Na John Gagarini, Kibaha
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mkuu wa wilaya ya Kibaha
Halima Kihemba wakati wa kuzindua Jukwaa la Uwajibikaji kwa Asasi ya Kitaifa ya
Ushirikiano wa Maendeleo ya Vijana (YPC)
ya mkoa wa Pwani na kusema kuwa mashamba hayo pia yatatumika kwa ajili ya
makazi.
Kihemba alisema kuwa mashamba hayo yalikuwa kero kwa wananchi
kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu na wamiliki licha ya kutakiwa
kuyaendeleza kisheria lakini wameshindwa na kuyafanya mapori makubwa.
“Baadhi ya mashamba yamerudishwa serikalini kama
tulivyoagizwa na tutahakikisha tunayapima kwa ajili ya viwanda ili kuweza
kuimarisha uchumi wa wakazi wa wilaya ya Kibaha pia sehemu yatapimwa kwa ajili
ya makazi,” alisema Kihemba.
Alisema kuwa maeneo hayo yaliyorejeshwa hayapaswi kuvamiwa
kwani kuna taarifa baadhi ya watu wameanza kuyavamia mashamba hayo jambo ambalo
ni kinyume cha sheria kwani yatatumiwa kwa mipango itakayokuwa imepangwa na si
kwa watu kuyavamia.
“Ni marufuku watu kuyavamia maeneo hayo ambayo yalirejeshwa
serikalini na kwa wale watakaojenga nyumba zao zitabomolewa wanachotakiwa ni
kusubiri utaratibu utakaowekwa na serikali na si kujichukulia kinyume cha
sheria,” alisema Kihemba.
Aidha alisema kuwa kwa kuwa serikali ya awamu ya tano
imepania kuinua uchumi wa Watanzania kupitia viwanda ili wawe na uchumi wa kati
ni vema na wao wakaunga mkono mpango huo kwa kuanzisha viwanda kwa kushirikiana
na sekta binafsi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment