Na John
Gagarini, Kibaha
MTAA wa
Zegereni wilayani Kibaha mkoani Pwani umewapa zawadi mbalimbali wanafunzi wa
darasa la saba waliofanya vizuri kwenye mitihani yao ya katikati ya muhula.
Akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa kukabidhi zawadi hizo kwa wanafunzi
hao Rashid Likunja alisema kuwa ameweka utartibu huo kwa wanafunzi wa darasa la
saba ili kuwapa hamasa ya kufanya vizuri kwenye mtihani wa kumaliza darasa la
saba.
Likunja alisema
kuwa zawadi anazotoa ni mfuko wake aliouanzisha kwa ajili ya kuwapa hamasa ya
wanafunzi wa mtaa huo kusoma kwa bidii na kuongeza ufaulu.
“Unajua mtaa
huu hakuna shule ya msingi ambapo wanafunzi huwabidi kwenda kusoma mtaa jirani
wa Visiga ambapo wengine wanatembea kilometa nane kila siku hivyo kuwakatisha
tamaa watoto hivyo kutotilia makazo elimu,” alisema Likunja.
Aidha alisema
kuwa kabla ya kuanza utaratibu huo wanafunzi wa mtaa huo walikuwa wakishika
nafasi za nyuma kuanzia 35 na kushuka chini lakini a kwa sasa wameanza
kuhamasika na wameweza kuingia kwenye 10 zaidi ya wanafunzi watano.
“Nimeanzisha
mfuko wa kuwasaidia wanafunzi wa mtaa wetu naomba na wadau wengine wajitokeze
kusaidia ili zawadi ziwe kubwa kwani nianazotoa ni ndogo lakini naamini wadau
zaidi watajitokeza kuniunga mkono juu ya suala la elimu ambalo nimelipa
kipaumbele cha kwanza,” alisema Likunja.
Moja ya
wazazi ambao mwanae kapewa zawadi baada ya kuwa moja ya wanafunzi walioingia
kwenye 10 bora Mwajabu Suleiman alisema kuwa mwenyekiti wao amewapa changamoto
kubwa ya kuwahamasisha wanafunzi kusoma kwa bidii.
Suleiman alisema
kuwa watamuunga mkono mwenyekiti wao kwa kuwahamasisha watoto wao kusoma kwa
bidii ili wawe chachu ya wanafunzi wenzao wanaoanza madarasa ya awali.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment