Na John Gagarini, Pwani
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu
diwani wa kata hiyo Hussein Malota alisema kuwa lengo la kukutana na pande hizo
ni kujadili jinsi gani ya kukabili changamoto hizo ambazo zimekuwa
zikisababisha mapigano.
Malota alisema kuwa wiki tatu zilizopita kulitokea ugomvi
baina ya pande hizo mbali baada ya wafugaji kudaiwa kuachia ngombe na kula
mazao ya wakulima hali ambayo ili sababisha vurugu za hapa na pale.
“Tayari tumeunda kamati za maridhiano za wakulima watano na
wafugaji watano ili kutunga sheria ndogondogo ambazo endapo mmoja atakiuka ataadhibiwa
kulingana na makubaliano ya kamati hiyo ili kudhibiti wale watakaokiuka
makubaliano hayo,” alisema Malota.
Alisema kuwa tatizo kubwa ni baadhi ya wafugaji wapya
wanaoingia kwenye vijiji mbalimbali kwani hawajui taratibu mara waingiapo
kwenye maeneo ya wenyeji hali ambayo inasababisha migogoro baina ya pande hizo.
“Tumeunda kamati hizi ili zitunge sheria ambazo zitawaabana
wale watakaokiuka kwani wajumbe wa hizo kamati watawajulisha wenzao makubaliano
yaliyoafikiwa lengo likiwa ni kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji waishi
kwa amani kama jamii moja,” alisema Malota.
Aidha alisema kuwa changamoto nyingine walioiona ni baadhi ya
wafugaji kuwaachia watoto wachunge mifugo hiyo ambayo ni makundi makubwa na
kushindwa kuyamudu wakati wakichunga na kusababisha matatizo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment