Na Mwandishi Wetu Dodoma
WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) wamefanikiwa kuendelea kutekeleza Malengo waliyojiwekea kwenye mpango mkakati wa mwaka 2021/22 hadi 2025/2026 pamoja na kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 ikiwa ni pamoja na kusimamia na kuhakikisha utengenezaji wa makazi bora kwa watumishi.
Hayo yamebainishwa na katibu mkuu mtendaji (TBA) Daudi Kondoro wakati akizungumza na wandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa majukumu wa wakala huo katika kipindi cha miaka miwili ya serikali ya awamu ya sita.
Kondoro amesema wakala wameendelea kutoa huduma ya uhakika ya makazi kwa serikali na kwa watumishi wa umma kwa kutoa huduma ya uhakika ya makazi na nyumba ambapo mpaka sasa kuna nyumba 1,622 zilizopangishwa kwa watumishi wa umma na pamoja na nyumba 7,700 zilizouzwa kwa watumishi wa umma Tanzania Bara Bara.
"TBA imetengeneza fursa za ajira na kutoa mafunzo kwa vitendo ambapo imetengeneza ajira takribani 100,000 kwa vijana walio na ujuzi na ambao hawana ujuzi kupitia miradi ambayo imekua ikitekelezwa,"alisema Kondoro.
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imeishukuru serikali ya Rais Dkt. Samia kwa kukuendelea kuwawezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ikiwemo kupewa fedha bilioni 54.2 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi.
No comments:
Post a Comment