Tuesday, August 30, 2016

BOMOABOMOA YALETA KIZAZAA MAILI MOJA KIBAHA


Na John Gagarini, Kibaha

WANANCHI wa eneo la Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani wamelia na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Pwani kuwa wawafikirie kwa kuwalipa fidia wakati wa zoezi la bomobomoa ambalo linatarajiwa kufanyika Novemba 23 mwaka huu.

Hataua hiyo imekuja baada ya TANROADS kutoa barua kwa watu waliojenga kwenye eneo la hifadhi ya barabara inayomilikiwa na wakala hiyo kwa wale waliojenga umbali wa mita 120 kwa kila upande wa barabara kuu ya Dar es Salaam Morogoro kuanzia Kiluvya hadi Tamco waanze kubomoa kabla ya zoezi hilo kwa kuwapa siku 90 kufanya hivyo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa Pwani Mrisho Swagala alisema kuwa mbali ya kuwtowlaipa fidia pia eneo linalopitiwa na zoezi hilo ni kubwa sana ikilinganishwa na maeneo mengine.

“Hatukati zoezi hilo kufanyika lakini wangeangalia namna ya kuwafidia wananchi kwani kuwabomolae bila ya kuwapa fidi itakuwa ni kitendo cha ukatili na kinakwenda kinyume cha haki za binaadamu kwani bomoa hiyo itawaacha watu wengi wakiwa hawana mahali pa kuishi na kwa wafanyabiashara hawatakuwa na sehemu ya kufanyia biashara,” alisema Swagala.

Alisema kuwa alisema kuwa sheria ya barabara iliyotungwa mwaka 1932 ambapo inadaiwa kuwa watu walilipwa fidia jambo ambalo kwa kipindi hicho fedha ilikuwa ni ndogo ukilinganisha hali halisi ya sasa hivyo kuna haja ya kuwafikiria.

Naye Ally Gonzi mwenyekiti wa ushirika wa wafanyabiashara wa soko la mkoa la Maili Moja alisema kuwa wao kama wafanyabiashara wansikitishwa na hatua hiyo kwani hadi sasa hawajui watakwenda kufanyia biashara wapi.

Gonzi alisema kuwa waliahidiwa kuwa watajengewa soko la kisasa lakini hadi sasa soko halijajengwa ambapo wao wako hapo kwa zaidi ya miaka 35 na Halmashauri ambao wao wako chini yao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mtaa wa Maili Moja Athuma Mkongota alisema kuwa wananchi wengi wamekwenda ofisini kwake kwenda kulalamika juu ya zoezi hilo ambalo litawakumba watu wengi ambao wako katikati ya mji huo.

Mkongota alisema kuwa ubomoaji huo umekuja baada ya kuisha kwa kesi iliyofunguliwa na wananchi kupinga hatua hiyo lakini walishindwa hata hivyo alisema kuwa hukumu ya kesi hiyo bado hajaipata.

Awali mkaguzi wa barabara wa mamlaka hiyo Livingston Urio alisema kuwa kwa sasa wanaendelea na zoezi la kutoa barua ambapo idadi kamili ya nyumba na vibanda vya biashara vitakavyobomolewa itajulikana.

Urio alisema kuwa ilikuwa ifanyike mwezi Agosti lakini waliongeza hadi Novemba lakini miaka ya nyuma tayari walishawawekea alama ya X mwaka 2004 lakini zoezi hilo halikufanyika lakini kwa sasa zoezi hilo linafanyika.

Alisema kuwa wananchi walipoenda mahakamani walishinda na kuonekana kuwa eneo hilo ni mali ya mamlaka hiyo na kuwa eneo hilo magari yanakwenda taratibu hivyo barabara kuharibika na baada ya bomoa hiyo eneo hilo litawekwa stendi kubwa na patapangwa vizuri ili mji uonekane vizuri.

“Kulingana na sheria ya barabara ya mwaka 1932 na kufanyiwa marekebisho 1958 kifunga na 52 na marekebisho ya sheria ya barabara na 13 ya mwaka 2007 sambamba na taratibu za sheria za usimamizi wa barabara kifungu na 30 (b) eneo la hifadhi ya barabara sehemu iliyotajwa hapo juu ni mita 120 sawa na futi 400 kwenda kila upande kutoka katikati ya barabara ni marufuku kufanya maendelezo yoyote katika eneo hilo,” alisema Urio.


Mwisho.  

No comments:

Post a Comment