Friday, September 23, 2016

WAWILI WAFA AJALINI MMOJA ACHOMWA MOTO

Na John Gagarini, Kibaha

WATU wawili wamefariki dunia na wengine 11 kujeruhiwa mkoani Pwani kufuatia ajali iliyohusisha mabasi madogo mawili ya abiria kugongana uso kwa uso huko Kiparanganda wilayani Mkuranga.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi mkoani humo Bonaventura Mushongi alisema kuwa watu hao walifariki papo hapo.

Mushongi alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Septemba 21 mwaka huu majira ya saa 10:30 jioni T363 DCV likiendeshwa na Zidadu Mohamed (25) mkazi wa Dar es Salaam akielekea Kimazinchana liligongana na T363DHD yote aina ya Toyota Hiace likiendeshwa na Miraji Mlonga (22) akielekea Dar es Salaam.

Aliwataja waliokufa kuwa ni Zuhura Haji (21) na Neema Julius (25) wote wakazi wa Kimazinchana wilaya ya Mkuranga ambapo miili yao imehifadhiwa kwenye Hopsitali ya Wilaya ya Mkuranga kusubiri ndugu kwa ajili ya mazishi.

Aidha aliwataja watu waliojeruhiwa kuwa ni Majeruhi ni Mariamu Aloyce (46) wa Kimazinchana Mariamu Sultan (60) mkzai wa Chanika, Yusufu Maziku (33) mkazi wa Kimazinchana,Kulwa Abdala (30) makzi wa Mbagala,Ibrahim Hamis (3) mkazi wa Mbagala na Fatma Abdul (25) mkazi wa Chanika.

Wengine ni Salum Mohamed (54) mkazi wa Mwalusembe, Litus Mwarami (26) mkazi wa Kimazinchana Kidawa Abdala (30) mkazi wa Mbagala, Issa Hemed (2) mkazi wa Kimazinchana na Greyson Ernest (23) mkazi wa Kimazinchana.

“Tuna washikilia madereva wote waili kutokana na kusababisha ajali hiyo na watafikishwa mahakamani mara upelelezi wa kesi hiyo utakapokamilika ili kujibu tuhuma hizo zinazowakabili,” alisema Mushongi.

Kwenye tukio lingine mkazi wa Kwa Mathias Hamis Tenende (38) aliuwawa kwa kupigwa kisha kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali kwa madai ya kutaka kuiba pikipiki eneo la Umwelani.

Mwisho.
 








No comments:

Post a Comment