Akikabidhi mfano wa hundi Meneja Uhusiano wa (TFS) Johary Kachwamba kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa fedha hizo ni kusaidia mahitaji mbalimbali.
Kachwamba amesema kuwa wana misitu zaidi ya 10 yenye ukubwa wa hekari 32,000 hivyo wameona watoe pole kwa wananchi waliokumbwa na changamoto ya mafuriko.
Amesema kuwa wataendelea kushirikiana na serikali kusaidia sehemu mbalimbali zilizokumbwa na changamoto kama hizo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani ameishukuru TFS kwa kujitolea fedha hizo kwani zitaweza kusaidia wananchi hao kuweza kukabili baadhi ya mahitaji.
Kunenge amesema kuwa mbali ya kutoa fedha hizo pia wametoa eneo kwenye Kitongoji cha Chumbi B ambapo wananchi wa Muhoro watahamishiwa hapo.
Amesema wanaishukuru TFS katika jitihada za kulinda na kutoa elimu juu ya kuhifadhi mazingira na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala.
Aidha amesema wanashauri wananchi kuondoka kwenye eneo ambalo ni mkondo wa Bonde la Mto Rufiji na wananchi wakae maeneo ambayo si hatarishi kwa mafuriko.
No comments:
Post a Comment