Na John Gagarini, Kibaha
USHIRIKA wa Wafanyabiashara wa Soko la mkoa la
Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani wameiomba Halmashauri ya Mji wa Kibaha
kuwapatia eneo lingine la kufanyia biashara baada ya eneo wanalofanyia shughuli
zao ambalo liko chini ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa kuvunjwa
baada ya miezi mitatu kuanzia mwezi Agosti.
Akizungumza mara baada ya mkutano mkuu wa wanachama
uliofanyika mjini Kibaha mwenyekiti wa ushirika huo Ally Gonzi alisema kuwa
hadi sasa hawajui hatma yao mara zoezi hilo litakapofanyika.
Gonzi tunaiomba Halmashauri kutujengea soko au kama
hawataweza kujenga ndani ya muda huo wa miezi mitatu ni vema wakaiomba wakala
hao kutuongezea muda wa kuwa hapa hadi pale tutakapokuwa tumejengewa soko
jipya.
“Tunamwomba Rais John Magufuli kutuangalia kwani
hapa tuko zaidi ya miaka 30 na hadi sasa Halmashauri bado haijatujengea soko
ambalo waliahidi kutujengea kutokana na eneo hilo kutokuwa la halmashauri,”
alisema Gonzi.
Alisema kuwa kwa kipindi kirefu Halmashauri hiyo
imekuwa ikiahidi kuwajengea soko la kisasa kwenye kitovu cha mji lakini hadi
wanapewa barua za kutakiwa kuondoka kwenye eneo hilo na Tanroads hadi sasa
hawajajengewa soko.
“Tunachoona kwa sasa kwa kuwa soko bado
halijajengwa ni vema wakatuongezea muda hata wa miaka miwili kwani Halmashauri
ilisema itakuwa imejenga soko ndani ya miezi 18 hivyo kwa kipindi hicho ni bora
tungebaki hapa kwanza lakini vinginevyo hatujui tutakwenda wapi,” alisema
Gonzi.
Aidha alisema kuwa mbali ya wao kutokuwa na mahali
pa kufanyia biashara pia Halmashauri itakosa mapato kwnai soko hilo ni moja ya
vyanzo vikuu vya mapato pia wao walikuwa wakitegemea hapo kwa ajili ya
kujipoatia kipato chao na familia zao.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment