BRAILO MEDIA

HABARI ZETU

Saturday, June 25, 2016

ZEGERENI KUJENGA SHULE YA MSINGI

Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha umefayatua matufali 2,500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa shule ya Msingi katika mtaa huo ambao unategemea mtaa wa Visiga kuwapeleka watoto wao umbali wa kilometa nane.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa zoezi la kuwapa zawadi wanafunzi wa darasa la saba ambao wamefanya vizuri na kuwa kwenye 10 bora mwenyekiti wa mtaa huo Rashid Likunja amesema kuwa wanatarajia kuanza ujenzi wa shule hiyo kuanzia Julai Mwaka huu ili ifikapo mwakani watoto wao waanze kusoma kwenye shule hiyo.

Likunja amesema kuwa fedha za kununulia kiwanja chenye ukubwa wa hekari sita zimetokana na mchango wa shilingi 5,000 kila kaya ambapo hatua ya ujenzi itaanza kwa kutumia tofaali hizo huku wakiwa na mifuko 12 ya simenti wakianza na madarasa mawili, ofisi na matundu manne ya vyoo.

Amesema kuwa kwa sasa wako kwenye harakati za kupata kibali cha ujenzi pamoja na ramani toka Halmashauri ya Mji ili waweze kuanza ujenzi huo na utawapunguzia watoto wao kwenda kusoma mbali pia huwabidi kuvuka barabara ya Morogoro ambapo ni hatari kwao kwani wengine ni wadogo sana.

Aidha amewataka wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ili waweze kutekeleza azma yao ya ujenzi wa shule hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwa watoto wanaotoka mtaa huo ambao wanafikia zaidi ya 200 wanaosoma madarasa mbalimbali kutoka mtaa huo ambao wanasoma shule jirani ya Visiga.


Mwisho.   
Posted by BRAILO MEDIA at 8:45 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Thursday, June 23, 2016

MILIKINI MAENEO KIHALALI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI-RC

Na John Gagarini, Kibaha

MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakazi wa mkoa huo kufuta taratibu na sheria za kumiliki ardhi ili kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo kwa sasa imeshamiri na inaweza kuhatarisha amani.

Aidha amesema kuwa mkoa hautasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu ambao wanavamia maeneo ya watu na kuyauza kama wanavyofanya baadhi ya watu kwani ni kinyume cha sheria na watachukuliwa hatua kali ili waachane na tabia hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na baadhi wananchi kutoka wilaya ya Mkuranga Ndikilo alisema kuwa kumekuwa na migogoro mingi ambayo imesababisha wananchi kutokuelewana wao kwa wao.

“Moja ya mfano ni Kijiji cha Kazole Kitongoji cha Magodani Kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga kuna baadhi ya watu wanajifanya kamati ya ardhi ya Kijiji hicho kulivamia shamba la kampuni ya Soap Allied Industry ambalo lina ukubwa wa hekari 1,750 likiwa na hati ya umiliki 271 ambayo iliipata tangu mwaka 1988 ambalo lilitengwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji,”alisema Ndikilo.

Ndikilo alisema kuwa kamati hiyo ambayo imekuwa ikiuza viwanja kwenye eneo hilo inafanya makosa kwa kuwauzia watu kwani wanachokifanya ni kinyume cha sheria kwani eneo hilo lina mmiliki halali ambaye anamiliki kisheria.

“Kama haitoshi watu hao walikwenda kwenye vyombo vya sheria lakini walishindwa na kuambiwa kuwa eneo hilo ni mali ya mtu hivyo hawapaswi kuingie kwenye eneo hilo lakini wanakamati hao bado wanaendelea kuwauzia watu na kujipatia mamilioni ambayo yote yanaingia mifukoni mwao na wamejinufaisha kupitia shamba hilo lakini wanawaibia watu kwani mmiliki mwenyewe yupo,” alisema Ndikilo.

Aidha alisema kuwa suala la shamba hilo linachukuliwa kisiasa lakini mwisho wa siku linaweza kusababisha uvunjifu wa amani kwani watu waliotoa fedha zao watakapoambiwa waondoke watadai fedha zao na hakuna mtu wa kuwarejeshea hivyo kuleta migogoro ambayo haitakiwi.

