Thursday, February 23, 2023

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO KUONGEZA UWEZO WA MAWASILIANO


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAMLAKA ya serikali Mtandao (eGA) imepanga kupanua uwezo wa Mtandao wa mawasiliano serikalini ( Government Network) na kuufikisha wilaya zote nchini Ili kurahisisha utekelezaji wa jitihada za serikali Mtandao na kuwafikishia huduma wananchi wote popote walipo.

Hayo yamesemwa na Mkurugezi mkuu wa mamlaka ya serikali mtandao Mhandisi Benedict Ndomba wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa mamlaka hiyo.

Ndomba amesema kuwa mfumo wa ubadilishaji taarifa serikalini imewezesha zaidi ya taasisi 50 kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo na amezitaka taasisi za umma ambazo hazijaunganishwa katika mfumo huo ziunganishwe Ili ziweze kubadilishana taarifa na taasisi nyingine pale inapohitajika.

"Jumla ya taasisi 200 zinatumia mfumo wa ofisi Mtandao kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi katika taasisi za umma pia umesaidia kupunguza matumizi ya karatasi kutunza mazingira na kuokoa fedha za serikali,"alisema Ndomba.

Serikali mtandao ni matumizi ya Teknolojia ya habari na mawasiliano ( TEHAMA) Katika utendaji kazi wa taasisi za umma na utoaji wa huduma kwa wananchi wenye lengo la kuongeza ufanisi wa utendaji kazi Katika taasisi ya umma pamoja na kuboresha utoaji huduma kwa umma Ili huduma hizo zipatikane kwa urahisi haraka na gharama nafuu. 

No comments:

Post a Comment