Sunday, February 21, 2016

MBUNGE AKABIDHI VITABU VYA SAYANSI

MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kushoto akimkabidhi kitabu ofisa elimu wa mji wa Halmashauri ya Chalinze Zainab Makwinya kulia na katikati ni mwanfunzi wa shule ya sekondari ya Mdaula Budi Tanganyika  

Na John Gagarini, Chalinze

KATIKA kuhamasisha wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi shirika lisilo la Kiserikali la Kulea Childcare Villages la Chalinze  kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete wamekabidhi vitabu 3,438 vyenye thamani ya shilingi milioni 70.
Vitabu hivyo vya Sayansi ni kwa ajili ya wanafunzi wote wa shule za Sekondari na vichache kwa wanafunzi wa Msingi kwa wanafunzi wa Jimbo la Chalinze ili kuwahamsisha kujifunza mambo mbali mbalimbali ya Sayansi.
Akikabidhi vitabu hivyo kwa mwalimu mkuu wa shuke ya Sekondari ya Mdaula Melkisedek Komba, Mbunge wa Jimbo hilo alisema kuwa lengo la kutolewa vitabu hivyo ni kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo hayo ili kupata wataalamu wengi wa Sayansi .
Ridhiwani alisema kuwa masomo ya Sayansi ndiyo yanaotoa wataalamu mbalimbali hivyo wadau wa elimu wanapaswa kutoa hamasa ya kwa wanafunzi kujifunza Sayansi ili waongeze idadi ya wanaosoma kwa lengo la kuwa na wanasayansi wengi.
“Sisi tukiwa ni wadau wa maendeleo tutaendelea kusaidiana na wadau wengine ili kuhakikisha kuwa tunawahamsisha wanafunzi kuyapenda masomo haya ambayo baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakiyaogopa kwa madai kuwa ni magumu hivyo ni vema tukawawekea mazingira ya kuona kuwa ni sawa na masomo mengine,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa serikali imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali kama ilivyo kwa shirika la Kulea Childcare ambalo limepata vitabu hivyo toka kwa marafiki zao wa nchini Marekani kwa ajili ya kusaidia sekta ya elimu.
Kwa upande wake mwasisi wa shirika hilo la Kulea Romie Mtenda alisema kuwa shirika lake limekuwa likisaidia sekta ya elimu ambapo hiyo ni mara ya pili kutoa msaada wa vitabu katika Jimbo hilo pia wamekuwa wakitoa misaada ya kielimu.
Mtenda alisema kuwa shirika lao limekuwa likitoa misaada kwa watoto yatima, wajane na watu wasishio kwenye mazingira magumu ikiwa ni pamoja na kuwasaidiaada, malazi, makazi na huduma nyingine za kijamii.   
Naye mwalimu mkuu wa Mdaula Komba alisema kuwa vitabu hivyo vitasaidia wanafunzi kwa ajili ya kujifunza Sayansi ambayo imekuwa ndiyo somo kuu kwa ajili ya wataalamu ambao wanabuni vitu mbalimbali ambavyo hutumiwa na watu.
Komba alisema kuwa msaada huo umekuja wakati mwafaka kwani wanafunzi wamekuwa na mahitaji ya vitabu vya Sayansi kwa ajili ya kujisomea hivyo vitawasaidia sana kupenda masomo hayo ambayo ni Bioloji, Sayansi na Hesabu. Vitabu hivyo vimetolewa kwa mgawanyo wa tarafa tano ambazo ni Chalinze vitabu 998, Msoga 910, Miono 610, mSata 610 na Kwaruhombo 610.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment