Wednesday, February 8, 2023

MAMLAKA YA USIMAMIZI BAHARI KUU KUJENGA KIWANDA KUCHAKATA SAMAKI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAMLAKA ya kusimamia uvuvi wa Bahari Kuu inatarajia Kujenga Kiwanda kikubwa cha kuchakata Samaki Mkoani Tanga ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani zaidi ya 100 kwa siku ambacho kitagharimu Dola Milioni 10 na kutoa fursa ya ajira kwa Watanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo,Dk Emanuel Sweke wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka ya usimamizi wa Bahari Kuu. 

Sweke amesema kuwa katika kudhibiti uvuvi haramu  Mamlaka hiyo imeweza kuweka mifumo madhubuti ambayo inaendana na Teknolojia kwakufanya doria mbalimbali kwa ajili ya kukomesha uvuvi haramu.

"Kutokana na shughuli zake Mamlaka hiyo imeweza kuvunja rekodi ya kukusanya mapato mengi kwa kipindi cha mwaka 2022 hadi kufikia shilingi bilioni 4.1 na wametoa jumla ya leseni za uvuvi 5336,"alisema Sweke.

Mamlaka ya kusimamia uvuvi wa Bahari Kuu imeanzishwa rasmi Mwaka 2010 lengo lake likiwa ni kusimamia shughuli zote za uvuvi wa Bahari Kuu na ufuatiliaji.

No comments:

Post a Comment