Na John Gagarini, Kibaha
Moja ya wafanyabiashara hao ambao ni Veronica Damiani akizungumza
na waandishi wa habari alisema kuwa wanashangaa Halmashauri hiyo kuwavunjia
vibanda vyao bila ya kuwaandikia barua ya kuwataka wasifanye biashara zao.
Damiani alisema kuwa wao wanajua serikali kabla ya kufanya
kitu lazima itoe taarifa ya maandishi kabla ya kufanya jambo lolote lakini wao
wanashangaa kuondolewa bila ya kupewa barua ya kuwahamisha katika eneo hilo.
“Sisi hatukatai kuondoka ila wangetupa taarifa juu ya
kututaka tuondoke katika eneo hili na siku chache zilizopita walikuja
wakatuambia kuwa tuendelee na biashara wakati majadiliano yanaendelea lakini
tunashangaa jana wamekuja na migambo na kutubomolea vibanda vyetu huku wakitupa
masaa matatu kwa ajili ya kuhama,” alisema Damiani.
Alisema kuwa sasa wao watenda wapi kufanya biashara kwani
maji wanayouza wengine wamekopa mikopo kwenye taasisi za kifedha kwa lengo la
kujipatia kipato chao na familia zao ambapo wengine ni wajane.
“Tunakopa fedha kwa ajili ya kufanyabiashara hizi sasa
tutarejeshaje fedha tulizokopa tunaomba viongozi wa ngazi za juu watuangalie
kwa jicho la huruma hatuna kipato kingine zaidi ya biashara hizi ambazo
zinatusaidia kuwasomesha watoto wetu kuanzia shule za msingi, sekondari na vyuo,”
alisema Damiani.
Kwa upande wake Mhandisi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha
Dismas Marango akijibu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Gladys
Dyamvunye alisema kuwa wafanyabiashara hao walikuwa wakifanyabiashara zao kimakosa
kwani hawakuwa na kibali chakufanyia biashara kwenye eneo hilo.
Marango alisema kuwa hawakuwapa barua kwani sehemu hiyo si
kwa ajili ya kufanyabiashara na kwamba mabanda hayo yanaonekana kama uchafu na
waliwapa taarifa kwa maneno wiki tatu zilizopita za kuwataka waondoke kwenye
eneo hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment