MWENGE wa Uhuru umeanza mbio zake Mkoani Pwani ukitokea Mkoani Morogoro ambapo utapitia miradi 126 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi trilioni 8.5.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge alipoupokea Mwenge huo eneo la Bwawani Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo, kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima.
Kungenge alisema kuwa kati ya miradi hiyo 18 itawekewa mawe ya msingi 22 itazinduliwa 86 itakaguliwa.
"Miradi hiyo imefanikiwa kutokana na Rais kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na ushirikiano kati ya viongozi, wananchi na wadau wa maendeleo katika kutafuta fedha hasa ikizingatiwa Pwani ni Mkoa wa kimkakati,"alisema Kunenge.
Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge Godfrey Eliakim Mzava alisema kuwa wanapofika kwenye miradi ya maendeleo wakute taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo pia nyaraka zote za msingi zinazoeleza utekelezaji wa miradi iliyoyopo na wataalamu watoe maelezo ya kina na vifaa vya upimaji ubora wa miradi viwepo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment