Na John
Gagarini, Kibaha
TAASISI
ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Pwani imemfikisha mahakamani Mzee
wa Baraza la Mahakama ya Mwanzo Maili Moja Kibaha Francis Ndawanje kwa tuhuma
za kuomba na kupokea Rushwa ya shilingi 100,000 ili kumsaidia mtuhumiwa
kushinda kesi yake.
Mtuhumiwa
alisomewa mashitaka kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha mbele ya
hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Pwani Herieth Mwailolo ambapo kwa
upande wa chini ya mwendesha mashitaka kutoka TAKUKURU Mkoa Pwani Sabina Weston.
Akisoma maelezo juu shitaka hilo Weston aliiambia Mahakama kuwa mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kutenda makosa hayo mawili kati ya tarehe 3 na 4 Agosti mwaka huu ambapo.
Mahakama iliambiwa kuwa mtuhimwa aliomba rushwa Agosti 3 kwa Omary Hoza ili amsaidie mkewe Mariamu Hoza ambaye ana kesi namba 324 kwenye mahakama hiyo hivyo kumuomba rushwa ya shilingi 100,000.
Akisoma maelezo juu shitaka hilo Weston aliiambia Mahakama kuwa mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kutenda makosa hayo mawili kati ya tarehe 3 na 4 Agosti mwaka huu ambapo.
Mahakama iliambiwa kuwa mtuhimwa aliomba rushwa Agosti 3 kwa Omary Hoza ili amsaidie mkewe Mariamu Hoza ambaye ana kesi namba 324 kwenye mahakama hiyo hivyo kumuomba rushwa ya shilingi 100,000.
Ikaelezwa
kuwa mtuhumiwa alipokea rushwa siku iliyofuata Agosti 4 alipokea fedha hizo
eneo la jirani na Kituo cha Polisi Tumbi jirani na barabara kuu ya Morogoro
Maili Moja wilayani Kibaha.
Baada ya
kusomwa mashtaka hayo mtuhumiwa alikana tuhuma hizo ambapo upande wa Taasisi
hiyo ulisema kuwa hauna pingamizi na dhamana kwa mtuhumiwa ili mradi akamilishe
masharti ya dhamana na yuko nje kwa dhamana ya shilingi 500,000 kwa wadhamini
wawili kila mmoja.
Hakimu alisema
kuwa wadhamini wanapaswa kuhakikisha mtuhumiwa anafika siku ya kesi hiyo ambayo
imepangwa kufanyika Agosti 15 mwaka huu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment