IMEELEZWA kuwa uanzishwaji wa kamati za magonjwa ya milipuko kutasaidia kuielimisha jamii kukabili magonjwa ili yasisambae kwa kasi na kutoleta athari.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alipokuwa akifungua mkutano wa kamati hiyo inayoundwa na wanajamii, wataalamu wa afya, viongozi wa dini na kamati ya usalama ya Wilaya.
John amesema kuwa kwa kuzingatia hilo itasaidia kukabili magonjwa ya mlipuko kwa kutoa elimu juu ya kukabiliana na magonjwa hayo.
Amezitaka kamati ya magonjwa ya milipuko kutoa elimu juu ya magonjwa kulingana na mila desturi na tamaduni za eneo husika.
Kwa upande wake Johnson Mndeme kutoka Wizara ya Afya Idara ya Kinga sehemu ya afya kwa Umma amesema kuwa malengo ya kuanzishwa kamati hizo ni kutoa elimu juu ya magonjwa ya mlipuko ili kuepukana na dhana potofu.
Kwa upande wake maganga mkuu wa Halmashauri ya Mji Kibaha Peter Nsanya amesema kuwa wanakamati wanapaswa kutoa elimu ya kupambana na magonjwa mbalimbali ndani ya jamii.
No comments:
Post a Comment