Na John
Gagarini, Kibaha
IDARA ya
Uhamiaji Mkoani Pwani imewataka wananchi
kutokubali kukaa na wageni ambao si raia Watanzania kwani ni kinyume cha
taratibu na endapo watabainika watachukulia hatua za kisheria kwa kuwatunza
wageni.
Hayo
yalisemwa na Naibu Kamishna wa Idara hiyo Grace Hokororo alipozungumza na
mwandishi wa habari hizi ofisni kwake mjini Kibaha na kusema kuwa kuna watu
wanaishi na wageni jambo ambalo ni kosa kisheria.
Hokororo
alisema kuwa kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiishi na wageni majumbani mwao
wengine wakiwa wamewapangisha, wamewaajiri au kuwapangisha kwenye nyumba zao
kama Raia wa Tanzania bila ya kufuata taratibu.
“Mgeni
yoyote anapoingia nchini anapaswa kufuata taratibu na lazima serikali au idara
hivyo watu wanaokaa nao au kufanya nao shughuli yoyote bila ya kufuata
taratuibu za nchi ni kosa na endapo wanagundua kuwa siyo raia wanapaswa kutoa
taarifa ili hatua zichukuliwe kwa mhamiaji haramu,” alisema Hokororo.
Alisema kuwa
changamoto inayowakabili ni uchache wa watumishi hali ambayo inawafanya
washindwe kuwadhibiti wahamiaji haramu hao ambao wamekuwa wakileta athari
nyingi kwa raia endapo atakaa kinyemela
bila ya kufuata taratibu.
“Kuna athari
mbalimbali zinazotokana na Raia wa nje kuishi bila ya kibali ikiwa ni pamoja na
kunyakua rasilimali kama vile mashamba na vitu vingine lakini akiishi kwa
kufuata taratibu kuna namna ya kupewa rasilimali bila ya kumwathiri mwenyeji,”
alisema Hokororo.
Aidha
alisema kuwa changamoto nyingine ni mkoa kutawanyika na njia za kuingilia ni
nyingi kwa kupitia kwenye Bahari ambako hakuna vyombo vya kufanya doria kwenye
bandari ambazo nyingine ni bubu ambazo zinatumika kama milango ya kuingilia.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment