NA
John Gagarini, Kibaha
WAKAZI
wa Mtaa wa Mbwate kata ya Msangani wilayani Kibaha mkoani Pwani wanahitaji
kiasi cha Shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa manne ya shule ya
sekondari kwenye mtaa huo.
Mtaa
huo una wanafunzi zaidi ya 500 wanaotoka kwenye mtaa huo kwenda kusoma kwenye
shule ya sekondari ya Nyumbu ambayo iko umbali wa kilometa zaidi ya 10 hali
ambayo inawapa wakati mgumu wanafunzi hao kutokana na umbali.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwenye eneo ambalo wanalifanyia usafi kwa ajili ya
ujenzi wa shule hiyo mwenyekiti wa mtaa huo Abdala Mtandio alisema kuwa
walikuwa wamelenga kuanza ujenzi mwakani lakini kutokana na wanafunzi wengi
wanaotoka kwenye mtaa huo kusoma mbali wameona afadhali waanze na madarasa
machache ili kuwasaidia watoto wao ili wasome karibu na wanakoishi.
“Tunaomba
wadau watusaidie kupata fedha hizo ili tuanze ujenzi kwani kwa sasa shule ya
sekondari ya Kata ya Nyumbu imeelemewa
na wanafunzi hivyo tunaiomba Halmashauri iwapunguzie wanafunzi hao kwenye shule
tutakayojenga kwani kwenye mtaa wetu kuna eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa
shule ya sekondari wakati kule hawana eneo la kuongeza madarasa,” alisema
Mtandio.
Mtandio
alisema kuwa kutokana na serikali kutaka shule kuongeza madarasa kwa zile
ambazo zina wanafunzi wengi ni vema Hlamashauri ikaongeza nguvu kwenye ujenzi
wa shule ambayo wanataka kujenga ili kupunguza mlundikano wa wanafunzi kwenye
shule hiyo ya Nyumbu.
“Tunaomba
wadau watusaidie kwani kwa sasa eneo limepatikana kwa ajili ya ujenzi ambalo
lina ukubwa wa hekari 10 tumeanza kwa kujitolea kufyeka vichaka na sasa
tunajitolea kungoa visiki ambapo pia tunaomba Halmashauri itusaidie greda kwa
ajili ya kungoa visiki tuliomba muda mrefu ambapo tathmini ilifanyika na
kuonekana kuwa zinahitajika kiasi cha shilingi milioni nane kwa ajili ya greda,”
alisema Mtandio.
Kwa
upande wake mmoja wa wakazi wa mtaa huo Steven Mwita alisema kuwa malengo ya
mtaa wetu ni kuanza ujenzi kuanzia mwezi wanne hivyo wanawaomba serikali na
wadau wengine wa maendeleo wawasaidie kwa kuwachangia kwa hali na mali ili
wafikie lengo la kujenga shule ya sekondari.
Mwita
alisema kuwa matarajio yao ni kufanya ujenzi wa kisasa wa ghorofa ili baadaye
wawe na elimu ya juu yaani kidato cha tano na cha sita kwa lengo la kuinua
sekta ya elimu kwenye mtaa pamoja na wilaya nzima ya Kibaha
Mwisho.
No comments:
Post a Comment