Na John Gagarini, Kibaha
Simbachawene aliyasema hayo alipotembelea Shirika hilo hivi
karibuni na kusema kuwa ndiyo sababu chuo hicho hakikuingizwa kwenye Taasisi ya
elimu ya juu kwani malengo yake ni kusomesha watu ambao ni wa ngazi ya kati.
Alisema kuwa kwa sasa kumekuwa na hali ya kila chuo kutaka
kuwa chuo kikuu hali ambayo itasababisha kusiwe na wataalamu wa ngazi ya kati
ambao wameonekana kuwa ndiyo wawajibikaji wakubwa.
“Kama kila chuo au taasisi itakuwa na malengo ya kuwa chuo
kikuu kuna hatari ya kuwapoteza wasomi wa ngazi ya kati kwani endapo kila mtu
atakuwa amesoma chuo kikuu hakutakuwa na watu wa kufanyakazi kwani kila mtu
atatakuwa mtawala,” alisema Simbachawene.
Alisema kuwa chuo hicho kilianzishwa kwa malengo ya kuwapatia
elimu watu wa vijijini lakini kikishafanywa chuo kikuu wananchi wenye elimu ya
kati hawatapata nafasi ya kusoma hivyo malengo ya kuisaidia jamii hayataweza
kufikiwa.
“Tunashindwa kupata wagunduzi kwani wanakuwa ni watu wenye
elimu ya kawaida sana kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea hawa ni watu waliosoma
elimu ya kawaida na wengine wanatoka vijijini hivyo na hapa ni sehemu ya
kuanzia lakini tukikibadilisha na kuwa chuo kikuu ni sawa na kuvunja daraja ambalo
watu wamekuwa wakitumia kuvukia kwenda mbele,” alisema Simbachawene.
Aidha alisema kuwa kuna tatizo la wataalamu wa kati kutokana
na watu wengi kuiacha elimu ya kati na kutaka kupata elimu ya juu hivyo kumekuw
ana pengo hapo katikakati pia wazingatie malengo ya kuanzishwa chuo hicho
ambacho zamani kilijukana kama chuo cha maendeleo ya waganga vijijini.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment