Na John
Gagarini, Kibaha
MKUU wa
mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakazi wa mkoa huo kufuta
taratibu na sheria za kumiliki ardhi ili kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo
kwa sasa imeshamiri na inaweza kuhatarisha amani.
Aidha amesema
kuwa mkoa hautasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu ambao wanavamia
maeneo ya watu na kuyauza kama wanavyofanya baadhi ya watu kwani ni kinyume cha
sheria na watachukuliwa hatua kali ili waachane na tabia hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa
na baadhi wananchi kutoka wilaya ya Mkuranga Ndikilo alisema kuwa kumekuwa na
migogoro mingi ambayo imesababisha wananchi kutokuelewana wao kwa wao.
“Moja
ya mfano ni Kijiji cha Kazole Kitongoji cha Magodani Kata ya Vikindu wilaya ya
Mkuranga kuna baadhi ya watu wanajifanya kamati ya ardhi ya Kijiji hicho
kulivamia shamba la kampuni ya Soap Allied Industry ambalo lina ukubwa wa
hekari 1,750 likiwa na hati ya umiliki 271 ambayo iliipata tangu mwaka 1988
ambalo lilitengwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji,”alisema Ndikilo.
Ndikilo
alisema kuwa kamati hiyo ambayo imekuwa ikiuza viwanja kwenye eneo hilo inafanya
makosa kwa kuwauzia watu kwani wanachokifanya ni kinyume cha sheria kwani eneo
hilo lina mmiliki halali ambaye anamiliki kisheria.
“Kama
haitoshi watu hao walikwenda kwenye vyombo vya sheria lakini walishindwa na
kuambiwa kuwa eneo hilo ni mali ya mtu hivyo hawapaswi kuingie kwenye eneo hilo
lakini wanakamati hao bado wanaendelea kuwauzia watu na kujipatia mamilioni
ambayo yote yanaingia mifukoni mwao na wamejinufaisha kupitia shamba hilo
lakini wanawaibia watu kwani mmiliki mwenyewe yupo,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema
kuwa suala la shamba hilo linachukuliwa kisiasa lakini mwisho wa siku linaweza kusababisha
uvunjifu wa amani kwani watu waliotoa fedha zao watakapoambiwa waondoke watadai
fedha zao na hakuna mtu wa kuwarejeshea hivyo kuleta migogoro ambayo haitakiwi.
Kwa upande
wake kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa ni vema
watu wakafuata sheria bila ya shuruti kwani eneo hilo limeshatolewa maamuzi
baada ya watu waliouziwa kwenda mahakamani na kuonekana kuwa kampuni hiyo ndiyo
yenye uhalali wa kumiliki eneo hilo hivyo watu kuingia humo ni kuvunja sheria
na wanaweza kukamatwa na polisi
Mushongi
alisema kuwa watu hawapaswi kuingia kwenye eneo hilo ambapo hivi karibuni zaidi
ya watu 20 waliingia kwenye shamba na kukamatwa na kwa kuwa hati ya umiliki
bado haijatenguliwa watu wasiingie na kama wanaona wana haki ni vema wakaenda
mahakama za juu kudai haki yao lakini si kulivamia.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment