Monday, August 8, 2016

DC ASHANGAA WATU KUFANYA NGONO KWENYE MAKABURI

Na John Gagarini, Kibaha

MKUU wa wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Asumter Mshama amesikitrishwa na baadhi ya wakazi wa mtaa wa Mwanalugali kata ya Tumbi wanaoshiriki kwenye vitendo vya kishirikina kwa kufanya ngono kwenye makaburi ya Air Msae yaliyopo katika mtaa huo na kusema kuwa serikali haitatoa fedha kwa ajili ya kuweka uzio kwenye makaburi hayo ili kuzuia vitendo hivyo.

Makaburi hayo ambayo yalianzishwa na halmashauri ya Mji wa Kibaha baada ya basi la Air Msae kupata ajali kwenye barabara kuu ya Morogoro ambapo ili ua watu wengi na maiti nyingi zilizikwa hapo baada ya kukosa ndugu.

Akizungumza na wakazi wa mtaa huo alisema kuwa inasikitisha kuona watu wanafanya vitendo hivyo juu ya makaburi kwani hiyo ni laana kwa watu wanaojihusisha na vietendo hivyo na serikali haitapeleka fedha kwa ajili ya kuweka uzio badala yake fedha hizo ni afadhali zipelekwe kwenye shughuli za maendeleo.

Mshama alitoa kauli hiyo kufuatia uongozi wa kata hiyo ambapo mtendaji wa kata hiyo Msemakweli Karia akisoma risala alisema kuwa moja ya changamoto zilizopo kwenye kata ni baadhi ya watu kujihuisha na uovu huo nyakati za usiku juu ya makaburi hayo pamoja na vitendo vingine viouvu ikiwa ni pamoja na uvuitaji wa bangi hivyo kuomba kupewa fedha kwa ajili ya kuweka uzio kuzuia watu hao.

“Haiwezekani kuweka uzio kwani watu wanaofanya vitendo hivyo wanajitafutia laana kwani hawawezi kupata utajiri kwa kufanya vitendo hivyo kwenye makaburi hayo ya umma ambayo yanatumika kuzika watu kwenye mji wa Kibaha na hiyo ni laana kwani wanaofanya hivyo wanasema kuwa kwa kuwa ajali hiyo iliua watu wengi hivyo na wao watapata utajiri mkubwa jambo ambalo ni dhana ambayo haipaswi kupewa nafasi kwani uchawi unarudisha nyuma maendeleo na mji unaoendekeza imani hizo hauwezi kupiga hatua,” alisema Mshama.

Aidha alisema ili wananachi wa weze kujiletea maendeleo wanapaswa kufanya kazi kwa bidii na si kuwa na imani za kishirikina ili kupata maendeleo suala hilo halipaswi kupewa kipaumbele bali jitihada za kufanya kazi kwa bidii ndizo zitakazowafanya wawe na maisha mazuri.

Awali akisoma risala ya Kata ya Tumbi mtendaji wa kata hiyo Msemakweli Karia amesema kuwa changamoto nyingine zilizopo katika eneo hilo ni ubovu wa barabara.

Mwisho. 
 




  




No comments:

Post a Comment