Kwa upande wake kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa ni vema watu wakafuata sheria bila ya shuruti kwani eneo hilo limeshatolewa maamuzi baada ya watu waliouziwa kwenda mahakamani na kuonekana kuwa kampuni hiyo ndiyo yenye uhalali wa kumiliki eneo hilo hivyo watu kuingia humo ni kuvunja sheria na wanaweza kukamatwa na polisi

Mushongi alisema kuwa watu hawapaswi kuingia kwenye eneo hilo ambapo hivi karibuni zaidi ya watu 20 waliingia kwenye shamba na kukamatwa na kwa kuwa hati ya umiliki bado haijatenguliwa watu wasiingie na kama wanaona wana haki ni vema wakaenda mahakama za juu kudai haki yao lakini si kulivamia.


Mwisho.       


Posted by BRAILO MEDIA at 1:41 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho
Posted by BRAILO MEDIA at 1:39 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho
Posted by BRAILO MEDIA at 1:39 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Monday, June 20, 2016

MWENYEKITI WA MTAA AWAZAWADIA WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI

Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha mkoani Pwani umewapa zawadi mbalimbali wanafunzi wa darasa la saba waliofanya vizuri kwenye mitihani yao ya katikati ya muhula.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa kukabidhi zawadi hizo kwa wanafunzi hao Rashid Likunja alisema kuwa ameweka utartibu huo kwa wanafunzi wa darasa la saba ili kuwapa hamasa ya kufanya vizuri kwenye mtihani wa kumaliza darasa la saba.

Likunja alisema kuwa zawadi anazotoa ni mfuko wake aliouanzisha kwa ajili ya kuwapa hamasa ya wanafunzi wa mtaa huo kusoma kwa bidii na kuongeza ufaulu.

“Unajua mtaa huu hakuna shule ya msingi ambapo wanafunzi huwabidi kwenda kusoma mtaa jirani wa Visiga ambapo wengine wanatembea kilometa nane kila siku hivyo kuwakatisha tamaa watoto hivyo kutotilia makazo elimu,” alisema Likunja.
Aidha alisema kuwa kabla ya kuanza utaratibu huo wanafunzi wa mtaa huo walikuwa wakishika nafasi za nyuma kuanzia 35 na kushuka chini lakini a kwa sasa wameanza kuhamasika na wameweza kuingia kwenye 10 zaidi ya wanafunzi watano.

“Nimeanzisha mfuko wa kuwasaidia wanafunzi wa mtaa wetu naomba na wadau wengine wajitokeze kusaidia ili zawadi ziwe kubwa kwani nianazotoa ni ndogo lakini naamini wadau zaidi watajitokeza kuniunga mkono juu ya suala la elimu ambalo nimelipa kipaumbele cha kwanza,” alisema Likunja.

Moja ya wazazi ambao mwanae kapewa zawadi baada ya kuwa moja ya wanafunzi walioingia kwenye 10 bora Mwajabu Suleiman alisema kuwa mwenyekiti wao amewapa changamoto kubwa ya kuwahamasisha wanafunzi kusoma kwa bidii.

Suleiman alisema kuwa watamuunga mkono mwenyekiti wao kwa kuwahamasisha watoto wao kusoma kwa bidii ili wawe chachu ya wanafunzi wenzao wanaoanza madarasa ya awali.


Mwisho.    
Posted by BRAILO MEDIA at 7:29 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

SIDO YATUMIA DOLA MILIONI 2

Na John Gagarini, Kibaha

SHIRIKA la Kuendeleza  Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kwa kushirikiana na wafadhili wake limetumia kiasi cha dola milioni mbili za Kimarekani kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uzalishaji bidha za vyakula zisizo na madhara kwa wajasiriamali zaidi ya 700.

Mratibu wa mafunzo hayo Happines Mchomvu alisema kuwa mafunzo hayo ambayo yametolewa kwa kipindi cha miaka miwili kwa lengo la kuhakikisha bidhaa wanazozalisha zinakuwa hazina madhara kwa watumiaji zinakuwa na usalama.

Mchomvu alisema kuwa mbali ya kuwa na usalama pia zinakuwa na viwango vya wa ubora wa kimataifa ili viweze kuuzwa sehemu yoyote ile duniani.

“Mafunzo hayo yalikuwa na malengo ya kuboresha bidhaa za maembe, viungo na asali ambapo wameweza kuwajengea uwezo wajasiriamali hao kutoka mikoa ya Tabora, Singida, Shinyanga, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam,” alisema Mchomvu.

Aidha alisema lengo ni kuhakikisha wajasiriamali kote nchini kuanzia ngazi ya mikoa hadi kwenye mitaa wanazalisha bidhaa zenye ubora na viwango kwa lengo la kuwa na soko la uhakikka la ndani na nje ya nchi ambapo bidhaa za Tanzania zinapendwa kutokana na uhalisia wake.

Kwa upande wake ofisa udhibiti wa ubora kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Magdalena Sademaki alisema kuwa kupitia mafunzo hayo wajasiriamali hao wameweza kutengeneza mifumo yao kimataifa kwa kupambana na vihatarishi ili visiweze kuingia kwenye vyakula.
Sademaki alisema kuwa katika kuhakikisha wajasiriamali hao wanatengeneza bidhaa zenye viwango wanashirikiana na SIDO kuwatambua ili waweze kufikia viwango vya uzalishaji wa bidhaa bora ili ziendane na viwango vya kimataifa.

Na mmoja wa wajasiriamli ambaye amehudhuria mafunzo hayo Zaloki Mohamed ameishukuru SIDO kwa kuwapatia elimu juu ya viwango vya bidhaa  wanazozalisha kwa kuzingatia  utaratibu wa viwango vya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO).

Mohamed  ameiomba serikali iwapunguzie tozo zinazotozwa kwa wajasiriamali ili wapate hati ya viwango ya bidhaa wanazozalisha na kuweza kufikia malengo  ya Tanzania ya kuwa na viwanda.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ufadhili wa Shirika la Biashara la Kimataifa (ITC) kupitia mpango wa kuendesha biashara wa shirika la World Trade Organisation (WTO) kwa kushirikiana na SIDO.

Mwisho. 





 

   




Posted by BRAILO MEDIA at 10:44 AM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Saturday, June 18, 2016

WAVUNJUA VIOO VYA MADIRISHA WAPAKA KINYESI OFISI YA KATA

Na John Gagarini, Kibaha
WATU wasiofahamika wamevunja vioo vya madisrisha na kupaka kinyesi kwenye ya ofisi ya kata ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani na kusababisha watumishi wa kata hiyo kushindwa kuingia ofisini mwishoni mwa wiki.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema alipofika ofisni majira ya saa moja asubuhi Juni 17 alikuta ofisi hiyo imepakazwa vinyesi vya binadamu na vioo vya madirisha ya vioo nane kuvunjwa kwa kupigwa mawe na watu hao.

Mtae alisema inadhaniwa kuwa kitendo hicho kimefanywa na baadhi ya watu waliovunjiwa nyumba zao ambao walikuwa na hasira ya kuvunjiwa nyumba zao na Halmashauri ya Mji wa Kibaha na kudai kuwa ofisi hiyo haikuwasaidia lolote.

“Eneo hilo lipo chini ya halmashauri ya Mji hivyo wananchi hao walikuwa wamevamia na kuishi hapo kinyume na sheria hawa wananchi walipoona wamevunjiwa nyumba zao wakaanza kulalamika kwanini ofisi yangu haiwasaidii,kiukweli wapo kinyume na taratibu tusingeweza kuwaunga mkono kwa hilo”alisema Mtae.

Aidha alisema kuwa baada ya kuona hali ile walikwenda kutoa taarifa kwenye ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha na polisi juu ya tukio hilo ambapo hadi sasa haijaweza kufahamika nani aliyetekeleza uharibifu huo. 

“Tumeshatoa taarifa polisi na mlinzi Richard Maduhu anahojiwa polisi kuhusiana na tukio hilo kwani wakati tukio hilo linatokea hakuweza kutoa taarifa sehemu yoyote hadi wao walipofika ofisini hapo,” alisema Mtae.

Naye diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi alisema kuwa kitendo hicho si cha kiungwana kwani hata kama wananchi hao walikuwa na madai yao ni vema wakafuata taratibu kuliko kuharibu ofisi ambayo inatoa huduma kwa wananchi.

Lutambi alisema kuwa suala hilo tayari wamelipeleka polisi ili kufuatilia kujua nani aliyefanya hivyo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake kwani hali hiyo ina hatarisha hali ya usalama wa watendaji wa ofisi ya kata ambapo kwa siku hiyo hawakuweza kufanya kazi kutokana na tukio hilo.
Mwisho.





