Na John Gagarini, Kibaha
ZOEZI la ubomoaji kwa amri ya
Mahakama vibanda vya biashara vilivyopo eneo la mtaa wa Picha ya Ndege wilayani
Kibaha mkoani Pwani umeingia kwenye mgogoro baada ya familia ya iliyodaiwa kujenga
kwenye eneo ambalo si lao wamedai vimebomolewa kimakosa.
Ubomoaji huoa ambao ulifanywa Julai
15 na kampuni ya udalali ya Coast Auction Mart baada ya kesi hiyo ambayo imedumu
kwa kipindi cha miaka 35 familia hiyo ya iliyoongozwa na Eva Pwele ambaye
alikuwa mlalamikaji bada ya baba yake mzazi Pwele Showe ailiyefungua kesi hiyo
kufariki dunia kumlalamikia Tonga Fueta kudai eneo hilo ni mali yake ambapo
mahakama ilimpa ushindi.
Akizungumza na mwandishi wa habari mdai
Eva Pwele alisema kuwa maamuzi ya mahakama yalikuwa ni mlalamikiwa kupewa eneo lenye ukubwa wa mita 3
na nchi 7 kwa mita 3 na nchi 5 na si mita 352.92 ikiwa ni maamuzi yaliyotolewa
na mahakama ya Mwanzo Kibaha mwaka 1980.
Pwele alisema kuwa baada ya maamuzi
ya mahakama hayo miezi mitatu iliyopita alifuatwa na dalali na kutakiwa avunje
mwenyewe lakini yeye hakufanya hivyo na kusema kuwa yeye anachojua ni
kumkabidhi eneo lenye ukubwa wa mita 3 na nchi 7 tu na si hadi kwenye eneo
walilojenga mabanda hayo ya biashara.
“Cha kushangaza siku ya tukio nililiona
watu wakija wakiwa Dalali na kuanza kubomoa mabanda yetu ambayo yalijengwa hivi
karibuni baada ya kutokuwa na wasiwasi juu ya eneo hilo kwani mapitio ya hukumu
yalisema kuwa katika maamuzi ya mwanzo hayakuonyesha ukubwa wa eneo lakini
mapitio hayo ya mwaka 2005 ndiyo yaliyosema kuwa mlalamikiwa alipaswa
kurudishiwa sehemu iliyotajwa hapo juu,” alisema Pwele.
Alisema kuwa mbali ya maamuzi
kukiukwa pia alishangaa wahusika wa bomoa hiyo kutokuwa na barua yoyote ambayo
inawaruhusu kufanya ubomoaji huo ambao umewatia hasara kubwa kutokana na
mabanda hayo kuvunjwa kwa madai ya kujengwa kwenye eneo la mlalamikiwa.
Kwa upande wake Tonga Fueta alisema
kuwa kwanza anamshukuru Mungu kwani baada ya kuhangaika kwa miaka 35 hatimaye
haki yake imepatikana kwani tangu mwanzo wa kesi hiyo ilipofunguliwa na
mlalamikaji alikuwa akishinda kuanzia mahakama ya mwanzo hadi mahakama kuu kabla
ya kukatiwa rufaa na mlalamikaji baada ya hukumu ya kwanza iliyotolewa na
hakimu Chungulu mwaka 1981.
Fueta alisema kuwa alinunua eneo hilo
mwaka 1969 kwa kiasi cha shilingi 400 toka kwa mtu aliyetajwa kwa jina la
Ramadhan na mwaka huo huo alimpa sehemu ya eneo hilo Pwele Showe ambaye kwa
sasa ni marehemu lakini aliongeza na eneo lake.
“Mwaka 1971 nyumba zetu na mdai wangu
zilivunjwa kupisha ujenzi wa barabara ya Morogoro ndipo naye akamfuata Ramadhan
ili amuuzie eneo na kumuuzia kwa shilingi 500 na ndipo aliponimbia nivunje
banda langu kwakuwa yeye ameshanunua ndipo tatizo hilo lilipoanzia,” alisema
Fueta.
Kufuatia bomoabomoa hiyo familia ya
Pwele imesema kuwa itatafuta haki yao kwenye vyombo vya kisheria kwani ubomoaji
huo umekiuka amri ya mahakama kwa kuvunja sehemu ambayo haihusiki kwani wao
walikuwa wakijiandaa kumkabidhi eneo kama ilivyoagizwa na mahakama.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment