Na John Gagarini, Kibaha
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha wakati
wa zoezi la kusafisha eneo la kujenga shule ya sekondari ya mtaa wa Mbwate raia
hao walisema kuwa utaratibu huo unatoa fursa kwa watoto wengi waliofikia umri
wa kwenda shule kupata nafasi hiyo.
Laura Pommerenke alisema kuwa utoaji wa elimu kwa wanafunzi
wa shule za msingi na sekondari utalifanya Taifa la Tanzania kuwa na watoto
wengi watakaokuwa wemekwenda shule tofauti na ilivyokuwa zamani.
“Utaratibu wa elimu bure ni mzuri kwani hata kule kwetu
ambako watu wanauwezo wanafunzi wanapata elimu bure hali ambayo inawafanya
watoto kupata elimu inayostahili kwa wakati na kuondokana na watu kutokuwa na
elimu,” alisema Pommerenke.
Alisema kuwa msingi wa elimu ya awali ukiwekwa utasaidia nchi
kukabiliana na tatizo la watoto wa Tanzania kukosa elimu hali ambayo itazidi
kuongeza umaskini lakini wakipata elimu watakuwa na uwezo wa kujitegemea.
Naye Marie Vogel alisema kuwa alisikia kuwa elimu ya Msingi
na Sekondari ili kuwa na gharama jambo ambalo liliwafanya watoto wengi
washindwe kwenda shule hivyo kuwafanya watoto wengi kuwa mitaani au kuanza
maisha kabla ya wakati wao.
Vogel alisema kuwa serikali ya Tanzania inapongezwa kutokana
na kuchukua maamuzi hayo ya kutoa elimu bure kwa wanafunzi wa elimu ya msingi
na sekondari kwani mpango huo utakuwa na manufaa makubwa kwa nchi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa huo Abdala Mtandio alisema
kuwa mpango wao wa kujenga shule ya sekondari kwenye mtaa wao umezingatia
tatizo la watoto wengi kusoma mbali na kujikuta wakitumia mwingi njiani.
Mtandio alisema kuwa malengo yao ni kujenga madarasa manne ya
kuanzia ili wanafunzi waanze kusoma hapo na wanahitaji kiasi cha shilingi
milioni 50 za kuanzia pia wamewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment