Na John Gagarini, Kibaha
MKUU mpya wa
wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Asumter Mshama ametoa siku 24 kwa watendaji wa
kata na maofisa tarafa kuhakikisha wanakamilisha zoezi la upatikanaji wa
madawati na atakayeshindwa kukamilisha zoezi hilo kwenye sehemu yake atakuwa
amejifukuzisha kazi mwenyewe.
Mshama ametoa
agizo hilo mjini Kibaha kwenye mkutano alioundaa na mkurugenzi wa Halmashauri
ya Mji wa Kibaha na watendaji hao na baadhi ya wakuu wa Idara za Elimu, Ardhi
na Mazingira na kusema kuwa watendaji hao wanapaswa kukamilisha zoezi hilo
ifikapo Julai 29 mwaka huu.
Amesema kuwa agizo
la Rais Dk John Magufuli ilikuwa ni Juni 30 mwaka huu hivyo hakuna sababu ya
watedaji hao kushindwa kutekeleza agizo hilo kwani muda uliotolewa ulishapita.
Aidha amesema
kuwa Baadhi ya watendaji wamefanikiwa kukamilisha zoezi nawapongeza lakini wengine
wameshindwa kukamilisha hivyo anatoa muda hadi Julai 29 wawe wamekamilisha na
atakayeshindwa atakuwa kajifukuzisha kazi mwenyewe kwa kushindwa kuwajibika.
Akielezea juu
ya uwezekano wa kukamilisha hilo amesema kuwa yeye kule alikotoka wilaya ya
Wangingombe mkoani Njombe alipambana na kufanikiwa kukamilisha zoezi hilo kwa
ufanisi mkubwa ambapo madawati yalipatikana na kuwa na ziada ya madawati 2,000
hivyo hata Kibaha hakuna sababu ya kushindwa kufanya hivyo kwani hakuna jambo
ambalo linashindikana.
Amesisitiza
kuwa Maagizo waliyopewa wao wakuu wa wilaya na Rais ni kuhakikisha hakuna
mwanafunzi anayekaa chini kwani haiwezekani nyumbani watoto wakae kwenye
makochi au sofa lakini wakifika shule wanakaa chini lazima watendaji hao
wahamasishe wananchi kuchangia miundombinu ya elimu.
Mkuu huyo wa
wilaya ya Kibaha amesema kuwa watendaji hao wanapaswa kuwahamasisha wananchi
kuchangia unpatikanaji wa madawati hakuna haja ya kusema kuwa eti watu wagumu
kuchangia.
Amesisitiza
kuwa Kama mtendaji ameshindwa kukamilisha zoei hilo ni kwamba ameshindwa kazi
kwani sheria zipo na wanapaswa kuzitumia ili kufanikisha zoezi hilo la
upatikaaji wa madawati.
Naye mtendaji
wa kata ya Kongowe Said Kayangu alikiri kuwa baadhi ya maeneo zoezi hilo
limeshindwa kufanikiwa kutokana na changamoto mbalimbali.
Kayangu
amesema kuwa watahakikisha muda uliosalia wanakamilisha zoezi hilo na kusema
kuwa watajipanga vizuri ili kufanikisha zoezi hilo ili kutekeleza agizo la Rais
Dk John Magufuli ili kila mtoto aweze kukaa kwenye dawati.
mwisho.
No comments:
Post a Comment