Tuesday, July 26, 2016

WADAU WACHANGIA BWENI LA SEKONDARI YA CHALINZE ILIYOUNGUA

Na John Gagarini, Kibaha
KUFUATIA kuungua bweni la shule ya sekondari ya Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kuungua kwa moto baadhi ya wadau wameanza kuichangia shule hiyo ili kusaidia wanafunzi ambao vifaa vyao vyote viliungua.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi diwani wa kata ya Bwiringu Lucas Lufunga alisema kuwa kutokana na tukio hilo waliitisha kikao cha kata kwa ajili ya kuangalia namna ya kuisaidia shule hiyo.
Lufunga alisema kuwa katika kikao hicho walifanikiwa kupata kiasi cha shilingi 449,000 na kunua vyakula kwa ajili ya kusaidia kwani vyakula viliungua na moto huo ambao ulitokea usiku wakati wanafunzi wakiwa wanjisomea masomo ya usiku.
“Tunaomba watu mbalimbali wajitokeze kuwasaidia wanafunzi walikuwa wakiishi kwenye bweni hilo kwani kufuatia moto huo hakuna kilichotoka kwani vyote viliteketea kabisa hivyo kuna haja ya kulichukulia kwa uzito wake tatizo hilo,” alisema Lufunga.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwalimu mkuu wa Shule hiyo Emanuel Kahabi alisema kuwa moto huo ulitokea wakati wanafunzi hao wakiwa wanajisomea madarasani usiku.
Kahabi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Julai 12 majira ya saa 2:50 usiku ambapo moto huo haukuweza kufahamika ulitokea wapi na kusababisha hasara kubwa ya bweni hilo na vifaa mbalimbali vikiwemo vya wanafunzi.
“Bweni hilo ambalo lilikuwa bwalo la chakula baada ya wanafunzi hao zaidi ya 100 kuhamishiwa humo kutokana na bweni lao kuungua kwa moto miezi michache iliyopita,” alisema Kahabi.
Alisema kuwa anawashukuru wadau ambao wameanza kuisaidi shule yake kutokana na moto huo ambao hadi sasa haijafahamika chanzo chake ni nini na kuwataka watu wakiwemo wakazi wa Chalinze, wilaya na mkoa amzima kuwasaidia wanafunzi hao.
Mwisho. 

No comments:

Post a Comment