Na Mwandishi Wetu Dodoma
MFUKO wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) unatarajia kutumia shilingi milioni 575 kwa ajili ya mradi wa kupeleka vifaa maalum vya TEHAMA vya kujifunzia kwa Shule 16 zenye watoto wenye mahitaji maalum hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Mtendaji mkuu wa mfuko wa mawasiliano kwa wote ( UCSAF) Justina Mashimba leo Februari 13,2023 Jijini Dodoma, wakati akielezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali za mfuko huo.
Mashimba amesema kuwa vifaa vitakavyopelekwa katika shule hizo ni pamoja na TV, mashine ya (Nukta Nundu) Orbit reader (Machine za Kisasa), Laptops, (Printa ya nukta nundu).
"Jumla ya shule 811 zimefikishiwa vifaa vya TEHAMA ambapo kwa wastani kila shule imepewa Kompyuta 5, Printa 1 na Projekta 1 kwa mwaka wa fedha wa 2022/23 ambapo Shule 150 zitafikishiwa vifaa vya TEHAMA bajeti yake ikiwa ni shilingi 1.9 na vifaa hivyo vitasaidia wanafunzi kusoma katika shule hizo,"amesema Mashimba
Amezitaka Shule hizo zitakazonufaika ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Mpwapwa (Mpwapwa-Dodoma), Sekondari ya Mkolani (Mwanza), Sekondari ya Kashaulili (Mpanda-Katavi), Sekondari ya Morogoro (Morogoro), Sekondari ya Shinyanga (Kishapu-Shinyanga), Sekondari ya Wavulana Songea (Songea), Sekondari ya Kazima (Tabora) na Sekondari ya Haile Selassie (Mjini Magharibi)
Aidha akizungumzia hali ya mawasiliano nchini amesema kuwa mwaka 2009 Huduma za Simu ilikuwa asilimia 45 wakati kwa sasa imeongezeka hadi kufikia asilimia 96,Teknolojia ya 2G ni asilimia 96,3G ni asilimia 72,4G ni asilimia 55 na Geographical Coverage ya 2G ni asilimia 69; 3G ni asilimia 55 na 4G ni asilimia 36.
Amesema kuwa upande wa ujenzi wa minara Vijiji UCSAF imeingia mikataba kufikisha huduma katika kata 1,242 zenye Vijiji 3,654, Wakazi 15,130,250 ambapo Minara 1,087 yenye Vijiji 3,378 na wakazi 13,320,750 na Utekelezaji unaendelea katika Minara 155 yenye Vijiji 276 na wakazi 1.8 kwa ruzuku iliyotolewa ya shilingi bilioni 199 ikiwemo pia mradi wa kimkakati wa Zanzibar Minara 42, Shehia 38 ruzuku bilioni 6.9
No comments:
Post a Comment