Na Mwandishi Wetu, Kibaha
Mbali ya kumshangaa kukaa na maiti muda mrefu pia
walimshangaa bibi huyo kumsafisha mwanae kwa taratibu za dini ya Kiislamu jambo
ambalo ni kinyume kwani huwa linafanywa na wanaume.
Tukio hilo lilitokea Fabruari 24 majira ya mchana ambapo
Mwanae Kassimu alifariki majira ya saa nane hapo nyumbani kwake baada ya
kudaiwa kuwa alikuwa anaumwa.
Wakizungumza na waandishi wa habari majirani wa Bibi huyo ambao
hawakutaka kutajwa majina yao magazetini walisema kuwa wameshangazwa na kitendo
hicho cha kukaa na maiti kwa muda wote huo bila kuomboleza kama ilivyo kwa watu
wanaofiwa ambao hulio kuashiria kuwa kuna msiba.
Walisema kuwa kilichowashangaza ni jinsi gani bibi huyo
alipomfanyia usafi mwanae wa kiume jambo ambalo ni kinyume na taratibu za dini
ya Kiislamu hali ambayo ndiyo imezua maswali mengi.
Alisema marehemu alipaswa kufanyiwa taratibu za kidini na
mwanaume na si mwanamke kama alivyofanya bibi huyo ambaye watu wengi
wamemshangaa kwa ujasiri huo.
“Inasikitisha sana kuona bibi huyu anafanya vitu kama hivyo
ndiyo maana kumekuwa na maneno mengi kutokana na kifo cha mwanae kutokana na
alivyofanya na pia haonyeshi kusikitika kifo cha mwanae tofauti na misiba
mingine,” walisema majirani hao.
Kwa upande wake Bibi huyo akizungumza na waandishi wa habari
nyumbani kwake alisema kuwa mwanae alilogwa kwa kutupiwa jini na watu ambao
hawaipendi familia yake na kusababisha kifo hicho.
Mchenga alisema kuwa siku ya tukio hilo mwanae alikuwa tu
nyumbani nay eye alikuwa akiendelea na shughuli zake na kushangaa kuona mwanae
hana uchangamfu.
“Ilipofika mchana mwanangu alifariki na kabla hajafariki
tulikubaliana nikifa mimi yeye ataniosha na akifa yeye mimi nitamwosha ndiyo
sababu ya mimi kufanya hivyo,” alisema Mchenga.
Alisema kuwa anashangaa kuona watu wanataka kumfanyia fujo
nyumbani kwake na kusema kuwa watu wanasema maneno mengi juu ya kifo cha mwanae
huyo.
Kutokana na watu kujazana nyumbani kwa bibi huyo ilibidi
jeshi la polisi kuuchukua mwili wa marehemu majira ya saa 3 usiku na baadaye
walirudi tena majira ya saa tano kasoro na kumchukua bibi huyo kutokana na
kuhofia usalama wake kwani watu walikuwa wakimzonga na kumzomea, Jeshi la
polisi limethibitisha kutokea tukio hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment