Saturday, June 25, 2016

WAKANUSHA KUPAKA KINYESI NA KUVUNJA OFISI YA KATA

Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI wa Mtaa wa Machinjioni Loliondoa au Sagulasagula waliobomolewa nyumba zao na Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani kwa tuhuma za kujenga nyumba kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko wamekanusha kuapaka kinyesi na kuvunja vioo vya ofisi ya kata ya Maili Moja.

Akizungumza na waandishi wa habari moja ya wahanga wa tukio la bomoa bomoa hiyo iliyofanyika Juni 16 na 17 mwaka huu ambapo watu hao walifanya uharibifu huu siku moja baada ya bomobomoa hiyo huku jumla ya nyumba 18 zilibomolewa, Said Tekelo amesema kuwa wao hawahusiki na tukio hilo na wamesikitishwa na kitendo hicho.

Tekelo amesema kuwa kitendo hicho kimefanywa na watu ambao walikuwa na malengo yao na hawaungi mkono watu waliofanya uharibifu huo kwani ni tukio ambalo ni kinyume cha sheria na hakistahili kuunga mkono.

Amesema kuwa wao kama wahanga wa bomobomoa hiyo hawawezi kufanya hivyo kwa sababu bado wako katika kutafuta haki yao waliyoipoteza baada ya nyumba zao kubomolewa pasipo kupewa fidia yoyote hivyo wasingeweza kufanya uharibifu.

Aidha amesema kuwa vi vema vyombo vya kisheria vikafanya yake ili kubaini wale waliofanya hivyo na kuwachukulia hatua kazi za kisheria kwani hao ni wahalifu kama wahalifu wengine na hawahusiani na waliobomolewa nyumba zao.

Amebainisha kuwa suala lao liko mahakamani tangu zoezi la kubomolewa nyumba zao lilipofanyika na hawaungi mkono watu waliofanya hivyo na wanawalaani vikali watu hao ambao wamejificha kwenye mwamvuli wa uhalifu.


MWISHO

No comments:

Post a Comment