Na Wellu Mtaki, Dodoma
MAMLAKA ya Serikali Mtandao ( EGA ) kuandaa na kutelekeza mikakati madhubuti ili huduma za Mtandao zote kupatikana ili kudhibiti matishio ya usalama mtandaoni na kurahisisha utoaji wa huduma kwa umma.
Hayo yamesemwa na Mkurugezi mkuu wa mamlaka ya serikali Mhandisi Benedict Benny Ndomba wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu kikao kazi cha tatu cha serikali Mtandao kinachotarajiwa kufanyika Februari 8 hadi 10 mwaka huu katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama ( mb).
Ndomba amesema kuwa takribani wadau 1,000 wa serikali Mtandao kutoka katika mashirika na taasisi za umma wakiwemo maafisa masuuli, wajumbe wa bodi, Wakuu wa vitengo vya tehama, maofisa tehama, rasilimali watu, mipango, mawasiliano, wahasibu pamoja na watumishi wote wa mifumo ya tehama serikali wanatatarajiwa kushiriki kikao hicho.
"Lengo la kikao hicho ni kijadiliana juu ya mafanikio, changamoto pamoja na kuweka mikakati mbalimbali ya kukuza serikali Mtandao nchin Ili kuhakikisha matumizi sahihi na salama ya tehama katika taasisi za umma,"alisema Ndomba.
Aidha alisema kuwa Mamlaka ya serikali Mtandao( (e-GA) ni taasisi iliyopewa jukumu la kuratibu, kusimamia na kukuza juhudi za serikali Mtandao pamoja na kuhimiza uzingatiwaji wa sera, Sheria, kanuni, viwango na miongozo ya serikali Mtandao katika taasisi za umma ili kuhakikisha matumizi sahihi na salama ya tehama yanazingatiwa katika taasisi hizo.
No comments:
Post a Comment