Na John
Gagarini, Kibaha
WAKAZI 200
wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani
Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa
maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO)
wilaya ya Kibaha kukamilika.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto
Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na
uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya
kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.
Emanuel
alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo
hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya
kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa
wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.
“Maji
haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya
miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa
mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.
Awali wananchi
hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro
kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila
ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.
Wakizungumza
na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin,
Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika
kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya
mkopo toka Dawasco.
Walisema
kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba
kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani
ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna
kinachoendelea hadi sasa.
“Kinachotushangaza
ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji
huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji
uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa
kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.
Mwisho
No comments:
Post a Comment