Na John Gagarini, Kibaha
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha
mwenyekiti wa chama hicho Hussein Kijazi alisema kuwa kumekuwa na lawama nyingi
kwa madereva wa Bodaboda kukiuka taratibu za uendeshaji hali ambayo inaweza
kuchangia kuongezeka kwa ajali.
Kijazi alisema kuwa ili kuwadhibiti madereva wanaokiuka
taratibu wameona bora waanzishe utaratibu huo ili iwe rahisi kuwabaini wale
wanokwenda kinyume cha sheria na kuwachukulia hatua za kisheria.
“Utaratibu huu tunatarajia utaanza wakati wowote kuanzia sasa
kwani kumekuwa na malalamiko mengi toka kwa watu mbalimbali wakilalamika kuwa
madereva hao wanavunja sheria na kuwa moja ya chanzo cha ajali,” alisema
Kijazi.
Alisema kuwa mtu akiona kuna tataizo kwa dereva fulani
anataja tu namba na wao watafuatilia ni dereva gani mwenye hiyo namba kisha
chama kitamwita na kumpa adhabu inayostahili kutokana na kosa lake.
“Makoti hayo yanayongaa hata nyakati za usiku yatatusaidia
kuwabaini madereva wanaokiuka utartibu wetu ambao tumejiwekea kwani baadhi ya
watu wanalalamika kuwa madereva wengine wanajihusisha na vitendo vya uhalifu
lakini wakiwa na makoti hayo itakuwa ni vigumu kuvunja taratibu kwani lazima
watajulikana na wataadhibiwa,” alisema Kijazi.
Aidha wameipongeza serikali kwa kufuta baadhi ya kodi
zikiwemo zile za TRA 90,000, Motor Vehicle 50,000 na kodi ambazo zilikuwa ni
kero kwao. Chama hicho kinawanachama 400 na wamiliki zaidi ya 100 na wana vituo
13 na kina lengo la kusaidia wakati wa matatizo ikiwa ni pamoja na kufiwa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment