Na John
Gagarini, Kibaha
MKAZI wa Mtaa
wa Karabaka-Misugusugu kata ya Misugusugu wilayani Kibaha mkoani Pwani Zawadi
Halfan (25) ameuwawa kwa kupigwa risasi na majambazi wakati akisubiri
kuunganishiwa kifurushi cha muda wa maongezi kwenye simu yake.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini
kwake mjini Kibaha kamanda wa Polisi mkoani humo Bonaventura Mushongi alisema
kuwa marehemu alikuwa amekaa kwenye benchi kwenye kibanda cha huduma za fedha
kwa mtandao mali ya Gaitano Joseph (30).
Mushongi alisema
kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 9 majira ya saa 2:30 usiku kwenye mtaa huo
ambapo marehemu alikuwa akisubiri huduma hiyo kabla ya mauti kumkuta.
“Marehemu
hakuwa mlengwa bali walikuwa wamemlenga Yohana Koseja (24) ambaye ni mfanyakazi
wa Mchungaji Raphael John ambaye ni mmiliki wa duka la M-Pesa ambapo majambazi
hao baada ya kufika walimwamuru Yohana asimame baada ya kufunga duka hilo lakini
alikimbia na kukaidi agizo la majambazi hayo ambayo yalikuwa matatu,” alisema
Mushongi.
“Kutokana na
Yohana kukimbia majambazi hayo yalianza kufyatua risasi ndipo moja ilimpata
marehemu sehemu ya mgongoni upande wa mgongoni na kufariki papo hapo ambapo walikuwa wakifyatua risasi hizo kwa Yohana
wakimhisi kuwa alikimbia na fedha bada ya kufunga duka,” alisema Mushongi.
Alisema baada
ya majambazi hao kutoka kwenye tukio la kwanza walivamia duka lingine la M-Pesa
lililopo pamoja na duka la madawa ya binadamu linalomilikiwa na Renovatus
Katabalo (29) mfanyabiashara na mkazi wa Kongowe ambapo duka lake lipo eneo
hilohilo la Karabaka na kupora kiasi cha shilingi 300,000.
“Chanzo cha
tukio hilo ni kuwania mali na msako unaendelea mkoa mzima ili kuwakamata
watuhumiwa ili wafikishwe kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili
za mauaji ambapo eneo la tukio maganda ya risasi aina ya SMG/SAR,” alisema
Mushongi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment