Na John
Gagarini, Kibaha
MWILI wa mtu
mmoja ambaye jina lake ambalo halikuweza kufahamika mara moja mwenye umri kati
ya miaka (33) na (38) umeokotwa huku ukiwa umepigwa risasi chini ya kidevu na
kutokea utosini.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi mwenyekiti wa mtaa wa Lulanzi kata ya Picha ya
Ndege wilayani Kibaha mkoani Pwani Thobias Shilole alisema kuwa marehemu
aliuwawa na watu wasiofahamika.
Shilole
alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 7 majira ya saa 3 asubuhi kwenye
korongo lililopo kwenye shamba linalomilikiwa na Saeed Yeslam Saeed ambapo
watoto waliokuwa wakichunga mbuzi ndiyo waliogundua mwili huo na kutoa taarifa
kwa wazazi wao ambao walitoa taarifa kwa balozi wao na ndiye aliyemjulisha juu
ya tukio hilo.
“Mwili huo
ulikuwa na jeraha la risasi chini ya kidevu na kufumua kichwa na mtu huyo
anahusishwa na tukio lililofanyika siku kama tatu zilizopita kwa kumpiga risasi
kwenye makalio na kumpora fedha mtu aliyetambulika kwa jina la Beno Nyoni (36)
mkazi wa Picha ya Ndege ambaye alikuwa akijenga nyumba yake eneo la mtaa wa
Lulanzi,” alisema Shilole.
Shilole
alisema kuwa watu hao wanaosadikiwa kuwa ni majambazi baada ya kumshambulia
walikimbia na kusababisha majeruhi huyo kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa
Pwani Tumbi lakini ilishindikana na kupelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili
kwa matibabu zaidi ambako hadi sasa anatibiwa baada ya kutolewa risasi
iliyokuwa mwilini.
“Tunaiomba
serikali kumlazimisha mmiliki kulifanyia usafi kwani pori kubwa ambalo limekuwa
likitumiwa na wahalifu kwa ajili ya kujificha na kufanya wizi kisha kujificha
huko kwani hata mwaka jana tulikuta mtu akiwa amejinyonga hivyo sehemu hiyo
usalama wake ni mdogo hasa ikizingatiwa eneo hilo liko umbali wa kilometa 2
toka barabara kuu ya Morogoro,” alisema Shilole.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Pwani Bonaventura Mushongi
alisema kuwa baada ya kuangaliwa marehemu alikutwa na jeraha kidevuni na
kichwani huku mwili wake ukianza kuharibika.
Msuhongi
alisema kuwa pembeni yake kulikutwa kofia ya kuficha sura ganda la risasi aina
ya SMG/SAR na nyaraka mbalimbali ambazo ni ramani za nyumba mbili, stakabadhi
za kibali cha ujenzi, hati ya hukumu ya shauri la mgogoro wa ardhi.
Alisema vitu
vingine vilivyokutwa ni kadi za biashara, kadi za benki za posta, NBC, Posta na
CRDB, kadi ya kupigia kura na leseni ya udereva vyote vikiwa na majina ya Nyoni
ambaye ni mfanyabiashara wa Picha ya Ndege.
“Vitu hivyo
ni vya Majeruhi huyo aliyofanyiwa tukio hilo la unyanganyi wa kutumia silaha na
kupora mali na walifika kwenye kwenye hilo kwa lengo la kugawana mali hizo
lakini inaonyesha walihitilafiana ndipo walipompiga marehemu risasi na kumuua
kisha walimpekekua kwani mifuko ya suruale yake ilkuwa iko nje na hakukutwa na
kitambulisho chochote na mwili umehifadhiwa hospitali ya Tumbi,” alisema
Mushongi.
Naye diwani
wa kata hiyo Robert Machumbe alisema kuwa shamba hilo lilikofanyika tukio hilo
lina pori kubwa sana hivyo ni vema Halmashauri likafanya utaratibu kama mmiliki
kashindwa litolewe kwa mtaa ili kuweza kujengwa huduma za jamii kama shule,
zahanati na huduma nyingine kwani kwa sasa limekuwa hatari kwa wananchi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment