Na John Gagarini, Kibaha
Mshindi huyo akizungumza na wandishi wa habari mjini Kibaha
baada ya kupewa tuzo na Dk Kikwete wakati wa sherehe za kuzindua jengo la CCM
Kibaha Mjini lililojengwa na Mbunge wa Jimbo hilo Silvestry Koka alisema kuwa kuthamini mchango wa wanachama au
makada wake ni moja ya njia za kuwapa motisha ili waendelee kukitetea chama
chao.
Ngombe alisema kuwa anamshukuru mwenyekiti kuliona hilo na
kutaka viongozi wa maeneo mengine kuiga utaratibu huo wa kuthamini mchango wa
wanaccm waliosababisha chama kushinda au kukipigania.
“Tunamshukuru mwenyekiti kwa kutupa tuzo na kuwataka viongozi
wa maneo mbalimbali kuwaenzi wanaccm waliojitolea kukipigania chama bila ya
kuchoka na mimi nimekuwa nikivaa sare ya chama kila siku ambapo kwa sasa nina
miaka tisa mfululizo bila ya kuacha,” alisema Ngombe.
Alisema kuwa anajisikia fahari kupewa tuzo hiyo ya uvaaji wa
sare kwani imempa moyo wa kuendelea kukipigania chama licha ya kukumbwa na
changamoto nyingi kutoka kwa wapinzani wao vyama vingine.
“Kuvaa kwangu sare za chama kwenye eneo lango la kufanyia
kazi imekuwa chachu ya chama chake kufanya vizuri kwani watu wamekuwa
wakinifahamu kwa uvaaji wangu huu na nimekuwa nikiwakabili wapinzani wetu kwa
hoja kwani wakishaniona wamekuwa wakinitania na mimi ndo ninapopata muda wa
kuwapa sera za chama huku wengine wakijiunga na chama kupitia kwangu kwani
naonyesha msimamo wangu wa chama,” alisema Ngombe.
Aidha alisema kuwa anashangazwa na baadhi ya wanaccm kuogopa
kuvaa sare za chama kwani hata kwenye vikao wengine wamekuwa hawavai licha ya
kutakiwa kuvaa wanapokuwa kwenye mikutano na vikao vya chama.
Alishauri tuzo hizo ziambatane na fedha kidogo kwa ajili ya
kuongeza motisha kwa wanaofanya vizuri kwneye nyanja mbalimbali za kukipigania
chama bila ya kuwa na woga wa aina yoyote tofauti na ilivyo wanachama au
wapenzi wa chama.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment