Na John Gagarini, Kibaha
WAKALA wa Misitu Tanzania (TFS) Kanda
ya Mashariki imefanikiwa kukusanya mapato yenye tahamani ya shilingi bilioni 13
kwa mwaka jana kutokana na tozo mbalimbali.
Akizungumza na mwandishi wa habari
hizi ofisini kwake mjini Kibaha meneja wa TFS Kanda ya Mashariki Dk Abel Masota
alisema kuwa tozo hizo ni pamoja na faini zinazotokana na ukiukwaji wa taratibu
za matumizi ya rasilimali za misitu ya hifadhi.
Dk Abel alisema kuwa mapato hayo ni
pamoja na ukataji wa vibali kwa ajili ya wafanyabiashara wa mazao ya misitu 17
kwenye misitu iliyo chini ya wakala hiyo kwenye kanda yake.
“Mapato hayo ni kwa kipindi cha mwaka
uliopita wa 2015 ambapo ni pamoja na leseni za biashara za mazao ya misitu,
faini na vibali mbalimbali vya biashara hizo za misitu na tunawataka
wafanyabiashara hao wafuate taratibu ili kuinusuru misitu yetu kwa kuvuna
kufuatatana na taratibu zilizowekwa,” alisema Dk Abel.
Alisema kuwa katika kuhakikisha
misitu inakuwa salama uvunaji wa mazao ya misitu umepangwa kwenye mashamba ya
miti ambayo si misitu ya hifadhi bali ni mistu ya wazi ambapo asilimia tano ya
mapato hurudi kwenye maeneo ya vijiji kwa ajili ya upandaji miti.
“Tunashirikiana na serikali za vijiji
kuhakikisha tano ya mapato zirudi kwa ajili ya upandaji miti kwa lengo la kuwa
na sehemu ya uvunaji wa miti kwani kama hakutakuwa na mashamba ya miti ni
dhahiri watu wafanyabiashara watakuwa wakivuna kwenye misitu ya hifadhi jambo
ambalo ni kinyume cha sheria,” alisema Dk Abel.
Alisema kuwa changamoto zinazoikabili
wakala ni pamoja na uvamizi wa watu kwenye hifadhi ya misitu, vitendea kazi,
kilimo na ufugaji kwenye hifadhi, uchomaji moto na uharibifu mwingine
unaofanywa na watu kwenye misitu hiyo ambayo iko kisheria na kuingia humo ni
kinyume cha sheria.
Aidha alisema wamekuwa wakifanya
doria alkini kutokana na misitu hiyo kuwa mikubwa ni vigumu kuweza kuwadhibiti
wahalifu wa misitu ambao wamekuwa wakivizia na kuingia na kufanya uharibifu na
Kanda ya Mashariki inaundwa na mikoa ya Pwani, Morogoro na Dar es Salaam.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment