Sunday, February 21, 2016

WAZIRI SIMBACHAWENE ALIPA NENO SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA

Na John Gagarini, Kibaha
SERIKALI imesema kuwa itaangalia upaya uendeshaji wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC) ili lizalishe liweze kujiendesha kwa ufanisi badala ya kuitegemea serikali ili kuboresha maslahi ya wafanyakazi wake na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene alipotembelea Shirika hilo kujionea utendaji kazi wake na na kuongea na wafanyakazi kujua changamoto zinazowakabili na kusema kuwa linapaswa kujiendesha kwa faida na si kuwa tegemezi.
Simbachawene alisema kuwa Shirika hilo la Umma lilianzishwa kwa lengo la kusaidia wananchi hasa wale wa vijijini kwa wakati ule lakini linapasw akubadilika kutokana na wakati na kuacha mifumo ya uendeshaji wa kizamani ambayo haiendani na hali halisi ya wakati uliopo hivyo kushindwa kunufaisha watumishi na wananchi.
“Haiwezekani Shirika kama hili lenye rasilimali na vyanzo vingi vya mapato ikiwa ni pamoja na ardhi kubwa linakuwa na watumishi ambao ni maskini huku wakikosa stahiki zao za kimsingi na kufanya liyumbe ni jambo la kusikitisha sana hivyo serikali itakaa na kuangalia njia za kuweza klirudisha kwenye uhalisia wake,” alisema Simbachawene.
Alisema kuwa Shirika linayumba kw asababu hakuna mipango mikakati ya kujiendesha kisasa kwani maono yake yanaonekana bado ni ya kizamani kwa kuendelea kudeka kwa serikali licha ya kuwa na fursa nyingi zianazolizunguka.
“Mbali ya mfumo wa uendeshaji kuwa na matataizo mengi pia wafanyakazi wamelalamika sana juu ya maslahi yao ikiwa ni pamoja na malipo ya kazi z aziada, kupandishwa madaraja na maslahi mengine nitakuja na majibu ya maswali yenu pia tume itaundwa kila sekta ili kubaini matatizo yaliyopo na kuyafanyia kazi,” alisema Simbachawene.
Kwa upanade wake mwenyekiti wa bodi ya Shirika Patrick Makungu alisema kuwa watazifanyia kazi changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wafanyakazi ambazo zinawafanya watumishi washindwe kutoa huduma bora.
Naye mkurugenzi wa Shirika la Elimu Kibaha Dk Cyprian Mpemba alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinawafanya washindwe kutoa huduma bora ikiwa ni pamoja na kuwa na mahitaji ya fedha kiasi cha shilingi bilioni 6.5 kwa ajili ya uendesheaji.
Dk Mpemba alisema kuwa mbali ya changamoto hizo wamepata mafaniko kupitia mfumo wa kieletroniki wa ukusanyaji wa mapato ya Hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Tumbi ambayo iko chini ya Shirika hilo kufanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni 3,000,000 toka 300,000 kwa siku.
Waziri alitembelea Hospitali hiyo, aliangalia mfumo wa ukusanyaji mapato wa kieletroniki uliobuniwa na shirika hilo, kampuni ya ufugaji kuku ya Organia, Shirika hilo lilianzishwa miaka zaidi ya 40 iliyopita na nchi za NORDIC likiwa na lengo la kupambana na adui watatu ambao ni ujinga, umaskini na maradhi na lina wafanyakazi zaidi ya 900 na lina miliki Hospitali ya Tumbi, Chuo cha Waganga wasaidizi, Chuo cha Ufundi Stadi VETA, Shule z a sekondari Kibaha wavulana na Wasichana, Tumbi, shule ya msingi Tumbi na awali     

 MWISHO

No comments:

Post a Comment