Tuesday, February 16, 2016

MADIWANI KUHAKIKI MAPATO YA STENDI

Na John Gagarini, Kibaha
MADIWANI wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha wanatarajiwa kusimamia utaratibu wa mapato kwenye stendi kuu ya mabasi ya Maili Moja ili kuhakiki ni magari mangapi ya abiria yanayolipa ushuru kwenye stendi hiyo.
Utaratibu huo ulipitishwa kwenye baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo ukiwa na lengo la kuhakikisha kuwa fedha zinazopatikana kwenye chanzo hicho kikubwa cha mapato cha Halmashauri hiyo.
Akizungumza kwenye kikao hicho mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Leonard Mloe alisema kuwa madiwani hao watakaa kituoni hapo ili kupata ukweli wa magari mangapi yanayolipa ushuru yanapopita hapo stendi.
“Tumeamua kufanya hivyo kwani mapato yanayopatikana kwa sasa hayana usahihi kwani idadi ya magari yanayolipa ushuru ni machache huku magari yanayopita hapo ni kubwa hivyo kukaa hapo kutatusaidia kujua ukweli wa mapato halisi ya stendi,” alisema Mlowe.
Mlowe alisema kuwa wanataka wakadirie mapto kwa uhakika na si kubahatisha kwani kwa sasa hawaridhiki na mapato yanayopatikana kwa sasa hivyo wameamua madiwani wake hapo ili kupata majibu sahihi.
“Hichi ni moja ya chanzo chetu cha mapato cha uhakika hivyo lazima tujue tunapata nini na kujua ni magari ya abiria ni mangapi yanayolipa ushuru wa stendi kwani iatatusadia kuwa na uhakika wa mapato ya chanzo hicho,” alisema Mloe.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Tumbi Hemed Chanyika alisema kuwa mapato ya stendi hayafahamiki undani wake kwani inaonekana baadhi ya watu wanatumia risiti feki za ushuru wa stendi kujinufaisha.
Chanyika alisema kuwa kwa madiwani hao kukaa hapo itasaidia sana kwani idadi ya magari ya abiria yanayoingia na kutoka kwenye stendi hiyo ambapo mabasi madogo yanalipia kiasi cha shilingi 500 na makubwa 1,000 kila yanapoingia na kutoka.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment