Monday, September 12, 2016

WAPONGEZA IDD EL HAJI KUFANYIKA KWA PAMOJA


Na John Gagarini, Kibaha

KUFUATIA sherehe ya Idd el Haji ambayo inahusisha na uchinjaji kufanyika jana ambapo waumini wa dini ya Kiislamu walisherehekea kwa pamoja tofauti na miaka mingine ambapo kila dhehebu lilikuwa likifanya siku tofauti safari hii wamefurahi kufanya kwa pamoja.

Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha baadhi ya waumini wa Kiislamu wamesema kuwa utaratibu wa kusherehekea kwa pamoja ni mzuri kwani unaonyesha umoja na ni vema ukaendelea hata kwa siku zijazo.

Mrisho Halfan “Swagala”  alisema kuwa hakuna sababu wao kama waumini wa imani moja kufanya sherehe kwa wakati tofauti na kufanya kama ni imani tofauti.

“Tunaomba viongozi wa taasisi hizi za dini yetu wakae kwa pamoja na kufanya vitu kwa pamoja kwani kama mwaka huu sikukuu imependeza kwani wote tumejumuika na hali hii imeondoa tofauti na kutufanya kitu kimoja,” alisema Swagala.

Alisema kuwa kuna haja ya kuunganisha umoja wa waislamu kama hivi kwa kiufanya sherehe hiyo ambayo ni kubwa kwa Waislamu kote duniani kukumbuka yale yaliyofanywa na mtume ikiwa ni kufanya mambo yanayompendeza Mungu.

Kwa upande wake Abubakari Lipambila kutoka Masjidi Hazarajii Maili Moja Kibaha alisema kuwa sikukuu hiyo ni kwa ajili ya kurejesha furaha kwa watu wote.

Lipambila alisema kuwa waumini wa dini ya kiislamu wanapaswa kujihadhari na shetani katika kipindi hichi cha sherehe kwani naye yuko kazini kwa kuwapotosha watu ili waende kinyume na imani kwa kujiingiza kwenye vitendo viovu.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment