yake ambao ndiyo waliokuwa wakiishi naye
kwa muda wote.

Kwa upande wake babu wa mwanafunzi huyo Daud Zakayo alisema kuwa mwanafunzi
huyo alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na walifanya jitihada
kumtafuta ambapo walitoa taarifa polisi na kwa ndugu lakini bila ya
mafanikio.

Zakayo alisema kuwa baada ya mjukuu wao kupatikana walitoa taarifa polisi
ambapo vijana hao walikamatwa kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tukio
hilo.
Naye mwalimu wa shule aliyokuwa akisoma Peter Mihayo alisema kuwa mwanafunzi huyo hajafukuzwa ila atasubiri hadi suala lake litakapokamilika kwani tayari liko kwenye vyombo vya sheria.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alipoulizwa kuhusiana na
tukio hilo alisema kuwa watuhumiwa wanashikiliwa na mara upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Mwisho.

AKUTWA AMEFIA GESTI

Na Mwandishi Wetu, Kibaha
MWILI wa mfanyabiashara wa Jijini Dar es Salaam Ambrose Mapunda anayekadiriwa kuwa na umri kati (50) na (55) umekutwa chini ya uvungu wa nyumba ya kualala wageni huku ukiwa mtupu bila ya nguo.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ofisa upelelezi wa mkoa wa Pwani wa jeshi la polisi Juma Yusuph alisema kuwa tukio hilo lilitokea kwenye nyumba ya kulala wageni kwenye nyumba ya kulala wageni ya Cham Cham iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Alisema tukio hilo lilitokea kati ya Fabruari 22 na 24 kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni huku ukiwa na jeraha kubwa kichwani huku shingo yake ikiwa imenyongwa.
“Marehemu alikutwa akiwa chini ya uvungu huku mwili wake ukiwa hauna nguo na jeraha huku ukiwa umenyongwa shingo ambapo mtu aliyehusika na tukio hilo hakuweza kufahamika mara moja,” alisema kamanda Yusuph.
Alibainisha kuwa marehemu hakukutwa na kitu chochote licha ya kuwa alifika kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni akiwa na begi kwenye chumba namba mbili.
“Ujumbe uliokutwa kwenye chumba hicho ulisema kuwa umenidhulumu tulikubaliana unilipe kiasi cha shilingi 20,000 lakini hujanilipa, ujumbe huu umeandaikwa na mtu asiyefahamika,” alisema Kamanda Yusuph.
Aidha alisema kuwa mhuduma na mlinzi wa nyumba hiyo ya kulala wageni wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo na polisi wanaendelea na uchunguzi.
Mwisho.  

AKUTWA AMEFIA GESTI

Na John Gagarini, Kibaha
MFANYABIASHARA wa Jijini Dar es Salaam Ambrose Mapunda mwenye umri kati ya 50 na 55 amekutwa amekufa na mwili wake kuwekwa chini ya uvungu wa kitanda wa nyumba ya kulala wageni ya Cham Cham Msata wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kwa niaba ya kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ofisa upelelezi wa Jeshi la polisi Juma Yusuph alisema kuwa mwili wa marehemu ulikutwa ukiwa uchi.
Kamanda Yusuph alisema kuwa tukio hilo lilitokea kati ya Fabruari 22 na 24 mwaka huu kwenye nyumba ya kulala wageni ya Cham Cham huku ukiwa na jeraha kubwa kichwani huku shingo yake ikiwa imenyongwa.
“Marehemu alikutwa akiwa chini ya uvungu huku mwili wake ukiwa hauna nguo na jeraha huku ukiwa umenyongwa shingo ambapo mtu aliyehusika na tukio hilo hakuweza kufahamika mara moja,” alisema kamanda Yusuph.
Alisema kuwa marehemu hakukutwa na chochote licha ya kuwa alifika kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni akiwa na begi kwenye chumba namba mbili.
“Ujumbe uliokutwa kwenye chumba hicho ulisema kuwa umenidhulumu tulikubaliana unilipe kiasi cha shilingi 20,000 lakini hujanilipa, ujumbe huu umeandaikwa na mtu asiyefahamika,” alisema Kamanda Yusuph.
Aidha alisema kuwa mhuduma na mlinzi wa nyumba hiyo ya kulala wageni wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo na polisi wanaendelea na uchunguzi.
Mwisho.  

Monday, February 25, 2013

MWANAFUNZI AFANYIWA UNYAMA



Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI wa shule ya sekondari ya Pangani Kata ya Pangani ambaye alikuwa aingie kidato cha pili mwaka huu mwenye umri wa miaka (16) ameshindwa kwenda shule baada ya kutekwa na vijana watatu kwa kipindi cha miezi mitatu ambapo alipata mimba na vijana hao waliitoa.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha huku akibubujikwa na machozi alisema kuwa vijana hao ambao ni wakulima kati yao wawili ni ndugu walimteka kwa kutumia visu walivyokuwanavyo.
Aliwataja vijana hao ambao anawatuhumu kumfanyia kitendo hicho kuwa ni Jonas Edward, Isaka Joseph na Faida Joseph ambao ni ndugu walimteka Novemba 3 mwaka jana baada ya kumdanganya kuwa anatakiwa kwenda kuchukua mzigo wa ndugu yake.
“Baada ya kwenda kufuata mzigo huo niliwakuta wakiwa na visu vitatu ambapo kila mmoja alikuwa na kisu na kunipeleka kwenye nyumba waliyokuwa wakiishi kusema kuwa hapo ndipo nitakapokuwa naishi na endapo nitajaribu kutoka basi wataniua,” alisema mwanafunzi huyo.
Alisema kuwa kwa kipindi chote hicho walikuwa wakifunga mlango kwa nje kwa kutumia kufuli kwa nje hali ambayo ilimfanya ashindwe kutoka pia ikizingatiwa kuwa nyumba hiyo iko mbali na nyumba zingine na kuwa katika kichaka.
“Faida ambaye ndiye aliyenifanya kama mke wake alinipa mimba lakini baada ya kuona hivyo walinilazimisha kuitoa kwa kutumia majani ya chai ambayo yalichemshwa na maji na kuniamuru ninywe na kusababisha mimba kutoka ambapo nilitokwa na damu nyingi na kupata maumivu makali,” alisema mwanafunzi huyo.
Aidha alisema kuwa walimtengenezea kajumba kadogo kwa kupanga matofali na miti kisha yeye kuingia humo mfano wa kaburi ambapo alikuwa akijisaidia kwenye mifuko ya plastiki na chupa kwa ajili ya haja ndogo na kuoga ni humo ndani.
“Kwa upande wa chakula walikuwa wakipika usiku tu kwani walikuwa wakifika majira ya saa sita au saba usiku wanapika tunakula ila asubuhi na mchana nilikuwa sili chakula hata mavazi yangu waliyachoama moto nikawa navaa nguo ya moja ya vijana hao,” aliongeza.
Aliongeza kuwa siku moja vijana hao walisahau kufunga mlango na ndipo alipotoka na kuomba msaada kwa mtu ambaye alimpeleka hadi nyumbani kwa walezi wake ambao ni babu na bibi yake ambao ndiyo waliokuwa wakiishi naye kwa muda wote.
Kwa upande wake babu wa mwanafunzi huyo Daud Zakayo alisema kuwa mwanafunzi huyo alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na walifanya jitihada kumtafuta ambapo walitoa taarifa polisi na kwa ndugu lakini bila ya mafanikio.
Zakayo alisema kuwa baada ya mjukuu wao kupatikana walitoa taarifa polisi ambapo vijana hao walikamatwa kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tukio hilo. Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema kuwa bado hajapata taarifa.
Mwisho.  

RAGE ACHANGIA TAWI LA SIMBA KIBAHA



Na John Gagarini, Kibaha
MWENYEKITI wa Klabu ya Simba Ismail Aden Rage ameendesha harambee kuchangia tawi la Simba Kwa Mfipa wilayani Kibaha mkoani Pwani kwa ajili ya shughuli mbalimbali ambapo alifanikisha kupatikana kwa kiasi cha shilingi 420,000.
Harambee hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki Kwa Mathias wilayani Kibaha kwenye ukumbi wa Back Yard ambapo mbali ya kuendesha harambee walijadili mambo mbali mbali ya kuisaidia klabu hiyo kufanikiwa kwenye mashindano mbalimbali.
Rage alitoa kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ishara ya kuanzisha harambee hiyo na kufuatiwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa NEC kutokea wilayani Kibaha Rugemalila Rutatina ambaye alitoa kiasi cha shilingi 100,000.
Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka yeye aliahidi kutoa kutoa kiasi cha shilingi 100,000 na wanachama, wapenzi na mashabiki wa timu hiyo nao walichangia fedha na kufikia kiasi hicho.
“Fedha hizi zilizochangwa zinapaswa kutumika kwa ajili ya malengo yaliyowekwa ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti pamoja na mambo mbalimbali ya tawi,” alisema Rage.
Aliwataka wadau wa Simba kujitokeza kuisaidia timu yao ili kuhakikisha inafanikiwa kutetea ubingwa wake wa ligi kuu ya Voda Com ambao kwa sasa inaonekana kama imeuweka rehani baada ya kufungwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Mwisho.

MBUNGE AREJEA KAZINI BAAADA YA KUUGUA KWA MIEZI SABA

HATIMAYE Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Said Bwanamdogo ameanza kazi baada ya kurejea toka nchini India  alipokuwa akipatiwa matibabu tangu alipougua miezi saba iliyopita wakati wa kikao cha Bunge mjini Dodoma Julai mwaka jana ameanza kazi kwa kuahidi kutekeleza ahadi zote zilizobaki alizoahidi.

  alitoa ahadi ya kutoa kiasi cha shilingi milioni nne kwa ajili ya kumalizia nyumba ya Mwalimu kwenye shule ya msingi Java na mifuko 50 ya saruji katika shule ya msingi Kwamakuru,Manda Mazingara ,Kata ya Mkange ili kukarabati madarasa matano ambayo yamebomoka.

Bwanamdogo alisema mbali ya mchango huo pia atatoa 200,000 za kununulia nyavu,400,000 ya umeme wa jua katika shule ya msingi Saadan, mabati 70 katika ujenzi wa soko la Saadan na mifuko 50 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Mkange.

Alisema ahadi hizo ni za awamu ya pili baada ya kukamilisha ahadi mbalimbali alizozitoa kipindi cha uchaguzi na kuzikamilisha kupitia fedha za mfuko wa jimbo fedha , wafadhili na binafsi.

"Lengo la kutoa vitu hivyo pamoja na fedha ni kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kutatua kero za wananchi zinatumika ipasavyo ili kuondoa kero ambazo zinaweza kutatuliwa na viongozi waliochaguliwa na wananchi katika chaguzi mbalimbali," alisema Bwanamdogo

Aliwataka viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM na serikali wajenge ushirikiano katika kufanya maamuzi na majukumu mbalimbali ili kuleta maendeleo hatimaye kukuza uchumi wa jimbo hilo.

"Msiwe na tabia ya kusemana ndani ya jamii na badala yake watumie vikao halali vya chama katika kuwekana sawa kama endapo kuna kiongozi anamapungufu ili kuleta heshima ya chama," alisema Bwanamdogo.

Mbunge huyo wa jimbo la Chalinze hicho ni kikao chake cha kwanza kuzungumza tangu arejee nchini India kwa matibabu mara baada ya kuugua kwa takriban miezi Saba kuaznia July 2012 alipoanza kuugua ghafla kwenye bunge lililofanyika mwezi huo.


Picha zikimuonyesha Mbunge Said Bwanamdogo akizungumza juzi katika kikao cha kwanza cha Halmashauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Mkange Tarafa ya Miono picha na John Gagarini.
4 attachments — Download all attachments   View all images   Share all images  
E89A9800.JPGE89A9800.JPG
1645K   View   Share   Download  
E89A9785.JPGE89A9785.JPG
1792K   View   Share   Download  
E89A9779.JPGE89A9779.JPG
1581K   View   Share   Download  
E89A9774.JPGE89A9774.JPG
1431K   View   Share   Download