Thursday, February 25, 2016

ZIMAMOTO PWANI WAZUIA UUZAJI PETROLI MAJUMBANI

Na John Gagarini, Kibaha
KIKOSI cha zimamoto na uokoaji mkoni pwani kimewata wananchikuacha kuuza mafuta aina ya Petroli majumbani mwao ili kuepukana na milipuko ya moto inayotokana na mafuta hayo ambayo ni hatari.
Hayo yalisema mjini Kibaha na kamanda wa kikosi hicho Goodluck Zelote alipoongea na mwandishi wa habari hizi na kusema kuwa uuzaji huo wa kiholela ni hatari kwani umesababisha madhara makubwa ya uharibifu wa mali na watu kupoteza maisha.
Zelote alisema kuwa uuzaji huu si salama kwani kuhifadhi mafuta ya petrol ndani ni hatari kutokana na mafuta hayo kuwa ni rahisi kuwaka hivyo kuyauza kwenye nyumba za kuishi ni hatari sana kwa maisha ya watu.
“Utaratibu wa kuuza mafuta unafahamika lakini kwa sasa kumeibuka watu kuweka mafuta kwenye madumu pamoja na kwenye chupa za maji kisha kuyauza kwa madereva pikipiki na mafuta haya huhifadhiwa ndani jambo ambalo ni la hatari sana kwani watu wamepoteza maisha,” alisema Zelote.
Alisema kuwa mafuta hayo yanatakiwa yawekwe kwenye matenki na kuchimbiwa chini ndiyo utaratibu unaotakiwa lakini baadhi wanakiuka taratibu hizo kwa kuyahifadhi kwenye madumu ya maji.
“Tayari tumeshatoa elimu kuhusiana na kuepuka vitu ambavyo vinachangia moto kuwa majumbani ikiwa ni pamoja na kuepukana na utaratibu huo pamoja na kutohifhadhi pikipiki ndani ya nyumba kwani ni hatari bali wamiliki wangeangalia namna ya kuzihifadhi pikipiki zao,” alisema Zelote.
Aidha alisema kuwa bado wanendelea na utaratibu wa kutoa elimu kwenye maeneo mbalimbali ambayo yana mikusanyiko ya watu kama vile mashuleni, vituo vya mabasi, mikutano na kwenye masoko kwa lengo la kuwapatia elimu juu ya kujikinga na majanga.
“Vifaa vya kuzimia moto vinapaswa kuwa kwenye sehemu mbalimbali za huduma pamoja na majumbani ambapo sheria iko wazi na kuna adhabu kutegemeana na kosa na ukubwa wa huduma na kuna faini ambayo inaanzia 100,000 au kifungo cha miezi sita,” alisema Zelote.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment