Na John
Gagarini, Kibaha
BINTI
aliyetambulika kwa jina la Judith Paulo anayekadiriwa kuwa na umri katia ya
miaka (18) na (22) anatuhumiwa kuzaa mtoto wa jinsia ya kike kisha kumtupa
mwanae jirani na jalala.
Akizungumza na
mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu mwenyekiti wa Kitongoji cha Pera kata
ya Pera Chalinze Mjini Hussein Mramba alisema kuwa tukio hilo lilitokea
Septemba 7 majira ya saa 12 asubuhi eneo la Kwa Mwarabu.
Mramba alisema
kuwa kichanga hicho chenye uzito wa kilogramu 3.2 kiliokotwa baada ya watoto
waliokuwa wakiokota vitu mbalimbali jirani na jalala huku kikiwa kimewekwa
kwenye mfuko wa Rambo.
“Watoto hao
ndiyo waliogundua na ndipo walipotoa taarifa kwa watu wazima na kwenda
kumchukua ambapo walimkuta mtoto huyo akiwa na afya njema huku akiwa
hajavalishwa nguo yoyote mwilini mwake na jambo la kumshukuru Mungu kuwa mtoto
huyo hakupata madhara yoyote,” alisema Mramba.
Alisema kuwa
baada ya hapo ilibidi wasamaria wema wampeleke Hospitali ili kuangalia namna ya
kumsaidia mtoto huyo ambaye kwa sasa yuko kwa mama mmoja ambaye amejitolea
kukaa naye wakati taratibu nyingine zinafanyika ili apelekwe sehemu stahiki.
“Kwa maelezo
tuliyopata baada ya kwenda Kituo cha Afya cha Chalinze ili kujua kama
alijifungua hapo ilibainika kuwa binti huyo alijifungua kituoni hapo juzi
majira ya saa 4 baada ya kufika hapo majira ya saa 3 usiku akiwa na uchungu wa
kujifungua huku akiwa hajaongozana na mtu yoyote,” alisema Mramba.
Mramba ambaye
pia ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mdogo wa Chalinze alisema kuwa baada ya
kujifungua alikaa kama masaa mawili kisha kuomba kuondoka baada ya kujifungua
salama na alimwomba muuguzi aondoke kwani alikuwa hajafunga mlango wa nyumba
anayoishi hivyo ana hofu ya kuibiwa vitu vyake.
“Kutokana na
utetezi wake huo ilibidi baadhi ya wazazi wamsaidia fedha kwa ajili ya kulipia
teksi baada ya kumuonea huruma ambapo yeye alifika hapo kituoni kwa kutumia
bodaboda,” alisema Mramba.
Aidha alisema
kuwa binti huyo alionekana kuwa na wasiwasi alipofika kituoni hapo lakini hata
hivyo baadhi ya wazazi waliokuwa hapo walijaribu kumweka sawa ili aone jambo la
uzazi ni la kawaida.
Alisema kuwa
taarifa hizo wamezitoa sehemu mbalimbali ikiw ani pamoja na polisi kwa ajili ya
kusaidia kupatikana kwa binti huyo ambapo mita kama 100 aliposhushwa na teksi
wamejaribu kuulizia lakini inavyoonekana kuwa hakuwa anakaa maeneo hayo kwani
jina hilo hakuna mtu anayelifahamu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment