Thursday, February 25, 2016

MSHINDI UVAAJI SARE ZA CCM ALONGA

Na John Gagarini, Kibaha
MSHINDI wa Uvaaji wa sare za Chama Cha Mapinduzi (CCM)Kibaha Mjini mkoani Pwani Said Ngombe amempongeza mwenyekiti wa chama hicho Dk Jakaya Kikwete kwa kutaka kuenziwa watu wanaokifanya chama kishinde kwenye chaguzi mbalimbali.
Mshindi huyo akizungumza na wandishi wa habari mjini Kibaha baada ya kupewa tuzo na Dk Kikwete wakati wa sherehe za kuzindua jengo la CCM Kibaha Mjini lililojengwa na Mbunge wa Jimbo hilo Silvestry Koka  alisema kuwa kuthamini mchango wa wanachama au makada wake ni moja ya njia za kuwapa motisha ili waendelee kukitetea chama chao.
Ngombe alisema kuwa anamshukuru mwenyekiti kuliona hilo na kutaka viongozi wa maeneo mengine kuiga utaratibu huo wa kuthamini mchango wa wanaccm waliosababisha chama kushinda au kukipigania.
“Tunamshukuru mwenyekiti kwa kutupa tuzo na kuwataka viongozi wa maneo mbalimbali kuwaenzi wanaccm waliojitolea kukipigania chama bila ya kuchoka na mimi nimekuwa nikivaa sare ya chama kila siku ambapo kwa sasa nina miaka tisa mfululizo bila ya kuacha,” alisema Ngombe.
Alisema kuwa anajisikia fahari kupewa tuzo hiyo ya uvaaji wa sare kwani imempa moyo wa kuendelea kukipigania chama licha ya kukumbwa na changamoto nyingi kutoka kwa wapinzani wao vyama vingine.
“Kuvaa kwangu sare za chama kwenye eneo lango la kufanyia kazi imekuwa chachu ya chama chake kufanya vizuri kwani watu wamekuwa wakinifahamu kwa uvaaji wangu huu na nimekuwa nikiwakabili wapinzani wetu kwa hoja kwani wakishaniona wamekuwa wakinitania na mimi ndo ninapopata muda wa kuwapa sera za chama huku wengine wakijiunga na chama kupitia kwangu kwani naonyesha msimamo wangu wa chama,” alisema Ngombe.
Aidha alisema kuwa anashangazwa na baadhi ya wanaccm kuogopa kuvaa sare za chama kwani hata kwenye vikao wengine wamekuwa hawavai licha ya kutakiwa kuvaa wanapokuwa kwenye mikutano na vikao vya chama.
Alishauri tuzo hizo ziambatane na fedha kidogo kwa ajili ya kuongeza motisha kwa wanaofanya vizuri kwneye nyanja mbalimbali za kukipigania chama bila ya kuwa na woga wa aina yoyote tofauti na ilivyo wanachama au wapenzi wa chama.
Mwisho.   

No comments:

Post a Comment