   



Click here to Reply or Forward
2.67 GB (17%) of 15 GB used
Manage
Terms - Privacy
Last account activity: 41 minutes ago
Details
mhariri
Add to circles
Show details
Posted by BRAILO MEDIA at 2:14 PM No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

Translate

Followers

Blog Archive

  • ▼  2026 (88)
    • ▼  June (19)
      • VIJANA WENYE VIPAJI VYA MICHEZO WATAKIWA KUWA NA N...
      • MWANADIPLOMASIA OMARY PUNZI ATEULIWA KUSHIRIKI MKU...
      • MAWAZO YA VIJANA
      • WALIPA KODI WATAKIWA KUONYESHA UZALENDO KWA KULIPA...
      • MAWAZO VIJANA CHALLENGE KUTUMIKA KIMAENDELEO
      • MAWAKALA WAITWA KUCHANGAMKIA VIPAJI TUMBI KIBAHA
      • WAZO BORA LA KIJANA KUNYAKUA MILIONI 50
      • VIJANA 100 KUWANIA MILIONI 50 VIJANA UCHUMI CHALLANGE
      • PWANI YAKUSANYA BILIONI 266
      • TAARIFA KWA UMMA
      • PWANI YAENDELEA KUHAMASISHA UCHANGIAJI DAMU KUOKOA...
      • *SERIKALI YADHAMIRIA KUWAENDELEZA WACHIMBAJI WADOG...
      • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIBAHA YATOA MIKOPO YA ...
      • LULU YA WAJANE KUANZISHA MRADI WA MINOFU YA KUKU
      • POLISI PWANI KUFANYA UCHUNGUZI KISAYANSI KUCHUNGUZ...
      • MAFANIKIO YA GLOBAL PARTNERSHIP FOR EDUCATION CHIN...
      • RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN AWEKA SHADA LA MAUA KA...
      • DK SAMIA SULUHU HASSAN KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMI...
      • RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI URUSI
    • ►  May (11)
    • ►  April (10)
    • ►  March (17)
    • ►  February (14)
    • ►  January (17)
  • ►  2025 (83)
    • ►  December (5)
    • ►  October (2)
    • ►  August (2)
    • ►  June (7)
    • ►  May (12)
    • ►  April (11)
    • ►  March (19)
    • ►  February (10)
    • ►  January (15)
  • ►  2024 (210)
    • ►  December (19)
    • ►  November (5)
    • ►  October (8)
    • ►  September (6)
    • ►  August (25)
    • ►  July (23)
    • ►  June (15)
    • ►  May (12)
    • ►  April (27)
    • ►  March (33)
    • ►  February (27)
    • ►  January (10)
  • ►  2023 (322)
    • ►  December (7)
    • ►  November (11)
    • ►  October (17)
    • ►  September (38)
    • ►  August (62)
    • ►  July (51)
    • ►  June (34)
    • ►  May (17)
    • ►  April (13)
    • ►  March (36)
    • ►  February (26)
    • ►  January (10)
  • ►  2022 (31)
    • ►  December (4)
    • ►  November (16)
    • ►  October (10)
    • ►  May (1)
  • ►  2019 (1)
    • ►  September (1)
  • ►  2017 (75)
    • ►  December (2)
    • ►  November (9)
    • ►  October (16)
    • ►  September (3)
    • ►  August (15)
    • ►  July (13)
    • ►  June (2)
    • ►  April (1)
    • ►  March (8)
    • ►  February (2)
    • ►  January (4)
  • ►  2016 (162)
    • ►  December (9)
    • ►  October (2)
    • ►  September (4)
    • ►  August (14)
    • ►  July (17)
    • ►  June (18)
    • ►  May (34)
    • ►  April (14)
    • ►  March (16)
    • ►  February (21)
    • ►  January (13)
  • ►  2015 (106)
    • ►  December (14)
    • ►  November (1)
    • ►  October (15)
    • ►  September (12)
    • ►  August (6)
    • ►  July (11)
    • ►  June (3)
    • ►  May (7)
    • ►  April (7)
    • ►  March (5)
    • ►  February (8)
    • ►  January (17)
  • ►  2014 (117)
    • ►  December (21)
    • ►  November (10)
    • ►  October (13)
    • ►  September (7)
    • ►  August (16)
    • ►  July (19)
    • ►  June (6)
    • ►  May (14)
    • ►  April (6)
    • ►  January (5)
  • ►  2013 (138)
    • ►  December (11)
    • ►  November (6)
    • ►  October (1)
    • ►  September (5)
    • ►  August (6)
    • ►  July (16)
    • ►  June (3)
    • ►  May (11)
    • ►  April (9)
    • ►  March (16)
    • ►  February (26)
    • ►  January (28)
  • ►  2012 (16)
    • ►  December (16)
Powered By Blogger

Pages

  • HABARI

About Me

BRAILO MEDIA
View my complete profile
GAGARINI. Picture Window theme. Powered by Blogger.