BRAILO MEDIA

HABARI ZETU

Saturday, June 18, 2016

MIGOGORO YA NDOA ISIWANYIME HAKI ZA MSINGI WATOTO

Na John Gagarini, Bagamoyo

WAZAZI na walezi wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametakiwa kutowanyima haki za msingi ikiwa ni pamoja na elimu watoto wao kutokana na migogoro yao ya ndoa.

Hayo yalisemwa na mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo Abdul Sharifu wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika kwenye wilaya hiyo yaliyofanyika shule ya Msingi Mwanamakuka Bagamoyo.

Sharifu alisema kuwa ugomvi baina ya wazazi imekuwa ikisababisha watoto wengi kukosa haki zao za msingi ikiwa ni pamoja na elimu hali ambayo imesababisha  wakose  maadili mazuri.

“Kutokana na migogoro ya kifamilia au ndoa imekuwa ikisababisha watoto wengi kukosa elimu ambayo ndiyo urithi pekee ambao anaweza kurithishwa mtoto na si mali ambazo zinaweza kwisha lakini elimu ni urithi wa kudumu,” alisema Sharifu.

Alisema kuwa mbali ya changamoto ya watoto kukosa elimu pia watoto wa kike hujikuta wakipata mimba za utotoni ambazo ni hatari kwa masiha yao kutokana na maumbile yao.

“Tunataka mashirika yasiyo ya kiserikali na serikali kuwachukua wale wote wanaobainika kuwapa mimba lazima hatua kali za kisheria zichukuliwe kwa kufuata mkondo wake ili kukomesha tabia hiyo mbaya,” alisema Sharifu.

Aidha alisema kuwa  watoto wenye ulemavu wa viungo na walemavu wengine wana haki kama wengine  hivyo jamii isiwanyanyapae ni lazima haki zao zitazamwe na kuwashirikisha katika mikutano mbalimbali na shughuli za kijamii ili kuibua vipaji vyao viweze kuwasaidia kuacha vitendo vya kuwaajiri watoto.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Kaya Fm, Marie Shaba alisema katika bara la Afrika, Kusini, Mashariki, mitaa, kwenye familia watoto walio wengi hawaishi kwa raha na wanakosa haki zao ambapo sherehe hizo zinapaswa kuwakumbusha kwa yaliyotokea nchini Afrika ya Kusini huko Soweto ambapo watoto 700 walifariki kwa kudai haki zao.
Kwa upande wa watoto akiwemo Fatuma Sadik, kutoka shule ya msingi Mbaruku alisema kufiwa na wazazi pia husababisha baadhi ya watoto kufukuzwa na ndugu na jamaa kwa tamaa za mali zilizoachwa na wazazi.

Alisema suala hilo husababisha watoto kukosa haki zao msingi za kuishi kwa amani na upendo na kwa mtazamo wa haraka hiyo si migogoro bali ni vita, machafuko na ukosefu wa amani na haki za msingi dhidi ya watoto na aliiomba jamii ilinde haki zao na kuzifanyia kazi kisheria ikiwemo haki ya kupata elimu, kulindwa, kusikilizwa na kupendwa pasipo kubaguliwa.

Mwisho



Posted by BRAILO MEDIA at 2:10 PM
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Translate

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (72)
    • ►  June (5)
    • ►  May (12)
    • ►  April (11)
    • ►  March (19)
    • ►  February (10)
    • ►  January (15)
  • ►  2024 (210)
    • ►  December (19)
    • ►  November (5)
    • ►  October (8)
    • ►  September (6)
    • ►  August (25)
    • ►  July (23)
    • ►  June (15)
    • ►  May (12)
    • ►  April (27)
    • ►  March (33)
    • ►  February (27)
    • ►  January (10)
  • ►  2023 (322)
    • ►  December (7)
    • ►  November (11)
    • ►  October (17)
    • ►  September (38)
    • ►  August (62)
    • ►  July (51)
    • ►  June (34)
    • ►  May (17)
    • ►  April (13)
    • ►  March (36)
    • ►  February (26)
    • ►  January (10)
  • ►  2022 (31)
    • ►  December (4)
    • ►  November (16)
    • ►  October (10)
    • ►  May (1)
  • ►  2019 (1)
    • ►  September (1)
  • ►  2017 (75)
    • ►  December (2)
    • ►  November (9)
    • ►  October (16)
    • ►  September (3)
    • ►  August (15)
    • ►  July (13)
    • ►  June (2)
    • ►  April (1)
    • ►  March (8)
    • ►  February (2)
    • ►  January (4)
  • ▼  2016 (162)
    • ►  December (9)
    • ►  October (2)
    • ►  September (4)
    • ►  August (14)
    • ►  July (17)
    • ▼  June (18)
      • WAKANUSHA KUPAKA KINYESI NA KUVUNJA OFISI YA KATA
      • ZEGERENI KUJENGA SHULE YA MSINGI
      • MILIKINI MAENEO KIHALALI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI-RC
      • KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI
      • KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI
      • MWENYEKITI WA MTAA AWAZAWADIA WANAFUNZI WALIOFANYA...
      • SIDO YATUMIA DOLA MILIONI 2
      • WAVUNJUA VIOO VYA MADIRISHA WAPAKA KINYESI OFISI Y...
      • BOMOABOMOA YALIZA WENGI KIBAHA
      • MIGOGORO YA NDOA ISIWANYIME HAKI ZA MSINGI WATOTO
      • WATATU WASHIKILIWA KWA MAUAJI YA DEREVA WA NOAH
      • RC ATAKA MKATABA WA UWEKEZAJI KUPITIWA UPYA
      • WATAKA TAARIFA KUHUSU ENEO LA UWEKEZAJI BAADA YA M...
      • WAWEKEZAJI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUDUM...
      • TCRA YATOA MAFUNZO KUHUSU KUFUTWA SIMU FEKI
      • JUMUIYA YA WAZAZI YASISITIZA UBORA WA ELIMU CHUO C...
      • WATAKA TAARIFA RASMI MRADI WA MIWA KUFUTWA
      • WAWEKEZAJI WADHIBITI USALAMA WA NCHI
    • ►  May (34)
    • ►  April (14)
    • ►  March (16)
    • ►  February (21)
    • ►  January (13)
  • ►  2015 (106)
    • ►  December (14)
    • ►  November (1)
    • ►  October (15)
    • ►  September (12)
    • ►  August (6)
    • ►  July (11)
    • ►  June (3)
    • ►  May (7)
    • ►  April (7)
    • ►  March (5)
    • ►  February (8)
    • ►  January (17)
  • ►  2014 (117)
    • ►  December (21)
    • ►  November (10)
    • ►  October (13)
    • ►  September (7)
    • ►  August (16)
    • ►  July (19)
    • ►  June (6)
    • ►  May (14)
    • ►  April (6)
    • ►  January (5)
  • ►  2013 (138)
    • ►  December (11)
    • ►  November (6)
    • ►  October (1)
    • ►  September (5)
    • ►  August (6)
    • ►  July (16)
    • ►  June (3)
    • ►  May (11)
    • ►  April (9)
    • ►  March (16)
    • ►  February (26)
    • ►  January (28)
  • ►  2012 (16)
    • ►  December (16)
Powered By Blogger

Pages

  • HABARI

About Me

BRAILO MEDIA
View my complete profile
GAGARINI. Picture Window theme. Powered by Blogger.