Na John Gagarini, Kibaha
Tukio hilo lilitokea Fabruari 25 majira ya saa 9 alfajiri
katika mtaa wa Tangini baada ya marehemu akiwa na mwenzake ambaye alikimbia
kuvunja na kutoa mchele huo kilogramu 100 na mafuta ya lita tatu galoni mbili.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha
mwenyekiti wa mtaa huo Leons Karoli alisema kuwa watu hao waligunduliwa na
baadhi ya madereva wa Bodaboda waliokuwa wakipita kwenye eneo la tukio na
kuwakuta watuhumiwa hao wakiwa na vitu hivyo wakiwa wamevipakia kwenye pikipiki
ya marehemu aina ya Boxer.
“Mashuhuda walisema kuwa marehemu alikuwa ndani ya hilo duka na
kujifanya kama ndiye mwenye duka akijifanya ndiyo analifungua lakini watu
walikuwa na wasiwasi kwani ilikuwa ni asubuhi sana jambo ambalo si la kawaida
kwa mmiliki huyo kulifungua muda huo huku ambaye mmiliki wake ni Mmbando,”
alisema Karoli.
Karoli alisema kuwa baada ya watu kuwa na wasiwasi
waliwasiliana na watu kujaa kisha kuanza kumpiga marehemu hadi alipopoteza
fahamu na mwenzake alifanikiwa kutoroka kwa kukimbia na kumwacha mwenzake
ambaye alibainika kuwa ni muuza matunda pia ni dereva bodaboda.
“Tulifanya mawasiliano na polisi na kuwajulisha kuwa kuna
mwizi kakamatwa lakini kabla hawajafika watu hao wenye hasira walimpiga kisha
kumchoma moto kwa kutumia mafuta ya petroli na kusababisha kifo chake,” alisema
Karoli.
Alisema kuwa marehemu alikuwa na begi ambalo lilikuwa na
vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na mkasi mkubwa unaotumika kukatia makufuli,
nondo, vocha za simu pamoja na fedha taslimu kiasi cha shilingi 150,000.
Jeshi la polisi mkoani Pwani lilithibitisha kutokea tukio
hilo na kuwataka wananchi kutojichukulia sheria mkononi kwa kutoa taarifa
polisi kwa hatua zaidi za kisheria na si kuwauwa watuhumiwa wa matukio ya
kihalifu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment