Thursday, August 11, 2016

MZEE WA BARAZA LA MAHAKAMA APANDISHWA KIZIMBANI KWA RUSHWA

Na John Gagarini, Kibaha

TAASISI ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Pwani imemfikisha mahakamani Mzee wa Baraza la Mahakama ya Mwanzo Maili Moja Kibaha Francis Ndawanje kwa tuhuma za kuomba na kupokea Rushwa ya shilingi 100,000 ili kumsaidia mtuhumiwa kushinda kesi yake.

Mtuhumiwa alisomewa mashitaka kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha  mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Pwani  Herieth Mwailolo ambapo kwa upande wa chini ya mwendesha mashitaka kutoka TAKUKURU Mkoa Pwani Sabina Weston.

Akisoma maelezo juu shitaka hilo Weston aliiambia Mahakama kuwa mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kutenda makosa hayo mawili kati ya tarehe 3 na 4  Agosti mwaka huu ambapo.

Mahakama iliambiwa kuwa mtuhimwa aliomba rushwa Agosti 3 kwa Omary Hoza ili amsaidie mkewe Mariamu Hoza ambaye ana kesi namba 324 kwenye mahakama hiyo hivyo kumuomba rushwa ya shilingi 100,000.

Ikaelezwa kuwa mtuhumiwa alipokea rushwa siku iliyofuata Agosti 4 alipokea fedha hizo eneo la jirani na Kituo cha Polisi Tumbi jirani na barabara kuu ya Morogoro Maili Moja wilayani Kibaha.

Baada ya kusomwa mashtaka hayo mtuhumiwa alikana tuhuma hizo ambapo upande wa Taasisi hiyo ulisema kuwa hauna pingamizi na dhamana kwa mtuhumiwa ili mradi akamilishe masharti ya dhamana na yuko nje kwa dhamana ya shilingi 500,000 kwa wadhamini wawili kila mmoja.

Hakimu alisema kuwa wadhamini wanapaswa kuhakikisha mtuhumiwa anafika siku ya kesi hiyo ambayo imepangwa kufanyika Agosti 15 mwaka huu.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment